JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumatatu, 19 Mei 2025

Mbeto amtaka Jussa atangaze sera za ACT, Maalim Seif yuko mbele ya haki


Na Mwandishi Wetu ,Zanzibar


Chama Cha Mapinduzi  kimemkanya Makamu Mwenyekiti  wa ACT  Wazalendo,  Ismail Jussa Ladhu ,kutaja  sera za chama chake na kumtaka  aache kulitumia jina la Hayati  Maalim  Seif Sharif  Hamad kama msingi wa sera.


Pia kimesisitiza iwapo ACT  hakina sera za kimaendeleo , akae kimya na kuacha kuwapumbaza wananchi kwa siasa za  porojo na uchepe.


Matamshi hayo yametamkwa na Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanziabr, Idara ya itikadi ,Uenezi na Mafunzo Khamis  Mbeto  Khamis, aliyemtaka Jussa asilitumie jina la Maalim  seif aliyetangulia mbele ya haki


Mbeto alisema kwa wananchi wa  zanzibari  hakuna hata mtu mmoja asiyejua  Jussa alikuwa rafiki  mwandani wa  Maalim seif kwa ukuruba na mnasaba wao.


Alisema wananchi wanataka  kusikia sera za ACT  , kisha wazilinganishe na sera zilizoleta  maendeleo chini  ya serikali ya Rais Dk  Hussein Ali Mwinyi .


"Kwa Chama cha siasa  makini  duniani sera huwa ndiyo dira ya ushindani  badala ya  porojo ,kejeli na matusi kama afanyavyo Jussa na wenzake" Alisema Mbeto.


Aidha  alimtaka  Jussa asiwafanye wazanzibari  kama watu wasio na  macho ya kuona  yale  yaliofanyika , au hawajui kutofautisha  maendeleo yaliokuwepo  awali na yaliopo sasa.


Mbeto alimtaka Jussa  kuelewa kuwa wazanzibari ni watu werevu mno  wana akili, maarifa na hekima hivyo hawaghilibiwi kwa porojo na siasa zake za chuki


'Wazanzibari hawako tayari    kuendelea kugawanywa kwa siasa za chuki  na hasama .Kiu yao ni  maendeleo ya nchi yao ,Umoja ,Usalama  na Ustawi  wa Amani "Alieleza


Katibu  huyo  Mwenezi  alimtaja   Jussa na wenzake mara nyingi  wamekuwa wakihubiri ubaguzi ambao kwa miaka mingi umechangia kuwagawa wananchi  wa Unguja  na Pemba


"Maalim Seif  hana sifa ya kuitwa shujaa au  jemedari wa Zanzibar. Jemedari Mkuu wa Mapinduzi  yalioleta zanzibar ukombozi  ni  Hayati Mzee  Abeid  Amani  Karume kupitia ASP  " Alisema Mbeto.


Aliongeza kusema kuwa Maalim  Seif ni atabaki kuwa kiongozj aliyekiwa na heshima  baada ya kupikwa ,kuandaliwa kisiasa na kiuongozi toka  akiwa mwanachama wa CCM.


Pia Katibu  huyo Mwenezi  alimkanya na kumueleimisha Makamu huyo Mwenyekiti  wa ACT  akimtaka aache kuvuruga  historia ya zanzibar kwa kudai  Maalim  seif ni jemedari na shujaa  wa Zanzibar.


"Maalim Seif ataheshimika kama Kiongozi  aliyewahi kuwa Waziri  wa Elimu ,Waziri  Kiongozi  pia Makamo  wa kwanza  wa Rais  SMZ si vinginevyo " Alisiaitiza  Mbeto .


Kwa upande  mwingine  Mbeto slimtaka Mwenyekiti  wa ACT  Wazalendo  Othman  Masoud  Othman ,ajiandae kushindwa katika uchaguzi mkuu ifikapo oktoba  mwaka  huu.


"Jussa  huwezi kuzifananisha sifa za uongozi alizokuwanazo  Hayati  Maalim  Seif na Othman  .Wazanzibari  wanahitaji kupata viongozi wenye maono na wapigania   maendeleo hivyo  asimlinganishe  Othman  na Maalim  Seif  "Alisema


Kadhalika  Mwenezi  huyo alisema Wazanzibari  hawawezi kutoa kura zao na kumpigia  othman  kwa nafasi ya urais kwani hata hiyo kazi ya kuwa makamo wa Rais  SMZ  imekuwa ikimshinda

0 comments:

Chapisha Maoni

Listen Mkisi Radio