JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumamosi, 24 Mei 2025

TASACO YAPOKEA MSAADA KUTOKA KWA MH. JERRY SILAA


 Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia na Mbunge wa Jimbo la Ukonga Mh .Jerry Silaa ametoa Shilingi Millioni 1na laki 7 kwa Taasisi isiyo ya Kiserikali inayohudumia jamii kwa kutoa Elimu ya huduma ndogo za kifedha (TASACO) ili kusaidia kikundi hicho Katika huduma wanayoitoa ya kukodisha,viti maturubai na vyombo kwenye shughuli mbalimbali.


Mh.Silaa ametoa Viti hivyo  Mei 23, 2025  siku ya Uzinduzi wa Taasisi hiyo  iliyopo katika Jimbo la Ukonga,Wilaya ya Ilala Jijini Dar es salaa ambapo amesema Viti hivyo vitawasaidia katika majukumu ya Kijamii na pale mtu atakapo pata tatizo.

Mh.ametoa wito kwa Viongozi wa Jimbo la Ukonga kuwakimbilia wananchi pindi wapatapo Changamoto kwasababu Mwananchi akipata Changamoto haangalii kama una pesa ila Imani Yako na kujitoa kwako wakati wa matatizo.


Aidha Mh.Silaa amewaasa Wanachama wa TaSaCo kutumia njia nzuri wa utunzaji wa Fedha ili kujihakikishia usalama wake huku akitolea Mfano kuwa mwanadamu Kila siku anachangamoto na wakati wowote anaweza akajikopesha Fedha za Taasisi na baadae akashindwa kuzirudisha.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa TaSaCo hiyo Paul Chegere amesema kuwa wao kama Taasisi wanaamini kuwa maisha yao yameunganishwa na umoja ili kujiwekea akiba na kukopeshana hatimaye kuleta maendeleo binafsi,kwa jamii na Taifa kwa ujumla.

Ameongeza kuwa tumqini lao limejikita kwenye fursa na uwezeashaji ili kizifikia fursa hizo kwa kujikwamua kiuchumi huku hatma yao ukiwa imefungamana na uwepo wa Taasisi mbalimbali zenye kutoa huduma rafikiza binafsi na Serikali kama vile Benki ,Bima za afya na nyinginezo.


Kadhalika amesema lengo na natamanio yao ni kwamba  wajasiriamali ambao hawako kwenye mifumo rasmi ya ajira ni kujiunga na bima za afya na kupata Matibabu kwa gharama nafuu.



TaSaCo ni Taasisi inayojumishwa na vikundi vya ujasiriamali vya kuweka na kukopa(vicoba) ambayo idadi yake inafikia 57,huku ukiwa na Wanachama 510 ambao wengi wamenufaika,wamefanikisha kuendesha maisha yao pamoja na kuinuka kiuchumi.


0 comments:

Chapisha Maoni

Listen Mkisi Radio