Donald Trump amesema amekubali pendekezo la chombo cha utangazaji cha Marekani Fox News kufanya mdahalo na Makamu wa Rais Kamala Harris tarehe 4 Septemba.
Mdahalo kati ya rais wa zamani na rais aliyeko madarakani Joe Biden ulikuwa umeratibiwa kwenye chombo hasimu cha ABC News Septemba 10 na Bi Harris alikubali kuchukua nafasi ya Bw Biden.
Lakini Bw Trump alisema mdahalo wa ABC "ulikatizwa" na kuondoka kwa Bw Biden kwenye kinyang'anyiro hicho. Bi Harris bado hajatoa maoni juu ya pendekezo jipya la Fox News.
Wagombea hao wawili watakuwa debeni kuwania kiti cha urais mnamo tarehe 8 Novemba, baada ya Bi Harris kuchaguliwa rasmi kama mgombea wa chama cha Democratic siku ya Ijumaa.
0 Comments