RAIS MWINYI:SMZ ITAHAKIKISHA MUUNGANO UNAENDELEA KUIMARIKA.

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeahidi Kuendelea kutoa Ushirikiano  Kuhakikisha Muungano  unaimarika  kufikia dhamira ya Waasisi  wake  ya kudumisha Uhuru,Umoja na Mshikamano wa Watanzania. 


Rais Dkt.Mwinyi amesema hayo   katika hafla ya Kutunuku Nishani za Kumbukumbu ya Muungano ilioambatana na  Uzinduzi wa Kitabu cha MWALIMU JULIUS NYERERE PHOTOGRAPHIC JOURNEY cha  Historia ya Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  uliofanyika Ikulu  ya Chamwino, Dodoma.

Ameeleza kuwa Watanzania Wana kila sababu ya kudumisha Muungano kwani ni Tunu ya Taifa  ya kujifaharisha nayo na ni kielelezo cha Muungano wa Mafanikio Barani Afrika.


Rais Dkt,Mwinyi  amesema Waasisi Mwalimu Julius Nyerere na   Mzee Abeid  Karume walikuwa na dhamira thabiti ya kuwaunganisha Watanzania Kisiasa,Kiuchumi na Kijamii kwa faida ya Vizazi vya sasa na Vijavyo Jambo linalopaswa kudumishwa na kila Mtanzania.

Halikadhalika Rais Dkt , Mwinyi amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa Juhudi anazozitekeleza za kumaliza Changamoto za Muungano kupitia Vikao  vya Majadiliano  hadi kubakia  Changamoto Tatu  hivi sasa Miongoni mwa  25 zilizokuwepo awali.



Aidha amesema Kitabu hicho kitawasaidia Watanzania waliozaliwa Baada ya Muungano  Kujifunza na kumtambua Muasisi Huyo wa Muungano na faida  ya Muungano huo tangu Kuasisiwa kwake Miaka 61iliyopita.

Kwa upande mwingine Rais Dkt, Mwinyi ameipongeza Kazi nzuri iliofanywa na Watunzi wa Kitabu hicho ilioonesha kuthamini Mchango wa  Baba wa Taifa na kutoa Rai ya kuchapishwa kwa wingi kopi za Kitabu hicho na kupatikana katika Maktaba Kuu zote hapa Nchini pamoja na  kwenye Mitandao ya Kijamii.

Kitabu hicho kimezinduliwa wakati Watanzania wanaadhimisha Miaka 61 ya Mafanikio ya Muungano wa Tanzania.

Post a Comment

Previous Post Next Post