JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Ijumaa, 9 Mei 2025

WAZIRI MKUU AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA KITAIFA YA MAZISHI YA VIONGOZI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Mei 09, 2025 ameongoza Kikao cha Kamati ya Kitaifa ya Mazishi ya aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Hayati Cleopa David Msuya kilichofanyika katika Ofisi ya ndogo za Waziri Mkuu, Magogoni Jijini Dar es Salaam.

TANZANIA YAWAKILISHWA VEMA KWENYE KAMBI YA MAFUNZO YA HUWAWEI

 

Wanafunzi wenye vipaji katika sekta ya teknolojia ya habari na mawasiliano kutoka vyuo vikuu 12 duniani, wameshiriki katika kambi ya mafunzo ya kimataifa ya Huawei Global Seeds for the Future, iliyofanyika kuanzia Aprili 9 hadi Aprili 17, 2025 katika makao makuu ya Huawei huko Shenzhen nchini China. 

Kambi hiyo ya mafunzo ilibeba maudhui yenye lengo la kuwaongezea uwezo wanafunzi hao katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na eneo la kidigiti, ubunifu na ujasiriamali. 

Kambi hiyo iliyodumu kwa muda wa wiki moja ni sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo ya teknolojia ya mawasiliano ya Huawei katika kuendelea kuwawezesha vijana wenye vipaji katika sekta ya teknolojia ya habari na mawasiliano. 

Nchi zilizoshiriki kambi hiyo ya mafunzo nchini China ni pamoja na Tanzania, Algeria, Cambodia, Laos, Uturuki, Ireland, Brazil, Mexico, Azerbaijan, Pakistan, Ethiopia na Afrika Kusini. 

Akizungumzia mkakati huo wa Huawei, mmoja wa wanufaika kutoka Tanzania akiiwakilisha Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa nne wa Shahada ya kwanza ya Sayansi katika Uhandisi wa Kielektroniki na Mawasiliano, Natasha Nassoro amesema mada za mwaka huu hazikuacha mshiriki yeyote nyuma akiweka bayana kuwa walijifunza mambo ya ndani na nje ya tasnia ya Tehama (ICT ) chini ya mpango ulioandaliwa vyema, ukihusisha utafiti na kupendekeza teknolojia tofauti za kuchagiza juhudi za uendelevu duniani chini ya mpango wa tech4good pamoja na kujenga na kuunganishwa na mtandao wa mabingwa wengine wenye vipaji. 

Ujumbe wa wanafunzi hao kutoka vyuo 12 duniani pia ulipata fursa ya kufanya ziara katika vituo vya maendeleo ya kiteknolojia kama vile kampuni ya Alibaba, kituo cha mafunzo cha Huawei Global, Red note, duka la Huawei Flagship pamoja na ziara za kitamaduni huko Shanghai, kutembelea mgahawa maarufu duniani na ziara ya ya kutembelea Jiji la Shenzhen.

Huawei ilizindua programu ya Seeds For the Future nchini Thailand mwaka 2008, na hadi kufikia mwaka huu imefanikiwa kuwakusanya pamoja wanafunzi kutoka nchi 141 duniani huku zaidi ya wanafunzi 18,000 wakinufaika. 

Seeds for the Future ni programu kuu ya Huawei ya kurudisha kwa jamii (CSR), na imekuwa ikiendeshwa kwa kuchagua vipaji vya vijana kutoka duniani kote ili kushiriki katika mafunzo ya muda mfupi yanayolenga kuwashindanisha kwenye teknolojia, kubadilishana tamaduni na kukuza moyo wa ujasiriamali. 

Mpango huo umekuwa pia ukitoa nafasi ya upendeleo kwa wanawake kwa kiwango cha ushiriki cha angalau theluthi moja wawe wanafunzi wa kike. 

MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KUFIKIA 75% MWAKA 2030 - DKT. BITEKO

* Dkt. Biteko akutana na Balozi wa Japan nchini

* Tanzania na Japan kuendelea kuimarisha ushirikiano wake

* Dkt. Biteko aishukuru Japan kufadhili m)mmradi wa umeme Singida

Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa Serikali imeendelea kuboresha, kuimarisha, kurahisisha na kuwezesha upatikanaji wa umeme na nishati safi ya kupikia kwa gharama nafuu ili kupunguza athari za kiafya, mabadiliko ya tabia nchi na kuboresha maisha ya wananchi.

Dkt. Biteko amesema hayo leo Mei 9, 2025 ofisini kwake jijini Dar es salaam wakati alipotembelewa na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Youichi Mikami.

“ Serikali imedhamiria kuwezesha matumizi ya nishati safi ya kupikia kutoka asilimia 21 hadi asilimia 75 ifikapo mwaka 2030 tumewashirikisha sekta binafsi ili kufikia azma hii,” amesema Dkt. Biteko.

Ameongeza kuwa Serikali imeandaa Mpango mahsusi wa Taifa wa Nishati kwa kipindi cha miaka mitano (National Energy Compact 2025 - 2030). Mpango ambao umeandaliwa kwa ushirikiano wa sekta binafsi na wameahidi kuchangia fedha mfano Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika.

Dkt. Biteko amesema fedha hizo zitasaidia kufikia malengo ya Mpango huo wenye lengo la kuhakikisha watu milioni 300 waliopo kwenye Ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara wanapata huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030.

Katika mazungumzo yake na Balozi wa Japan, Mhe. Mikami Dkt. Biteko ameishukuru Serikali ya Japan kwa ushirikiano wake katika utekelezaji wa miradi ya umeme nchini.

“Tunawashukuru kwa ushirikiano wenu na kwa kufadhili mradi wa uunganishaji umeme kutoka Singida hadi nchini Kenya ambao tayari umekamilika. Tunapenda pia kushirikiana nanyi katika miradi ya gesi. Nchi zetu zimekuwa na ushirikiano mzuri na nia ya dhati ya kuhudumia wananchi wake” amesema Dkt. Biteko.

Kwa upande wake, Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Youichi Mikami amesema kuwa nchi yake na Tanzania zimekuwa na uhusiano wa muda mrefu na kuwa Japan itaendelea kuimarisha uhusiano huo.

Pia, ameipongeza Tanzania kwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali (Mission 300) uliofanyika hivi karibuni ambao ulilenga kujadili kuhusu usambazaji wa nishati ya umeme barani Afrika  

"KAMPENI YA 'SOMA NA MTI, ISHI NA MTI' YAZINDULIWA KILOMBERO: MITI LAKI MOJA KUPANDWA SHULENI"

 

........................

Katika kuimarisha juhudi za uhifadhi wa mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, wamezindua rasmi kampeni ya kitaifa ya "Soma na Mti, Ishi na Mti" katika Wilaya ya Kilombero, mkoani Morogoro, ambapo miti 100,000 inatarajiwa kupandwa katika shule za msingi na sekondari kama sehemu ya mkakati wa kuhamasisha elimu ya mazingira miongoni mwa wanafunzi.

Uzinduzi huo umefanyika katika Shule ya Msingi Sululu na kuongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Wakili Dustan Kyobya, ambaye amesisitiza umuhimu wa kuelimisha watoto kuhusu utunzaji wa mazingira tangu wakiwa wadogo.

“Mpango huu utakwenda sambamba na upandaji miti pembezoni mwa barabara kuu ya Kidatu–Mlimba. Hii si kampeni ya miti tu, ni kampeni ya maisha, kwa kuwa mazingira bora ni msingi wa maendeleo endelevu,” alisema DC Kyobya.

Aidha ameipongeza TFS kwa kutoa miche bure kwa wananchi na kuongoza juhudi za kurejesha uoto wa asili unaopotea kutokana na ukataji wa miti na uharibifu wa mazingira, ambapo amesisitiza yeyote atakayehusika na uharibifu wa mazingira, ikiwemo kuingiza mifugo katika maeneo ya hifadhi, hatavumiliwa.

Amesema Miti ni kichocheo kikubwa cha mvua, husaidia kuhifadhi unyevu ardhini, na huchangia katika kutunza vyanzo vya maji – jambo linalosaidia kilimo, uzalishaji wa umeme, na usalama wa chakula.

Kwa upande wake, Mhifadhi wa Wilaya ya Kilombero, Bi. Zalina Hassan, alisema TFS imekwisha toa miche 6,000 katika awamu ya kwanza ya kampeni hiyo, ambayo itapandwa katika shule na maeneo ya barabara ya Kidatu–Ifakara.

“Natoa wito kwa wananchi kufika katika ofisi za TFS kuchukua miche inayotolewa bure na kushiriki katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi,” aliongeza Bi. Zalina.

Bi. Zalina amesema kuwa miti ina mchango mkubwa katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi kwa kufyonza hewa ukaa (carbon dioxide) na kutoa oksijeni. “Tunapopanda miti tunapunguza kiwango cha gesi chafuzi hewani, tunasaidia anga letu na mustakabali wa vizazi vijavyo,” alisema.

Naye Mkurugenzi wa kampeni ya "Soma na Mti Tanzania" alisema lengo ni kuwahimiza wanafunzi kuanzia ngazi ya awali hadi vyuo vikuu kushiriki kikamilifu katika kupanda na kutunza miti katika maeneo yao ya jamii.

Kampeni hii inalenga kuibua kizazi chenye uelewa wa mazingira, kuhifadhi vyanzo vya maji, na kuongeza mvua kwa ajili ya shughuli za kilimo na uzalishaji wa umeme – hasa katika wilaya yenye ardhi oevu kama Kilombero.  

MAWAZIRI WA AFYA WA EAC WARIDHIA TANZANIA KUWA MWENYEJI WA VITUO VIWILI VYA UMAHIRI VYA KIKANDA

 

Mawaziri wa Afya kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wamekutana jijini Arusha katika Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Afya na kuridhia rasmi uanzishwaji wa Vituo viwili vya Umahiri vya Kikanda nchini Tanzania. 

Uamuzi huo umetokana na mapendekezo yaliyowasilishwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu kuanzishwa kwa Kituo cha Umahiri cha Sayansi ya Afya ya Kinywa na meno kitakachokuwa chini ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na Kituo cha Umahiri cha Upandikizaji Uloto na Sayansi ya Magonjwa ya Damu kitakachokuwa chini ya Hospitali ya Benjamin Mkapa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, Mhe. Dkt. Godwin Mollel (Mb.) Naibu Waziri wa Afya na Kiongozi wa ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alieleza kuwa Tanzania itaendelea kuunga mkono ajenda ya afya ya EAC kwa kuimarisha mifumo ya afya, kuwekeza katika rasilimali watu na miundombinu ya afya ili kwenda sambamba na vipaumbele vya kitaifa na kikanda. Pia alisisitiza kuanzishwa kwa vituo vya umahiri ni hatua muhimu katika kuongeza uwezo wa huduma za afya maalum ndani ya kanda. 

Katika kukabiliana na changamoto mpya za kiafya kama ugonjwa wa Mpox, Mhe. Dkt. Mollel alitoa wito kwa nchi wanachama kuimarisha mfumo wa ufuatiliaji wa magonjwa, kuboresha maabara, na kuongeza ushirikiano katika maeneo ya mipaka.

Vilevile alitoa msisitizo wa umuhimu wa ushirikishwaji wa jamii na mawasiliano sahihi katika kupambana na upotoshaji na unyanyapaa unaohusiana na magonjwa. Aidha, alisisitiza azma ya Tanzania kuendeleza elimu ya tiba kupitia miradi na program za kikanda na juhudi za kuoanisha mitaala ya tiba na udaktari katika Jumuiya. 

RAIS MWINYI:ZANZIBAR ITAENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MSUMBIJI


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi amesema  Zanzibar itaendelea   kuimarisha Ushirikiano  wa kiuchumi na Diplomasia na Msumbiji kwa manufaa ya Nchi hizo mbili.


Rais Dkt.Mwinyi amesema hayo alipokuwa na Mazungumzo na Rais wa Msumbiji Daniel Francisco Chapo  ambaye yupo nchini kwa ziara maalum yaliofanyika Ikulu, Zanzibar tarehe 9 Mei 2025.


Aidha Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa uamuzi wa kufanya ziara ya Kwanza Tanzania ikiwemo Zanzibar  baada ya kuchaguliwa kunaonesha kuthamini Ushirikiano huo ulioasisiwa na Viongozi  Waasisi wa Mataifa hayo.


Halikadhalika Rais Dkt, Mwinyi amebainisha Maeneo Matano ya kiuchumi ambayo nchi hizo zinaweza kushirikiana kuwa ni Uchumi wa Buluu, Mafuta na Gesi, Uvuvi wa Bahari Kuu, Utalii na Uwekezaji .


Ameeleza kuwa Uzoefu wa Msumbiji katika  sekta ya Mafuta na Gesi ni eneo muhimu la Kiuchumi ambalo Zanzibar inaweza kujifunza kupitia Uzoefu huo wa takribani miaka 20 wa Msumbiji katika sekta hiyo .


Vilevile Rais Dkt,Mwinyi ameeleza kuwa Mafanikio ya  Zanzibar katika Sekta ya Uchumi wa Buluu nayo ni Sekta Muhimu ambayo Msumbiji inaweza   kujifunza kutokana na Mafanikio ya sekta hiyo hapa nchini.

Akizungumzia Lugha ya Kiswahili  Dkt, Mwinyi amesema ni fursa nyengine muhimu ya Ushirikiano  itakayowezesha nchi hizo kubadilishana Walimu kwa Zanzibar kutoa Walimu wa Kiswahili na Msumbiji kutoa Walimu wa Lugha ya Kireno kujifunza hatua ikayochangia kuchochea Utalii kwa nchi hizo .


Kwa upande mwingine Rais Dkt,Mwinyi ameihakikishia Msumbiji kuwa  Serikali itaendelea kutoa Ushirikiano wa kutosha kwa Wananchi wenye asili ya Msumbiji Waliopo Zanzibar wanaofikia 3000 ambao tayari wengine wameshapewa Uraia wa Tanzania.

Naye Rais Daniel Fransisco Chapo amesema Msumbiji ina dhamira ya dhati ya Kuimarisha Ushirikiano na Zanzibar na ziara yake imelenga kukamilisha azma. hiyo.


Rais Chapo ameeleza kuwa ziara hiyo itafungua milango na fursa za Kiuchumi baina ya nchi hizo pamoja Uhusiamo wa kidiplomasia wa muda mrefu.


Ameipongeza Zanzibar kwa mafanikio inayoyapata kupitia Sekta ya Utalii na Uchumi wa Buluu na kwamba Msumbiji ina kila sababu ya Kujifunza.


Alizungumzia Sekta ya Mafuta na Gesi amesema  Msumbiji imepiga hatua kubwa katika Maendeleo ya Sekta hiyo na  kuihakikishia Zanzibar  kuwa Nchi yake ipo tayari  kubadilishana uzoefu katika sekta hiyo kwa Kuwa na mazungumzo na timu za Watendaji wa pande zote mbili.

AWAMU YA TATU YA MRADI WA MAABARA WA (EAC) WAZINDULIWA LEO, NAIBU WAZIRI WA AFYADKT. GODWIN MOLLEL AKISHIRIKI KATIKA UZINDUZI HUO.


 Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel ameshiriki katika uzinduzi wa Awamu ya Tatu ya Mradi wa Mtandao wa Maabara wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Mobile Labaratory Project Phase III) uliofanyika tarehe 9 Mei, 2025 katika Makao Makuu ya EAC jijini Arusha kando ya Mkutano wa 25 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Afya wa Jumuiya hiyo.


Mradi huo unaolenga kuimarisha uwezo wa nchi wanachama kukabiliana na milipuko ya magonjwa na dharura za afya kwa njia ya uchunguzi wa haraka wa maabara sambamba na kuwajengea uwezo wataalam wa maabara katika nchi wanachama za EAC.

Viongozi wengine waliombatana na Dkt. Mollel katika uzinduzi huo ni: Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia anayeshughulikia masuala ya sayansi, Prof. Daniel Mushi, Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe na maafisa waandamizi kutoka katika Wizara, Idara na taasisi za Serikali Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ya Mapinduzi Zanzibar.


Aidha, katika awamu ya kwanza na ya pili ya mradi huo Tanzania ilinufaika kwa kupata vifaa na mafunzo ya kitaalam, maabara mbili za afya zinazotembea (Mobile Laboratories) na kuimarisha mifumo ya taarifa na uhifadhi wa sampuli.

Tanzania inaendelea kushirikiana na nchi wanachama kuimarisha mifumo ya afya ya kikanda ili kuyafikia malengo yaliyowekwa ya kuwazesha wananchi kupata huduma bora za afya na zenye uhakika.

MUENDELEZO WA ZIARA YA KAMATI YA SIASA CCM MKOA DAR ES SALAAM KUKAGUA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KWA MIRADI YA KIJAMII NA MIRADI YA MAENDELEO

 

📍Ubungo

🗓08 May 2025


Abasi Mtemvu Mwenyekiti wa CCM Mkoa ameongozana na wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa katika Ukaguzi utekelezaji wa ilani ya CCM Wilaya ya Ubungo.  Mwenyekiti *Mtemvu* amewapongeza watendaji wa serikali katika kutekeleza miradi hiyo na amewasisitiza wananchi kutunza miradi hiyo ambayo imetumia gharama kubwa kwa ajili ya maendeleo ya wana Ubungo. Miradi iliyokaguliwa ni:- 


🎤 ~*Mradi wa maji wa booster* (DAWASA)- KIBAMBA ambao unagharimu *Tsh Bilioni 36.9* ambapo mradi huo unatarajia kunufaisha zaidi ya wananchi takribani *77000* wa wilaya ya ubungo, Temeke na Ilala kwani maji yatakuwa yanatoka mara mbili kwa wiki

🎤~*Mradi wa ujenzi wa vyumba 4 vya madarasa na matundu 8 ya vyoo* katika shule ya sekondari ya Mbezi Inn, ambapo mradi huo umegharimu *Tsh milioni 114* mpaka kukamilika kwake

 


🎤~*Mradi wa ujenzi wa uboreshaji wa kituo cha afya makulumla* ambao unatekelezwa kwa pesa za ndani kwa gharama ya *Tsh milioni 380* ambao ulianza 2022 na unatarajiwa kukamilika mapema tarehe 1/6/2025 ambapo mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar Es salaam ndugu *Abasi Mtemvu* amewasihi mafundi katika mradi huu kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha haraka mradi huu.

🎤~ *Mradi wa ufungaji wa Ufungaji wa Transforma 4* kubwa kituo cha umeme cha NIT ambao unafadhiliwa na pesa za ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa gharama ya *Tsh Bilioni 125* ambapo unatarajiwa kukamilika tarehe 3/11/2025 kwani vifaa vimekamilika kwa 95%


Kadhalika; Mkuu wa mkoa wa Dar Es salaam ndugu *Albert Chalamila* ameijulisha kamati ya siasa ya CCM mkoa wa Dar Es salaam kuwa ameziagiza Halmashauri zote zinazounda mkoa wa Dar Es salaam kuhakikisha *zinatenga Fedha ili kujenga vituo vya polisi kwa kushirikiana na jeshi la polisi* ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuendelea kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao ndani ya jiji la Dar Es salaam.

Pongezi kwa serikali ya awamu ya sita chini ya Uongozi  wa Rais *Dkt Samia Suluhu Hassan* kwa kuendelea kusogeza huduma za kijamii kwa wananchi wa Ubungo


*Imetolewa na Idara ya siasa na uenezi mkoa wa Dar Es saalam*


#Ccm Imara

#Kaziiendelee

# DktSamiaMitanoTena🖐🏿


©️Kazi na Utu Tunasonga mbele 2025

Listen Mkisi Radio