JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumapili, 1 Juni 2025

PROFESA MDEBE: MATUMIZI YA NISHATI JADIDIFU YAMESAIDIA KUPUNGUZA VIFO VYA WATOTO NJITI


Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Shule ya Madini na Jiosayansi , Profesa Evelyne Mbede (wa pili kushoto) na  wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wadau wa Nishati Jadidifu Tanzania (TAREA), Prosper Magali wakiwa na Katibu Mtendaji wa TAREA, Mhandisi Mathew Matimbwi akifuatilia. akitembelea madanda anuai ya wadau wa nishati jadidifu kwenye hafla ya ufungaji wa Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu yaliofanyika jijini Dar es Salaam. 

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Shule ya Madini na Jiosayansi , Profesa Evelyne Mbede (wa pili kushoto) na  wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wadau wa Nishati Jadidifu Tanzania (TAREA), Prosper Magali wakiwa na Katibu Mtendaji wa TAREA, Mhandisi Mathew Matimbwi akifuatilia. akitembelea madanda anuai ya wadau wa nishati jadidifu kwenye hafla ya ufungaji wa Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu yaliofanyika jijini Dar es Salaam. 

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Shule ya Madini na Jiosayansi , Profesa Evelyne Mbede (wa pili kushoto) akitembelea madanda anuai ya wadau wa nishati jadidifu kwenye hafla ya ufungaji wa Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mtendaji wa TAREA, Mhandisi Mathew Matimbwi akifuatilia.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Shule ya Madini na Jiosayansi , Profesa Evelyne Mbede akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufunga rasmi Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu yaliofanyika jijini Dar es Salaam.

Katibu Mtendaji wa TAREA, Mhandisi Mathew Matimbwi akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya hafla ya kufunga Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu yaliofanyika jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu

MHADHIRI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Shule ya Madini na Jiosayansi , Profesa Evelyne Mbede amesema matumizi ya Nishati Jadidifu yamesaidia kupunguza vifo vya watoto wanaozaliwa kabla ya miezi yao kutimia (njiti).

 Profesa Mbede ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu aliyasema hayo Mei 29, 2025 wakati akifunga maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

“Zamani wajawazito walikuwa wakijifungua kwa shida vijijini kutokana na kukosa umeme hadi kusababisha watoto waliozaliwa chini ya muda wao (njiti) kupoteza maisha lakini leo hii kwa kutumia nishati jadidifu imesaidia kuokoa maisha ya watoto hao,” alisema Mbede.

Alisema nishati jadidifu hivi sasa inatumika katika vituo vya afya na zahanati mbalimbali nchini na si kwa Tanzania tu bali dunia nzima kusaidia nishati ya umeme kwenye vituo hivyo muhimu kwa jamii.

Profesa Mdebe alisema kumalizika kwa maadhimisho hayo ndio mwanzo wa maandalizi ya maadhimisho ya msimu mwingine wa 2026 mwakani.

Alisema maadhimisho hayo yamekuwa yakipanua wigo wa ubunifu, kwani vijana wengi wamekuwa wakiibuka na bunifu mbalimbali na kuongeza matumizi ya nishati jadidifu na kusaidia maeneo yenye uhitaji, ambako hakuna umeme wa TANESCO na REA na kutatua changamoto za wananchi.

Profesa huyo alisema Tanzania kushiriki katika maadhimisho hayo ni kuendana na hali ya mazingira dunia ili kufikia malengo ya 2030 ya kukabiliana na tabianchi.

 “Maonesho haya yanatija sana, kama nchi tumetoka mbali zamani tulikuwa tukitegemea umeme wa Tanesco pekee lakini hivi sasa tunazalisha umeme kwa kutumia vifaa mbalimbali na hii ni hatua kubwa,” alisema Mbede.

Maadhimisho hayo yaliandaliwa na Jumuiya ya Wadau wa Nishati Jadidifu Tanzania (TAREA) kwa kushirikiana na Wizara ya Madini na wadau mbalimbali wa sekta hiyo.

0 comments:

Chapisha Maoni

Listen Mkisi Radio