JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumatatu, 19 Mei 2025

MASHAHIDI WA MAJI DAR WAPAZA SAUTI UCHAFUZI WA MITO



Na Mussa Khalid

Mashahidi wa Maji Taka na Maji safi Mkoa wa Dar es salaam wameiomba serikali kupitia Mamlaka za usimazizi wa mazingra kusimamia Sheria ,sera na kanuni katika kuwachukulia hatua watu au viwanda vinavyofanya uharibifu wa mazingra ikiwemo kwenye mito katika maeneo mbalimbali.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Mashahidi wa Maji Mkoa wa Dar es salaam Zaharani Omary wakati waliposhirikiana na watendaji wa serikali za mitaa Kigogo na VINGUNGUTI kupofanya ziara ya kukagua mito Msimbazi,Kibangu na Tenge ili kuangalia maeneo korofi yanayotiririsha Maji yasiyomazuri katika mito hiyo.

Aidha amesema kuwa lengo lao ni kuikumbusha serikali kusaidia kutatua changamoto hiyo katika mito hiyo ambayo Maji mabaya yamekuwa yakiingia kutoka viwandani na hivyo kuathiri Wananchi.

"Tumepita katika kiwanda cha Betri Yuwasa tumekuta Kuna Maji yasiyomazuri yanatiririshwa katika mito Msimbazi,pia tumepita kiwanda Cha Nida tumekutana na kadhia hiyo na hata ushahidi wa picha upo kutokana na shida hiyo kwani Kuna baadhi ya Wananchi wanapatashida na Maji hayo"amesema Zaharani

Amesema kutokana na serikali kuwa ni sikivu inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan wanaimani watasaidia katika kufanya utatuzi wa siala hilo ili kuweza kuisaidia jamii.

Akitolea mfano kuwa kutokana na uharibifu unaofanywa na baadhi ya viwanda katika mito hiyo inasababisha mpaka viumbe hai vinavyokaa kwenye Maji kutokuwepo kutokana na kushindwa kuhimili Maji hayo yenye sumu.

Aidha amesema kuwa wataendelea kupaza sauti kila wakati ili kuhakikisha changamoto ambazo zinaikumba jamii kupitia uharibifu unaofanywa na baadhi ya watu au viwanda katika mito inapatiwa ufumbuzi.

Huo umekuwa ni muendelezo wa Mashahidi wa Maji kupita na kujionea kadhia ya uharibifu wa mazingra husuani katika rasiliali maji katika maeneo mbalimbali ili kupaza sauti Kwa kuzijulisha Mamlaka za ufanyaji maaamuzi kufanya utatuzi wa changamoto hizo.


0 comments:

Chapisha Maoni

Listen Mkisi Radio