JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Ijumaa, 30 Mei 2025

Mbeto : Wana CCM wameondoka Dodoma kibabe ,vifua mbele tayari kwa ushindi


 Mbeto : Wana CCM wameondoka Dodoma kibabe ,vifua mbele tayari  kwa ushindi


Na Mwandishi  Wetu, Dodoma 



Chama Cha Mapinduzi kimesema Wajumbe wake wa Mkutano  Mkuu wa  Taifa , wanaondoka katika Jiji la Dodoma huku  wakiwa wamebeba  matumaini  ya kupata  ushindi kuliko  wakati  wowote. 


Mamia  ya  Wajumbe hao  toka Mikoa  ya Tanzania Bara na Zanzibar  wameliacha Jiji Kuu hilo la Tanzania ,wakiamini chama  chao kitashinda uchaguzi  Oktoba  Mwaka huu. 


Matamshi hayo yametamkwa na Katibu  wa Kamati  Maalum  yya  NEC Zanzibar  , Idara ya itikadi , Uenezi na Mafunzo,  Khamsi Mbeto Khamis ,aliyesema  kazi iliobaki  ni kuinadi Ilani  mpya  ya CCM ya Uchaguzi   Mwaka 2025 -2030 kwa nguvu zote .


Mbeto  alisema hakuna Chama cha Siasa wala mgombea atakaehimili  kimbunga cha Kampeni  za CCM ambazo zitaanza Miezi michache ijayo toka sasa.


Alisema Uwasilishaji wa  taarifa ya matokeo ya Ilani  Uchaguzi ya Mwaka 2020-2025, tija na  mafanikio ya utekelezaji wa maendeleo  ya kisekta , kumedhihirisha nia thabit walionayo Marais ,  Dk Samia  Suluhu  Hassan na mwenzake , Dk Hussein  Ali Mwinyi .


"Wajumbe  wa Mkutano Mkuu wameondoka  Dodoma  wakiwa wamebeba vikapu vya matumaini ya ushindi . Silaha ya ushindi  wa chama cha siasa hutokana na ubora wa Ilani ,  sera  na mipango ya maendeleo " Alisema Mbeto .


Aidha, Katibu huyo Mwenezi , alisifu kazi kubwa iliiofanywa na Serikali zote mbili  katika  azma ya kutumikia wananchi na kuweka mkazo  katika utatuzi wa changamoto za  maendeleo ya kisekta. 


Alisema  matokeo  ya utekelezaji wa Ilani iliopita ya Mwaka  2020-2025 , imeelezea mafanikio ya Sekta za Afya , Elimu , Uwekezaji , Miundombinu , Nishati ya Umeme na gesi  , Ufugaji na  ukuzaji Kilimo.


 'Taifa limepiga hatua nyingi za kimaendeleo hususan  katika sekta ya Usafiri,  Mawasiliano  na Makaazi ya Nyumba  bora za  kisiasa, ujenzi  wa Masoko, Barabara ,  Shule  za Msingi na 

Sekondari ikiwemo  Ujenzi wa Vituo vya Afya na Zahanati " Alieleza 


Pia alisema  Ilani iliopita imetaja na kuonyesha mafanikio  katika ukuaji wa  Uchumi  wa Taifa , pato la Taifa,   Viwanda, Uhusiano wa Kimataifa , Diplomasia, Michezo na Siasa  pia mikopo ya  taaisis za  kimatiafa na Elimu ya juu .


Kadhalika  Mbeto  alisema taarifa katika  ilani iliopita  imeonyesha jinsi halmashauri   za wilaya zilivyoanzisha miradi ya Maji Safi na Salama ,  Barabara za Vijijini, Wilaya na Mikoa hadi  kukamilika kwake.


"Matumaini makubwa ya Wananchi yamebebwa na ilani mpya Uchaguzi wa  Mwaka huu  2025-2530 .Utekelezaji  wa mipango iliiomo katika   ilani hiyo itaipaisha na kuifanya Tanzania kuwa miongoni   mwa Nchi za uchumi  Kati "Alieleza katibu  huyo Mwenezi

0 comments:

Chapisha Maoni

Listen Mkisi Radio