RECAP : WASIRA AMTAHADHARISHA MARTHA KARUA WA KENYA KUJIPIMA UBAVU NA CCM

 

Amesema kama anajiona anaweza kutatua migogoro aende nchi nyingine za Afrika


Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira amemjia juu Mwanasheria maarufu na mwanasiasa wa nchini Kenya Martha Karua,  ambaye amekuja nchini kumtetea Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu,  anayekabiliwa na tuhuma za uhaini na kuchapisha picha za uongo mtandaoni.

Wasira amemtaka mwanasheria huyo kuacha kujipima uzito na Chama Cha Mapinduzi huku akimwambia pia kuwa Chama kinaheshimu mamlaka ya Mahakama na Tume Huru ya Uchaguzi (INEC).

Amesisitiza kama Karua anajiona anaweza kushughulika na migoro basi atatue matatizo yaliyoko nchini kwake au mgogoro unaoendelea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya  Congo (DRC). 

Akizungumza mbele ya wananchi wa Mkoa wa Dodoma Leo Aprili 25, 2025 , akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuelezea faida za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Wasira alitumia nafasi hiyo kumjibu Karua hatua kwa hatua na kumtaka aache kuingilia mambo asiyoyajua vizuri.

“Tanzania hatuvurugi amani ya Afrika Mashariki isipokuwa tunaendesha mambo yetu kwa amani na salamu ninazompatia Mwanasheria Martha Karua ni kwamba aache kujipima na CCM, CCM ni chama kikubwa Afrika kinachoanza na nyumba kumi," alisema.

Aliongeza kuwa "CCM haina hofu na chama chochote lakini hatuwezi kuingilia kazi ya Mahakama na hatuwezi kuingilia shughuli za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwa kuwa ni vyombo vyenye mamlaka, lakini kama ni mjuzi ashughulike na mambo ya Kenya."


"Akishindwa arudi nyumbani akaendeshe chama chake ambacho sera zake hazijulikani. Atuache Tanzania tuchaguane kwa utaratibu wetu hata mwenyewe na zungumza hapa nilichaguliwa kwa kishindo katika nafasi hii ndani ya Chama, naamini dozi hii inamtosha," amesema 

Wakati Wasira anamjibu mwanasheria huyo wa Kenya alisema Chama kinamheshimu kwa kuwa ni mtu wa Afrika Mashariki, pia kinaheshimu taaluma yake ya sheria.

Martha ni Mwenyekiti  wa Chama cha People’s Liberation Party (PLP) cha Kenya.

“Anahaki kama mwanasheria kama ameitwa na watu wanaoshtakiwa, sasa pale kuna 'katatizo' tuna Polisi, Mahakama na Tundu Lissu. Sasa Polisi wakikukuta umekosea hawaendi kwa Wasira kusema kwamba umekosea wao wamesomeshwa kujua kama umekosea, wakikuchukua hawaruhusiwi kukaa na wewe muda mrefu.

Post a Comment

Previous Post Next Post