JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Alhamisi, 8 Mei 2025

BALOZI MBUNDI AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA MAKATIBU WAKUU WA EAC

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Balozi Stephen P. Mbundi leo tarehe 8 Mei, 2025 ameongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kikao cha Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kinachofanyika jijini Arusha.


Kikao hicho na kikao cha maafisa waandamizi wa EAC kilichofanyika kuanzia tarehe 5 hadi 7 Mei, 2025 sehemu ya maandalizi ya Mkutano wa 25 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Afya wa Jumuiya hiyo utakaofanyika tarehe 9 Mei, 2025.


Kikao hicho cha Makatibu Wakuu kinaangazia vipaumbele vya sekta ya afya katika Jumuiya ikiwemo: Maboresho ya mifumo ya afya inayosomana, ushirikiano katika uchunguzi wa magonjwa ya milipuko na ya kuambukiza, upatikanaji wa teknolojia ya kisasa na bora katika huduma za afya na uimarishaji wa mfumo wa usimamizi wa sekta ya afya.


Akitoa salamu za Serikali katika ufunguzi wa kikao hicho Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia anayeshughulikia masuala ya sayansi, Prof. Daniel Mushi kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi ameipongeza Sekretarieti pamoja na maafisa waandamizi kwa uratibu na maandalizi mazuri ya nyaraka ili kuwezesha Baraza la Mawaziri kutoka na miongozo mizuri ya kisera na kupata uelewa wa pamoja juu ya masuala ya kitaalamu katika masuala ya afya


‘’ Nina imani kuwa majadiliano haya yatatoa uelekeo kwa nchi wanachama katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto za sekta ya afya zilizopo na zinazoendelea kujitokeza ulimwenguni ili kujenga utayari wa pamoja wa kukabiliana nazo’’ Prof. Mushi.


Kadhalika, ameainisha jitihada zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kutatua changamoto za afya ambazo ni: Kuendelea kuimarisha mfumo wa afya katika pande zake mbili za muungano (Tanzania Bara na Zanzibar) kwa kuboresha miundombinu; uwekezaji wa rasimali watu pamoja na kuwajengea uwezo.


Jitihada nyingine ni pamoja na matumizi ya vifaa tiba vya kidigitali na msisitizo wa ujumuishi na usawa wa upatikanaji wa huduma bora za afya kwa jamii zenye uwezo mdogo na zilizo mbali na huduma za afya.


Viongozi wengine walioshiriki mkutano huu ni pamoja na Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Maghembe, Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Benjamini Mkapa-Dodoma Prof. Abel Makubi na maafisa wengine waandamizi kutoka katika Wizara, Idara na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

MAMA MARIAM MWINYI AZINDUA ZANZIBAR AFYA WEEK

 

Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi amesema  Maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya Nchi yoyote yanahitaji  jamii yenye Watu wenye Afya Bora.


Mama Mariam ambae pia ni Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Zanzibar Maisha Bora Foundation(ZMBF) amesema hayo alipoizindua  Zanzibar Afya Week  katika Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege , Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 8 Mei 2025.


Amesema Zanzibar Afya Week ni fursa nyengine Muhimu  ya Kuhakikisha  Wananchi wànapata huduma Bora za Afya ikiwemo Elimu ya Afya na Uchunguzi wa Magonjwa mbalimbali Ikiwemo Kisukari, Presha, Saratani ya Matiti , Macho  na  Moyo.


 Mariam Mwinyi ameeleza kuwa Zanzibar Maisha Bora Foundation imejizatiti  kushirikiana na Serikali  Kuimarisha huduma za Afya na Kuifanya Zanzibar kuwa na  Watu wenye Afya Bora na kituo Muhimu cha Utabibu kinachotambulika.


Aidha, Mariam Mwinyi amesema hatua zinazochukuliwa na Wizara ya Afya hivi sasa zinaakisi dhamira ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi ya kuifanya Zanzibar kutoa huduma za Matibabu, Kupunguza Rufaa za kwenda nje ya Nchi kufuata Matibabu na kupunguza bajeti za Matibabu na Wageni wanaofika Zanzibar Kupata huduma  za Uhakika za Matibabu.


Halikadhalika Mariam Mwinyi amefahamisha kuwa kupitia Kampeni ya Afya Bora Maisha bora ZMBF imeweza kuwafikia Wananchi 21, 500 kupitia Kambi nne za Afya kuwapatia  Wananchi Elimu ya Afya , Unguja na Pemba 


Vilevile Zanzibar Maisha Bora Foundation  imefanikiwa kupitia Mpango wa Lishe imeweza  kuwafikia Wanawake 2,830 Unguja na Pemba   kuwapatia Elimu ya Lishe na Afya  ya Uzazi na mama wajawazito huduma za Kliniki. 



Kwa upande mwingine Mariam Mwinyi amefahamisha kuwa Programu ya Tumaini Initiative ya ZMBF imeweza  kuwafikia Wasichana balehe 8,676 Unguja na Pemba  wa Skuli za Msingi na Sekondari na kuwapatia Tumaini kits na Elimu ya hedhi Salama na kuchangia Mahudhurio Skuli na kusoma kwa  Waweze kusoma kwa kujiamini.


Mama Mariam Mwinyi amesema Serikali imepiga hatua kubwa katika  kuimarisha Hospitali na Vituo vya Afya pamoja na Sera na Teknolojia ya Utoaji wa huduma katika Sekta ya Afya na kuipongeza kwa Mafanikio hayo.  


Uzinduzi huo uliambatana na Programu za Lishe Bora 2025, Afya Mama na Mtoto 2025 na Shehia Afya Programu 2025

RAIS MWINYI:TUENDELEE KUDUMISHA AMANI KWA UMOJA NA MSHIKAMANO NCHINI

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi amewanasihi Wananchi wa Tanzania kuendelea kudumisha umoja, mshikamano na amani kwa mustakabali mwema wa Taifa kwa vizazi vya sasa na vizazi vijavyo na kujiepusha na matendo yanayoweza kuleta mgawanyiko.


Rais Dkt.Mwinyi amesema hayo alipofungua  Dua Maalum ya kumuombea Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan pamoja na Mamufti, Masheikh, na Waislamu waliotangulia mbele ya haki  iliofanyika katika Msikiti wa Mohamed VI-Bakwata Makao Makuu, Kinondoni Jijini Dar es Salaam tarehe 8 Mei 2025.


Aidha , Rais Dkt.Mwinyi amewapongeza Uongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kwa kuendeleza utaratibu wa Dua ya kila Mwaka na kuiombea nchi amani .


Halikadhalika Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa amani ina umuhimu mkubwa katika  Uchaguzi Mkuu Mwaka huu kabla , wakati na baada ya Uchaguzi huo.


Rais Dkt.Mwinyi amesema jukumu la kuwaombea Dua Masheikh,  Walimu, na Waislamu waliohai na waliotangulia  mbele ya haki na kuiombea amani   Nchi ni miongoni mwa dalili za imani ya kweli kwa Waumini wa Dini ya Kiislamu kwa mikusanyiko yenye kheri kwa mustakabali wa Taifa.

MRITHI WA PAPA FRANCISCO APATIKANA LEO MEI 8 2025

HUYU HAPA PAPA MPYA, KIONGOZI MKUU WA DHEHEDU LA KANISA KATORIKI DUNIANI.

Robert Francis Prevost, aliyezaliwa tarehe 14 Septemba 1955 mjini Chicago, Marekani, ni Papa mpya wa Kanisa Katoliki, akichukua jina la Papa Leo wa XIV.  Kuchaguliwa kwake mnamo Mei 8, 2025, kunamfanya kuwa Mmarekani wa kwanza kushika wadhifa huu katika historia ya miaka 2,000 ya Kanisa Katoliki.

ELIMU NA MAISHA YAKE YA AWALI

Prevost alihitimu Shahada ya Sayansi katika Hisabati kutoka Chuo Kikuu cha Villanova mwaka 1977.  Baadaye, alijiunga na Shirika la Mtakatifu Augustino (OSA) mwaka huo huo, na akaweka nadhiri zake za milele mnamo Agosti 1981.  Alipata Shahada ya Uzamili katika Theolojia kutoka Catholic Theological Union mjini Chicago, na kisha Shahada ya Uzamili na Shahada ya Uzamivu katika Sheria ya Kanisa kutoka Chuo Kikuu cha Kipapa cha Mtakatifu Thomas Aquinas (Angelicum) mjini Roma  .


HUDUMA YA KICHUNGAJI NA UONGOZI 

Baada ya kupewa daraja la upadre mwaka 1982, Prevost alitumwa Peru mwaka 1985 kama mmisionari.  Alitumikia katika maeneo mbalimbali ya Peru, ikiwa ni pamoja

KIKWETE ATETA NA UONGOZI WA KIWANDA CHA DANGOTE- MTWARA.

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete leo Alhamisi amefanya mazungumzo na Ujumbe wa Kiwanda cha Kutengeneza Cement Cha Dongote kutokea Mtwara walipokuja kumtembea Ofisini Dodoma wakiongozwa na Meneja wa Kiwanda hicho Nchini Bwana Adeyemi Fajobi. 

Mazungumzo yao yamejikita zaidi kuzungumzia maeneo yenye changamoto na utatuzi wake. Pia Serikali kuwakumbusha umuhimu wa kiwanda hicho kwa Watanzania haswa ajira na kukuza uchumi wa miji ikianza na Mkoa wa Mtwara. 


Kwa upande wake Bwana Adeyemi amemsisitizia Waziri kuendelea kufanya kazi kutatua changamoto zinazotoka mahala pa kazi na kuiomba Serikali kuendelea kushirikiana nao huku Waziri Kikwete akimuahidi kuwa serikali itaendelea kufanya kazi nao kwa pamoja kustawisha kiwanda kicho kikubwa kwa ustawi wa uchumi wa Tanzania. 

#KaziInaendelea #DangoteCement

MAJALIWA AHANI MSIBA WA MHE. CLEOPA DAVID MSUYA


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Mei 8, 2025 amehani msiba wa aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Cleopa David Msuya, Upanga Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na wanafamilia pamoja na waombolezaji wengine, Mheshimiwa Majaliwa, amewasihi kuendelea kumuombea Mhe. Msuya na wawe wavumilivu katika kipindi hiki kigumu.

Marehemu Cleopa Msuya alifariki Mei 07, 2025 katika hospitali ya Mzena Jijini Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu.

WEATHER FORECAST FOR THE NEXT 24 HOURS


 

TANAPA YAENDESHA MAFUNZO YA USIMAMIZI WA VIATARISHI


Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) limefanikiwa kuendesha mafunzo muhimu ya Usimamizi wa Viatarishi kwa Wakuu wa Kanda, Wasimamizi wa Ofisi Viunganishi, Maafisa wa Hifadhi kutoka maeneo mbalimbali ya nchi.


Mafunzo hayo, yaliyofanyika katika ofisi ya Kiunganishi ya TANAPA, Dodoma kuanzia Mei 5 hadi 9, 2025, yamelenga kuimarisha ufanisi katika usimamizi wa viatarishi kwa kutoa ujuzi na mbinu bora za kutambua, kudhibiti, na kuripoti viatarishi katika ngazi zote za Shirika.


Akizungumza katika katika hafla ya ufunguzi wa mafunzo haya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Godwell Meng’ataki ambaye pia ni Mkuu wa Kanda ya Kusini alieleza kuwa Semina hii elekezi inalenga kuimarisha ujuzi, uelewa wa pamoja na mbinu bora za kusimamia vihatarishi jambo ambalo ni msingi wa Utawala Bora na uwajibikaji wa TANAPA.


“Mafunzo haya ni sehemu ya juhudi za TANAPA, katika kuhakikisha kuwa utawala bora na uwajibikaji unazingatiwa katika usimamizi wa Hifadhi za Taifa, hivyo kuimarisha Uhifadhi na Utalii endelevu nchini ni matarajio yangu kuwa tukirejea katika maeneo yetu ya kazi tutakuwa na nguvu mpya ya kuhakikisha viatarishi vinatambuliwa, mikakati ya kuvithibiti inatekelezwa ipasavyo, na taarifa sahihi zinaandaliwa kwa wakati katika ngazi zote za shirika.” alisema Kamishna Meng’ataki


Semina hii elekezi, iliongozwa na wataalamu kutoka Wizara ya Fedha wakiongozwa na Msaidizi Mkaguzi Mkuu wa ndani Bw. Abrahamu Elisamia Msechu, ambaye aliendesha mafunzo katika kuimarisha utekelezaji wa Usimamizi wa Viatarishi, huku Dkt. Bernard Mnzava kutoka Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) akitoa mafunzo ya kina kuhusu mbinu bora za usimamizi wa viatarishi ili kufikia malengo.


Sambamba na hayo, mafunzo ya vitendo yalifanyika kupitia Mfumo wa Usimamizi wa Viatarishi wa TANAPA, Risk Information Management System (RIMS), ambapo Maafisa wa kutoka kitengo cha TEHAMA walionyesha namna bora ya matumizi ya  mfumo huo katika usimamizi wa viatarishi.

Listen Mkisi Radio