Ijumaa, 30 Mei 2025
JICA YAAHIDI KUENDELEA KUISHIKA MKONO SERIKALI YA TANZANIA-MAJALIWA
JICA YAAHIDI KUENDELEA KUISHIKA MKONO SERIKALI YA TANZANIA-MAJALIWA
_▪️JICA, Benki ya Dunia na AFDB watoa Dola za Marekani mil 516 miradi ya kilimo_
_▪️Washauri elekezi wawili Mjapan na Mtanzaniia wawekwa TIC kurahisha uwekezaji_
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) limeihakikishia Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa itaendelea kushirikiana nayo katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi.
Hatua hiyo imetokana na namna ambavyo Serikali imekuwa ikisimamia kikamilifu matumizi ya fedha mbalimbali zinazotolewa na wadau wa maendeleo likiwemo shirika hilo. Waziri Mkuu amesema “Serikali itaendelea itaendelea kusimamia ipasavyo fedha zote za maendeleo zinazoletwa nchini na kuhakikisha zinatumika kama ilivyokusudiwa.”
Ameyasema hayo juzi (Jumatano, Mei 28, 2025) alipokutana na Makamu wa Rais wa JICA, Miyazaki Katsura kwenye ukumbi wa Mikutano wa Tachibana uliopo katika hotel ya New Otani, Tokyo nchini Japan akiwa katika ziara yake ya kikazi.
Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa JICA kuendelea kutafuta wadau zaidi wa maendeleo kwa ajili upatikanaji wa fedha zitakazowezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuwafanya Watanzania kushiriki katika shughuli mbalimbali za kiuchumi.
Amesema lengo la wito huo ni kuwezesha upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kufanikisha utekelezaji wa malengo ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kuwa wanafungua milango ya kiuchumi ili wananchi wengi washiriki katika miradi mbalimbali ya maendeleo na kujiongezea kipato.
“Lengo la kutafuta wadau hawa ni kuwawezesha wananchi washiriki kwenye shughuli mbalimbali za kiuchumi, wanaotaka kuingia kwenye biashara, wanaotaka kuingia kwenye kilimo, sekta ya madini, sekta ya uvuvi na ufugaji haya ni maeneo ambayo tumeyawekea umuhimu.”
Waziri Mkuu amesema Serikali inataka kuona wananchi wanaendesha shughuli za kibiashara kukiwa na huduma zote katika mazingira rahisi, ikilinganishwa pia na utekelezaji wa miradi ya elimu, afya, miundombinu, nishati, ujenzi wa barabara pamoja na kilimo ni maeneo yanayotiliwa mkazo.
Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa JICA, Miyazaki Katsura alisema shirika lao linaendelea kutekeleza miradi mbalimbali nchini kwa kushirikiana na wadau wengine ikiwemo Benki ya Dunia katika mradi wa Ustahimilivu wa Chakula.
Makamu huyo wa Rais wa JICA alisema kuwa shirika lao litaendelea kushirikiana na Serikali katika kufanikisha miradi mbalimbali inayotekelezwa nchini ikiwemo ya kuimarisha sekta ya miundombinu na usafirishaji.
Naye, Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde ametumia fursa hiyo kuushukuru uongozi wa JICA kwa kushirikiana na Benki ya Dunia (WB), Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) kwa kutoa mikopo yenye masharti nafuu ya zaidi ya Dola za Marekani milioni 516 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kilimo.
Mheshimiwa Silinde ametaja miradi hiyo kuwa ni Mradi wa Ustahimilivu wa Chakula (TSRP) unaogharimu zaidi ya Dola za Marekani milioni 371 ambazo kati yake Benki ya Dunia imetoa Dola milioni 300.05 na JICA imetoa Dola milioni 71.09, ambapo utekelezaji wa mradi huo unafanyika kwa miaka mitano kuanzia 2025 hadi 2030.
Amesema mradi mwingine ni wa Tanzania Agricultural Inputs Support Project (TAISP) unaotekelezwa kwa ubia kati ya Benki ya Maendeleo Afrika na JICA unaohusika na utoaji wa ruzuku katika pembejeo za kilimo.
Waziri Shilinde amesema mradi huo unaotarajiwa kugharimu Dola za Marekani milioni 145, ambapo kati ya fedha hizo, JICA wanatoa dola milioni 70 na AfDB dola milioni 75.49 na ulianza kutekelezwa mwaka 2024 na utakamilika 2028. Tayari dola milioni 40 zimelipwa kwa kampuni 17 kwa ajili ya usambazaji wa mbolea.
Waziri Silinde amesema fedha hizo zimetolewa baada ya wadau hao kuridhishwa na namna ambavyo Serikali inasimamia sekta ya kilimo kwa mafanikio makubwa. Hata hivyo amewaomba wawekezaji na wafanyabiashara wa Japan waje kuwekeza katika kilimo cha umwagiliaji hususan kwenye teknolojia ya umwagiliaji.
Naye, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Zanzibar, Ali Mohamed Ameir amesema katika vikao hivyo amewahakikishia wawekezaji na wafanyabiashara wa Japan uwepo wa mazingira wezeshi ya kutekeleza majukumu yao Zanzibar ikiwemo hali ya amani na utulivu.
Pia, Mheshimiwa Ameir ametumia fursa hiyo kuiomba JICA kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika kukamilisha miradi miwili ya ujenzi ikiwemo upanuzi wa soko na jiko la samaki katika eneo la Malindi hususani kutoa vifaa kwa wafanyabiashara pamoja na mradi wa usambazaji maji mijini katika Mkoa wa Mjini Magharibi. Miradi yote inatekelezwa kwa awamu ya pili.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Gilead Teri ameishukuru Serikali ya Japan kupitia JICA kwa kugharamia washauri elekezi wawili ambao watakuwa kiungo kati ya wawekezaji na wafanyabiashara wa Japan na Tanzania.
Amesema washauri hao elekezi ambao watakuwepo TIC mmoja ni Mtanzania na mwingine Mjapani watakuwa na majukumu ya kutoa taarifa za namna ya kufanikisha uwekezaji kati ya Tanzania na Japan.
“Lengo la huyu mwelekezi kutoka Japan ni kuzungumza na kusaidia makampuni na wawekezaji kutoka Japan kupata taarifa za namna ya kuja kuwekeza Tanzania na huyu wa Tanzania ni kusaidia Watanzania wote wanaotaka kuuza bidhaa zao Japan waweze kupata usaidizi kupitia kituo cha uwekezaji.”
Awali, Meneja Uenezi na Masoko wa Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA), Khamis Dunia alisema ushiriki wa Tanzania kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Osaka (World Expo Osaka 2025) yanayoendelea nchini Japan umeiwezesha mamlaka yao kutangaza fursa za uwekezaji na biashara zilizopo Zanzibar.
Alisema mbali na maonesho hayo, pia kitendo cha kushiriki katika mikutano iliyomhusisha Waziri Mkuu pamoja na wawekezaji na wafanyabiashara wakubwa wa Kijapan vilivyofanyika jijini Tokyo alipata fursa ya kuelezea vipaumbe vya uwekezaji vilivyopo Zanzibar ikiwemo uchumi wa buluu na utalii jambo ambalo liliwavutia wawekezaji hao ambao tayari baadhi yao wameonesha nia ya kuwekeza Zanzibar.
Mbeto : Wana CCM wameondoka Dodoma kibabe ,vifua mbele tayari kwa ushindi
Mbeto : Wana CCM wameondoka Dodoma kibabe ,vifua mbele tayari kwa ushindi
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Chama Cha Mapinduzi kimesema Wajumbe wake wa Mkutano Mkuu wa Taifa , wanaondoka katika Jiji la Dodoma huku wakiwa wamebeba matumaini ya kupata ushindi kuliko wakati wowote.
Mamia ya Wajumbe hao toka Mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar wameliacha Jiji Kuu hilo la Tanzania ,wakiamini chama chao kitashinda uchaguzi Oktoba Mwaka huu.
Matamshi hayo yametamkwa na Katibu wa Kamati Maalum yya NEC Zanzibar , Idara ya itikadi , Uenezi na Mafunzo, Khamsi Mbeto Khamis ,aliyesema kazi iliobaki ni kuinadi Ilani mpya ya CCM ya Uchaguzi Mwaka 2025 -2030 kwa nguvu zote .
Mbeto alisema hakuna Chama cha Siasa wala mgombea atakaehimili kimbunga cha Kampeni za CCM ambazo zitaanza Miezi michache ijayo toka sasa.
Alisema Uwasilishaji wa taarifa ya matokeo ya Ilani Uchaguzi ya Mwaka 2020-2025, tija na mafanikio ya utekelezaji wa maendeleo ya kisekta , kumedhihirisha nia thabit walionayo Marais , Dk Samia Suluhu Hassan na mwenzake , Dk Hussein Ali Mwinyi .
"Wajumbe wa Mkutano Mkuu wameondoka Dodoma wakiwa wamebeba vikapu vya matumaini ya ushindi . Silaha ya ushindi wa chama cha siasa hutokana na ubora wa Ilani , sera na mipango ya maendeleo " Alisema Mbeto .
Aidha, Katibu huyo Mwenezi , alisifu kazi kubwa iliiofanywa na Serikali zote mbili katika azma ya kutumikia wananchi na kuweka mkazo katika utatuzi wa changamoto za maendeleo ya kisekta.
Alisema matokeo ya utekelezaji wa Ilani iliopita ya Mwaka 2020-2025 , imeelezea mafanikio ya Sekta za Afya , Elimu , Uwekezaji , Miundombinu , Nishati ya Umeme na gesi , Ufugaji na ukuzaji Kilimo.
'Taifa limepiga hatua nyingi za kimaendeleo hususan katika sekta ya Usafiri, Mawasiliano na Makaazi ya Nyumba bora za kisiasa, ujenzi wa Masoko, Barabara , Shule za Msingi na
Sekondari ikiwemo Ujenzi wa Vituo vya Afya na Zahanati " Alieleza
Pia alisema Ilani iliopita imetaja na kuonyesha mafanikio katika ukuaji wa Uchumi wa Taifa , pato la Taifa, Viwanda, Uhusiano wa Kimataifa , Diplomasia, Michezo na Siasa pia mikopo ya taaisis za kimatiafa na Elimu ya juu .
Kadhalika Mbeto alisema taarifa katika ilani iliopita imeonyesha jinsi halmashauri za wilaya zilivyoanzisha miradi ya Maji Safi na Salama , Barabara za Vijijini, Wilaya na Mikoa hadi kukamilika kwake.
"Matumaini makubwa ya Wananchi yamebebwa na ilani mpya Uchaguzi wa Mwaka huu 2025-2530 .Utekelezaji wa mipango iliiomo katika ilani hiyo itaipaisha na kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa Nchi za uchumi Kati "Alieleza katibu huyo Mwenezi
Vijana 26 Kushiriki progranu ya Mandela Washington Fellowship 2025 nchini Marekani
Vijana 26 Kushiriki progranu ya Mandela Washington Fellowship 2025 nchini Marekani
Vijana waliochaguliwa kushiriki progranu ya Mandela Washington Fellowship kwa mwaka 2025, wamekumbushwa kuwa fursa waliyoipata haikuja kwa bahati, isipokuwa kutokana na majukumu wanayoyafanya ambayo yana mchango mkubwa kwa jamii.
Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa wakati anawapa nasaha za kuwaaga vijana hao 26 jijini Dodoma Mei 30, 2025.
Balozi Mussa aliwataka kutumia fursa hiyo kujifunza mambo mapya kwa kuwa nchi wanayokwenda imeendelea kiuchumi na kiteknolojia duniani na itawapa fursa pia ya kukutana na raia wa mataifa mbalimbali wenye uzoefu na mila tofauti.
Vijana hao ambao wanatarajiwa kwenda nchini Marekani Juni na kurejea Agosti 2025, wametakiwa kulitangaza jina la Tanzania kwa watu watakaokutana nao. "Mtalitangaza jina la nchi yetu kwa kuheshimu sheria za nchi mnayokwenda, kutangaza utamaduni mzuri wa Tanzania na kuelezea kwa ufasaha mambo makubwa na mazuri ya nchi kama vile mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama, maziwa, mito na maendeleo ya miundombinu", Balozi Mussa alisema.
Balozi Mussa alisema kuwa kuwepo kwao katika programu hiyo ni kielezo cha uhusiano mzuri wa kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na Marekani ambao umedumu tokea ulipoanzishwa mwaka 1961.
Pogranu ya Mandela Washington Fellowship ilizinduliwa mwaka 2014 na hadi sasa vijana 6500 kutoka nchi za Afrika wamefaidika na mpango huo ambao unalenga kuwajengea uwezo vijana, kupata mbinu na ujuzi wa uongozi utakaosaidia kuleta mabadiliko chanya ya kiuchumi, kisiasa na kijamii barani Afrika.
WAKULIMA WA PARACHICHI WAPONGEZA RUZUKU YA MBOLEA
Wakulima wa parachichi mkoani Njombe wameishukuru Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwapatia mbolea ya ruzuku ambayo imewasaidia kuongeza tija na uzalishaji katika zao hilo.
Wakizungumza na wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) walipotembelea Chama cha Msingi cha Ng’anda AMCOS na kampuni ya mkulima wa parachichi ya Avo Nemes Green Limited, tarehe 28 Mei, 2025, wakulima hao walisema ruzuku hiyo imepunguza gharama za uzalishaji na kuwawezesha kuajiri nguvu kazi zaidi kwenye mashamba yao.
Mkulima mkubwa wa parachichi, Bw. Stephen Mlimbila, alieleza kuwa kupitia ruzuku hiyo, amepunguza gharama na fedha alizokuwa akizitumia kununua mbolea sasa zimeelekezwa kwenye ulipaji wa vibarua wanaohudumia shamba lake lenye ukubwa wa ekari 210 na kuwa chanzo cha ajira kwa wananchi wengi wasiokuwa na kazi.
Akijibu ombi la wakulima wa chama cha Ushirika Ng’anda cha kusajiliwa kuwa wakala wa mbolea za ruzuku, Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya TFRA, John Cheyo, amemwelekeza Meneja wa TFRA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bw. Joshua Ng’ondya, kuhakikisha Chama hicho kinasajiliwa na kusaidia kusambaza pembejeo hiyo kwa wanachama wake na kutatua changamoto ya ucheleweshaji pindi inapohitajika.
Cheyo alisisitiza kuwa serikali inatamani kuona wakulima wanaongeza tija na uzalishaji, akiwahimiza kulima kwa bidii ili kuzalisha mara mbili zaidi ya msimu uliopita ili kukuza uchumi wao.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya GBRI Business Solutions Company Limited, inayojihusisha na ununuzi na uongezaji thamani wa zao la parachichi Hadija Jabir, amewasihi wakulima kuzingatia matumizi sahihi ya mbolea kwenye zao la parachichi ili wazalishe kwa wingi na ubora unaohitajika kwenye soko la nje.
Alhamisi, 29 Mei 2025
WATUHUMIWA 12 WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA MAKOSA YA UHUJUMU UCHUMI
Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Temeke, Holle Makungu akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa kutoa taarifa ya utendaji wa kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Machi 2025.
Wanahabari na maafisa TAKUKURU walioshiriki kwenye mkutano wa Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Temeke, Holle Makungu akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa kutoa taarifa ya utendaji wa kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Machi 2025.
..........
NA MUSSA KHALID
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Temeke imewafikisha mahakamani watuhumiwa kumi na wawili kwa mashtaka ya uhujumu uchumi,Ubadhirifu na Utakatishaji fedha kiasi cha zaidi ya milioni 165.14
Hayo yameelezwa leo jijini Dar es salaam na Mkuu wa TAKUKURU (M)Temeke,Holle Makungu wakati akizungumza na wananahabari akitoa taarifa ya kipindi cha Januari hadi Machi mwaka huu ambapo amesema mashtaka hayo yamefunguliwa katika mahakama ya Wilaya Kigamboni.
Mkuu huyo wa TAKUKURU
Temeke amewataja baadhi ya washtakiwa hao kuwa ni pamoja na Annie Nyabugumba
Maugo ambaye ni Afisa Hesabu(Ofisi ya Rais TAMISEMI)Tumsifu Christopher
Kachira,(afisa mwandamizi OR-TAMISEMI) na Aidani Zabron Mponzi (Ofisa hesabu
OR-TAMISEMI).
Wengine ni Jonathan
Stanley Manguli (aliyekuwa Afisa hesabu OR TAMISEMI),Godrey James
Martiny(aliyekuwa mkuu wa kitengo cha Fedha na Uhasibu),Juvenalis Mauna(Mkuu wa
kitengo cha udhibiti taka na Usafi wa Mazingira),Josephat
Mtembei(Mhandisi),Bibiana Mdete (Mtunza Bohari)na Henry Herman(Afisa
Ugavi).
Mbali na Watendaji hao wapo pia wakandarasi walioshatakiwa katika kesi hiyo ni Hamis Kashinje Manfred,Paulo Sam Mwakyusa na Godwin Adamson Cheyo ambao kampuni zao zinatumika kutakatisha fedha hizo.
Aidha,Makungu,amesema kwa mujibu wa hati ya mashtaka,makosa wanayoshtakiwa nayo ni kusababisha hasara kinyume cha kifungu cha 10(1) cha jedwali la kwanza na kifungu cha 57 na 60(2) cha sheria ya Uhujumu Uchumi sura ya 200 mapitio ya 2022,kosa la utakatishaji fedha k/f cha 12(1)(a) na 13(1) (a) cha Sheria ya utakatishaji fedha sura 423 ya mapitio 2022,ubadhirifu kinyume na k/f cha 28(2) cha Sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa sura ya 329.
Aidha Makungu,amesema washtakiwa hao wamepelekwa mahabusu kwa kuwa makosa yao hayana dhamana hadi kesi yao itakapokuja tena mahakamani hapo tarehe 12/6/2025 kwa ajili ya kutajawa.
Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, watuhumiwa wanakabiliwa na kosa la kusababisha hasara, kinyume na kifungu cha 10(1) cha Jedwali la Kwanza pamoja na vifungu vya 57 na 60(2) vya Sheria ya Uhujumu Uchumi, Sura ya 200 (Marejeo ya 2022).
Kosa la utakatishaji fedha, kinyume na vifungu vya 12(1)(a) na 13(1)(a) vya Sheria ya Utakatishaji Fedha, Sura ya 423 (Marejeo ya 2022) pamoja na kosa la ubadhirifu, kinyume na kifungu cha 28(2) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Sura ya 329
Katika hatua nyingine,TAKUKURU mkoa wa Temeke imefuatili miradi 13 yenye thamani ya TZS zaidi Bilioni 11,ambapo kati ya miradi 13 miradi mitano (5) ilitolewa ushauri wa kurekebisha mapungufu yaliyobainika.
Hata hivyo Taasisi hiyo imetaja mikakati yake kwa kipindi cha April mpaka Juni mwaka huu kuwa ni kuimarisha juhudi za kuzuia rushwa kwa kuongeza ushiriki wa kila mwananchi na wadau mbalimbali katika kukabili tatizo la rushwa hasa katika uchaguzi wa viongozi wa kisiasa unaotarajiwa kufanyika kwa mwaka.
pIA TAKUKURU inaendelea kuelimisha jamii kwa njia mbalimbali, zikiwemo kuimarisha klabu za wapinga rushwa katika shule za msingi, sekondari, na vyuo, kufanya mikutano ya hadhara na semina, kushiriki maonesho mbalimbali pamoja na kurusha vipindi vya televisheni na redio
KAPINGA ATAJA VIGEZO VYA ZIADA UPELEKAJI UMEME VITONGOJINI
WAZIRI MKUU MAJALIWA AKUTANA NA WAZIRI MKUU WA JAPAN
_▪️Asema Japan itaendelea kuimarisha ushirikiano na Serikali ya Tanzania_
_▪️Aagiza tathmini ya barabara za Kibiti-Lindi na Morogoro-Dodoma_
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekutana na Waziri Mkuu wa Japan, Ishiba Shigeru ambaye amemuhakikishia kuwa nchi hiyo itaendelea kuimarisha ushirikiano na Tanzania jambo ambalo linalenga kuchochea ukuaji wa uchumi kutokana na fursa zitakazoendelea kupatikana kupitia mahusiano hayo.
Amekutana na kiongozi huyo leo (Alhamisi, Mei 29, 2025) katika ofisi ya Waziri Mkuu Tokyo, Japan, ambapo Mheshimiwa Majaliwa amesema ahadi hiyo inazidi kutoa fursa ya wawekezaji na wafanyabiashara wa Japan pamoja na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) kuendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Mheshimiwa Majaliwa ametumia fursa hiyo kumueleza Waziri Mkuu huyo kuwa pamoja na miradi mingine wanayotekeleza nchini, Japan kupitia JICA iangalie uwezekano wa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kuzifanyia ukarabati mkubwa barabara za Morogoro-Dodoma na barabara ya Kibiti-Lindi ambayo imeharibika kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha nchini.
Amesema Waziri Mkuu wa Japan baada ya kupata maelezo hayo ameuelekeza uongozi wa JICA pamoja na Balozi wa Japan nchini Tanzania Youichi Mikami kwenda kutembelea barabara hizo na kuzifanyia tathmini ya uharibifu na kisha kuwasilisha taarifa ili Serikali ya Japan ione namna itakavyoshirikiana na Tanzania katika utekelezaji wake.
Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Japan amepongeza kuendelea kuimarika kwa ushirikiano kati ya Tanzania na Japan na kwamba ameahidi kuhakikisha makampuni mbalimbali ya Japan yataendelea kufanyakazi na Tanzania ili kuisaidia katika kukuza uchumi, kuendelea masuala ya kijamii na teknolojia kwani wanatambua idadi ya watu nchini inaendelea kuongezeka.
Jumatano, 28 Mei 2025
SERIKALI YAKAGUA MIGODI 13, 279, BOHARI ZA BARUTI 164 KUDHIBITI USALAMA
JUMLA ya migodi 13,279 pamoja na bohari za baruti 164 zimekaguliwa nchini kuanzia Julai 2024 hadi Machi 2025.
Hayo yameelezwa leo Mei 28, 2025 jijini Mwanza na Mkurugenzi wa Idara ya Leseni wa Tume ya Madini, Mhandisi Aziza Swedi, akizungumza kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa Tume hiyo, Mhandisi Ramadhan Lwamo, katika kikao kazi cha wakaguzi wa migodi na baruti kutoka mikoa mbalimbali nchini.
Amesema kuwa miongoni mwa migodi hiyo iliyokaguliwa ni migodi mikubwa saba, migodi ya kati 46, migodi midogo 13,226 pamoja na bohari za baruti 164.
“Kaguzi hizi zimeimarisha Sekta ya Madini na kuongeza makusanyo ya Serikali kupitia maduhuli, hivyo kuchangia katika kuimarisha uchumi na Pato la Taifa,” amesema Mhandisi Aziza.
Ameongeza kuwa, “Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan ina matarajio makubwa kwa Sekta ya Madini kutokana na mchango wake mkubwa katika Pato la Taifa. Kufikia mwaka 2024, sekta hii ilichangia asilimia 10.1 ya Pato la Taifa, ikiwa ni zaidi ya lengo la asilimia 10 lililowekwa kufikiwa mwaka 2025.”
Mhandisi Aziza ameeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na kazi kubwa ya Idara ya Ukaguzi wa Migodi, ambayo ndiyo chanzo kikuu cha maduhuli ya Serikali katika sekta hiyo.
Aidha, amewakumbusha wakaguzi kuzingatia Sheria ya Madini Na. 123 katika utekelezaji wa majukumu yao, ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo kuhusu masuala ya afya na usalama mahali pa kazi, uhifadhi wa mazingira, na matumizi salama ya baruti ili kuepuka ajali.
“Naagiza kila mkoa kutambua maeneo yenye hatari kubwa ya ajali na kuyawasilisha kwa Mkaguzi Mkuu wa Migodi, ili kuweka mikakati shirikishi ya kuzuia ajali katika maeneo hayo,” amesisitiza.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Migodi na Mazingira, Mhandisi Hamisi Kamando, amesema kikao hicho cha nne kwa wakaguzi wa migodi kinalenga kujengeana uwezo katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa kuwa wao ni uti wa mgongo wa usimamizi wa Sekta ya Madini.
“Wakaguzi wa migodi wana jukumu kubwa. Malengo ya ukusanyaji wa maduhuli yaliyowekwa na Serikali hutegemea vyanzo vya mapato vinavyosimamiwa na wakaguzi. Bila kulinda vyanzo hivyo, mapato hayawezi kupatikana. Tutaendelea kujifunza na kuboresha utendaji ili kuhakikisha tunafikia malengo,” amesema Mhandisi Kamando.
Aidha, amebainisha madhara ya kutofanya ukaguzi, yakiwemo ajali katika migodi zinazosababisha vifo, kusimamishwa kwa shughuli za uchimbaji, na kupungua kwa mapato ya Serikali.

OFISI YA TRA MBULU KUJENGWA 2026/27
TFRA YAWATAKA WAKULIMA WA KAHAWA KUZINGATIA KANUNI NA TEKNOLOJIA KWENYE KILIMO
Mwenyekiti wa Bodi ya TFRA Akipata ufafanuzi kutoka kwa Meneja wa TFRA Nyanda za Juu Kusini, Joshua Ng'ondya wa kahawa iliyokobolewa kutoka katika _CPU central pulpery unit_ na baadae kuanikwa katika kichanja tayari kwa kupelekwa katika viwanda vya kukoboa kahawa na baadaye kuuzwa mnadani. Wajumbe wa bodi ya TFRA Dkt. Peter Shimo ( kushoto) na Hadija Jabir wakifurahia matunda yaliyosheheni kwenye mti wa kahawa wakati wa ziara ya kikazi kwa mkulima LOHE TANZANIA LIMITED, tarehe 27 Mei, 2025 Mbinga mkoani Ruvuma
Mwenyekiti wa Bodi ya TFRA, Dkt. Anthony Diallo akiwa katika picha na wajumbe alioambatana nao wakati wa ziara yenye lengo la kufuatilia utekelezaji wa mpango wa ruzuku katika mazao ya kimkakati ya kahawa na parachichi kwa mikoa ya nyanda za juu kusini, ikiwa ni mkoa wa Ruvuma tarehe 27 Mei, 2025
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Dkt. Anthony Diallo akizungumza na wajumbe wa Bodi wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Kahawa Mbinga (MBIFACU) Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma tarehe 27 Mei, 2025.
Wajumbe wa bodi ya TFRA, Dkt. Peter Shimo (kulia) akifuatiwa na Lilian Gabriel na Hadija Jabir (Kushoto) wakimsikiliza Meneja wa shamba la kahawa lenye ukubwa wa ekari 113 linalomilikiwa na kampuni ya LOHE Tanzania Limited, Regnald Mapunda wakati wa ziara ya bodi tarehe 27 Mei, 2025
Mwenyekiti wa Bodi ya TFRA, Dkt. Anthony Diallo wa pili kutoka kushoto akiwa na wajumbe wa bodi, menejimenti ya TFRA na Wajumbe wa Bodi ya Chama Kikuu cha Ushirika cha Wakulima wa Miwa mara baada ya kikao kilichofanyika katika ukumbi wao wa mikutano Mbinga mkoani Ruvuma tarehe 27 Mei, 2025
...................
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) amewataka wakulima wa Kahawa Mbinga Mkoani Ruvuma kuzingatia kanuni na teknolojia bora za kilimo cha kahawa ili waweze kuongeza tija ya uzalishaji, fursa ya kujiajiri na kuondokana na umaskini.
Dkt. Diallo ametoa ushauri huo tarehe 27 Mei, 2025, Mkoani Ruvuma ikiwa ni siku ya pili ya ziara ya Bodi ya TFRA kwenye Chama Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Kahawa (MBIFACU), lengo kuu likiwa ni kufuatilia utekelezaji wa mpango wa ruzuku katika mazao ya kimkakati ya kahawa na parachichi kwa mikoa ya nyanda za juu kusini.
Dkt. Diallo amesema, gharama na nguvu anayoitumia mkulima kuwekeza kwenye ekari moja ya shamba la kahawa, lazima ilingane na thamani ya uzalishaji anaoutarajia ambao ili kuupata ni lazima mkulima azingatie kutumia maarifa na sayansi katika uzalishaji wa zao hilo.
Aidha, Dkt. Diallo amewasihi wakulima kuondokana na tabia ya kukalili majina ya mbolea na badala yake wazingatie aina ya virutubisho vinavyohitajika kwenye mashamba yao na kununua mbolea yenye sifa zinazoendana na mahitaji ya udongo wa shamba lake.
Akiwa katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya mbinga, Kanisius Marco, Dkt. Diallo alimuomba kufuatilia taarifa ya wakulima waliopimiwa afya ya udongo na maafisa kilimo waliowezeshwa kwa vifaa hivyo (Soil Scanner) ili kuwasaidia wakulima kuondokana na hasara ya kutumia mbolea kimazoea na kuishia kupata hasara.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Kanisius Marco ameeleza kuridhishwa na ushirikiano baina ya TFRA na watendaji ngazi ya Mkoa, Wilaya hadi vijiji unaowezesha kuwafikia wakulima na kutatua changamoto zao huku akikiri tangu afike wilayani hapo hajakutana na changamoto ya upatikanaji wa mbolea kwa wakulima.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Idara ya Kilimo na Mifugo wa Mkoa wa Ruvuma, Afisa Kilimo Onesmo Mpuya, ameishukuru Serikali kwa mpango wa ruzuku, akisema kabla ya mpango huo walikuwa wakikadiria kiwango cha matumizi ya mbolea kwa wakulima wao, lakini sasa kupitia mfumo wa pembejeo za kilimo, wanaweza kupata taarifa sahihi za matumizi na kufanya makadirio sahihi kwa misimu inayofuata ya kilimo.
Naye Michael Kanduyu Mwenyekiti wa MBIFACU ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kutekeleza mpango wa mbolea ya ruzuku iliyowezesha kuongeza uzalishaji wa kahawa kutoka tani 16,000 hadi kufikia tani 24,000.</
Jumanne, 27 Mei 2025
MILIONI 815.453 KUMALIZA KERO YA MAJI VIJIJI VINNE WILAYANI MTWARA
Picha no 382 Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2025 Ismail Ali Ussi,akiangalia kisima cha maji katika kilichofanyiwa ukarabati mkubwa kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji kwa Wananchi wa Vijiji vya Ndumbwe,Dihimba,Mpondomo na Kinyamu Wilayani Mtwara,kushoto Meneja wa Ruwasa Wilaya ya Mtwara Hamis Mashindike na kulia Mkuu wa Wilaya hiyo Abdala Mwaipaya.
