Na Mwandishi Wetu ,Zanzibar
Chama Cha Mapinduzi kimemkanya Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Ismail Jussa Ladhu ,kutaja sera za chama chake na kumtaka aache kulitumia jina la Hayati Maalim Seif Sharif Hamad kama msingi wa sera.
Pia kimesisitiza iwapo ACT hakina sera za kimaendeleo , akae kimya na kuacha kuwapumbaza wananchi kwa siasa za porojo na uchepe.
Matamshi hayo yametamkwa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanziabr, Idara ya itikadi ,Uenezi na Mafunzo Khamis Mbeto Khamis, aliyemtaka Jussa asilitumie jina la Maalim seif aliyetangulia mbele ya haki
Mbeto alisema kwa wananchi wa zanzibari hakuna hata mtu mmoja asiyejua Jussa alikuwa rafiki mwandani wa Maalim seif kwa ukuruba na mnasaba wao.
Alisema wananchi wanataka kusikia sera za ACT , kisha wazilinganishe na sera zilizoleta maendeleo chini ya serikali ya Rais Dk Hussein Ali Mwinyi .
"Kwa Chama cha siasa makini duniani sera huwa ndiyo dira ya ushindani badala ya porojo ,kejeli na matusi kama afanyavyo Jussa na wenzake" Alisema Mbeto.
Aidha alimtaka Jussa asiwafanye wazanzibari kama watu wasio na macho ya kuona yale yaliofanyika , au hawajui kutofautisha maendeleo yaliokuwepo awali na yaliopo sasa.
Mbeto alimtaka Jussa kuelewa kuwa wazanzibari ni watu werevu mno wana akili, maarifa na hekima hivyo hawaghilibiwi kwa porojo na siasa zake za chuki
'Wazanzibari hawako tayari kuendelea kugawanywa kwa siasa za chuki na hasama .Kiu yao ni maendeleo ya nchi yao ,Umoja ,Usalama na Ustawi wa Amani "Alieleza
Katibu huyo Mwenezi alimtaja Jussa na wenzake mara nyingi wamekuwa wakihubiri ubaguzi ambao kwa miaka mingi umechangia kuwagawa wananchi wa Unguja na Pemba
"Maalim Seif hana sifa ya kuitwa shujaa au jemedari wa Zanzibar. Jemedari Mkuu wa Mapinduzi yalioleta zanzibar ukombozi ni Hayati Mzee Abeid Amani Karume kupitia ASP " Alisema Mbeto.
Aliongeza kusema kuwa Maalim Seif ni atabaki kuwa kiongozj aliyekiwa na heshima baada ya kupikwa ,kuandaliwa kisiasa na kiuongozi toka akiwa mwanachama wa CCM.
Pia Katibu huyo Mwenezi alimkanya na kumueleimisha Makamu huyo Mwenyekiti wa ACT akimtaka aache kuvuruga historia ya zanzibar kwa kudai Maalim seif ni jemedari na shujaa wa Zanzibar.
"Maalim Seif ataheshimika kama Kiongozi aliyewahi kuwa Waziri wa Elimu ,Waziri Kiongozi pia Makamo wa kwanza wa Rais SMZ si vinginevyo " Alisiaitiza Mbeto .
Kwa upande mwingine Mbeto slimtaka Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Othman Masoud Othman ,ajiandae kushindwa katika uchaguzi mkuu ifikapo oktoba mwaka huu.
"Jussa huwezi kuzifananisha sifa za uongozi alizokuwanazo Hayati Maalim Seif na Othman .Wazanzibari wanahitaji kupata viongozi wenye maono na wapigania maendeleo hivyo asimlinganishe Othman na Maalim Seif "Alisema
Kadhalika Mwenezi huyo alisema Wazanzibari hawawezi kutoa kura zao na kumpigia othman kwa nafasi ya urais kwani hata hiyo kazi ya kuwa makamo wa Rais SMZ imekuwa ikimshinda
0 comments:
Chapisha Maoni