JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumatatu, 16 Juni 2025

BEI YA KUJAZA GESI (LPG) KWA MATUMIZI YA KUPIKIA NI HIMILIVU – KAPINGA


........................

📌 Wizara ya Nishati na TAMISEMI zaendelea kushirikiana kuhakikisha  Shule mpya zinafungwa mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema gharama ya kujaza gesi kwenye mitungi (LPG) ni himilivu ikiwa ni jitihada zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ili kuwezesha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Juni 16, 2025 katika ziara ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Simiyu  wakati wa kuzindua Shule Maalum ya Sayansi ya Wasichana ya Simiyu ambayo imefungwa miundombinu ya nishati safi ya kupikia. 

“Mheshimiwa Rais ulituelekeza Taasisi ambazo zinahudumia watu zaidi ya mia moja tuzifungie miundombinu ya nishati safi ya kupikia, Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na TAMISEMI tunatekeleza agizo hilo kwa kuzifungia mifumo ya nishati safi shule mpya ambazo zinajengwa." Amesema Kapinga

Ameeleza kuwa,  uwezo wa shule hiyo ni wanafunzi 800 na mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia iliyofungwa ina uwezo wa kuhudumia wanafunzi 800.

Ameongeza kuwa, kwa idadi hiyo ya wanafunzi 800  mtungi wa gesi katika Shule ya Wasichana Simiyu utakuwa ukijazwa kila  baada ya miezi miwili.


MKOMI AKAGUA BANDA LA MALIASILI.


..................

Na Sixmund Begashe - Dodoma

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi, akiwa ameambatana na Kamati ya Maandalizi ya Wiki ya Utumishi Umma ametembelea Banda la Maliasili na Utalii kwa lengo la kukagua kujionea hatua ya maandalizi kabla ya ufunguzi rasmi wa maonesho hayo, hapo kesho tarehe 17 Juni 2025, Jijini Dodoma.

Aidha Bw. Mkomi ameipongeza Wizara hiyo, kwa hatua ya nzuri ya maandalizi pamoja na ushiriki katika maonesho hayo muhimu kwa maslahi mapana ya Taifa na wananchi kwa ujumla. 

Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Taasisi zake inashiriki maonesho hayo kama sehemu ya kusogeza huduma zake karibu zaidi na  wananchi.

Maonesho hayo yanafanyika katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma kuanzia leo tarehe 16 - 23/06/2023.

WIKI YA UTUMISHI WA UMMA DODOMA,KATIBU MKUU ATEMBELEA BANDA LA NCC

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais -Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma S. Mkomi akisoma maelezo kwenye Banda la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) alipotembelea banda hilo leo akiwa na viongozi wengine mbalimbali kutoka katika ofisi yake.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais -Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma S.  Mkomi, akiingia kwenye Banda la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC).

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais -Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora , Bw. Juma S. Mkomi akipewa maelezo na Afisa Habari na Uhusiano Mkuu wa Baraza la Taifa la Ujenzi  (NCC), Bi. Namsembaeli Mduma, kuhusu majukumu ya Baraza hilo wakati alipotembelea banda la NCC akiwa na viongozi wengine kutoka katika ofisi yake.

Mkurugenzi wa Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Benard Makhanda akisaini kitabu cha wageni katika Banda la NCC baada ya kupata maelezo mbalimbali kuhusu NCC.
Mkurugenzi Msaidizi wa Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Jafari Maganga akisaini kitabu cha wageni katika Banda la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) baada ya kusikia Maelezo kuhusu Baraza hilo. Be  Maganga alikuwa ameambatana na Mkurugenzi Makhanda pamoja na Katibu Mkuu wa UTUMISHI kutembelea banda hilo.

....................

Katibu Mkuu Utumishi apongeza maandalizi ya banda la NCC
Aelezwa kuhusu majukumu yanayotekelezwa na kupongeza

KATIBU Mkuu, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (UTUMISHI), Bw. Juma S. Mkomi, ametembelea banda la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma leo na kukagua maandalizi yake.

Akiwa na viongozi wengine kutoka katika ofisi hiyo ya Rais (UTUMISHI) miongoni mwao akiwa ni Mkurugenzi Benard Makhanda na Mkurugenzi Msaidizi Jafari Maganga, Katibu Mkuu amepongeza maandalizi ya banda hilo na kusikiliza maelezo kuhusu majukumu mbalimbali yanayotekelezwa na NCC.

Katika maelezo hayo yaliyotolewa na Afisa Habari na Uhusiano Mkuu wa NCC, Bi. Namsembaeli Mduma, Katibu Mkuu alielezwa baadhi ya majukumu hayo kuwa ni pamoja na kutoa ushauri wa kitaalamu, uratibu wa usuluhishi wa migogoro inayohusu sekta ya ujenzi na uandaaji wa fahirisi ya bei ya vifaa vya ujenzi.

Majukumu mengine ni kuratibu na kufanya utafiti, ukaguzi wa kiufundi wa miradi mbalimbali ya ujenzi inayotekelezwa nchini, kutoa mafunzo yakuwajengea uwezo wadau wa sekta ya ujenzi, wakiwemo wahandisi, wakadiriaji majenzi, wabunifu majengo na wengine kutoka katika sekta mbalimbali.

Wiki ya Utumishi wa Umma iliyoanza Juni 16, mwaka huu, itazinduliwa rasmi kesho na kuhitimishwa Juni 23, mwaka huu.

ETDCO YAKAMILISHA MRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME KILOVOLTI 132 TABORA - KATAVI


............................

Kampuni ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji wa Umeme (ETDCO) imekamilisha ujenzi wa laini mpya ya umeme yenye msongo wa kilovolti 132 kutoka mkoani Tabora hadi Katavi.

Laini hiyo, yenye urefu wa kilomita 383, kukamilika kwake ni hatua muhimu ya kuunganisha Mkoa wa Katavi na Gridi ya Taifa.

Akizungumza leo, Juni 16, 2025, wakati wa majaribio ya laini hiyo katika kituo cha kupoza umeme cha Mpanda mkoani Katavi, Kaimu Meneja Mkuu wa ETDCO, CPA Sadock Mugendi, amesema ujenzi huo umekamilika kwa asilimia 100.

CPA.  Mugendi ameishukuru Serikali na Wizara ya Nishati kupitia TANESCO kwa kuiamini kampuni hiyo kutekeleza mradi huo wa kimkakati.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa ETDCO, Mhandisi Dismas Massawe, amesema gharama ya mradi huo ni shilingi bilioni 116, fedha ambazo zimetolewa na Serikali ya Tanzania. 

Amesema kuwa gharama hiyo inahusisha ujenzi wa laini ya kusafirisha umeme kwa umbali wa kilomita 383 kutoka Tabora hadi Mpanda hadi Katavi.

Mradi huo ni sehemu ya juhudi za Serikali za kupeleka umeme wa uhakika wa Gridi ya Taifa kwenye maeneo ambayo hayakuwa yameunganishwa awali, kama Mkoa wa Katavi ikiwa na lengo la kuchochea maendeleo kwa kutumia nishati safi, salama, na rafiki kwa mazingira.


 

TRA WAAGIZWA KUFUATA SHERIA NA TARATIBU ZA UTUMISHI WA UMMA

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) akijibu swali bungeni jijini Dodoma.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano, WF - Dodoma)

................

Na Farida Ramadhani, WF – Dodoma

Serikali imemwagiza Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakikisha kuwa watumishi wa Mamlaka hiyo wanafuata taratibu na sheria zilizowekwa.

Agizo hilo limetolewa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb)alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mhe. Janejelly Ntate aliyeeleza kuwa Sheria ya Usimamizi wa Kodi haitekelezwi kwa wafanyabiashara ambao wamesajiliwa kwa mara kwanza na wanatakiwa kulipa jumla ya kodi aliyoahirishiwa baada ya miezi sita (6) kwa awamu tatu.

Mhe. Ntate alisema wafanyabiashara bado wanalipwa kabla ya miezi sita kinyume na matakwa ya sheria hiyo.

Mhe. Chande Serikali kupitia Bunge, ilifanya marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Kodi (Tax Administration Act, 2015) Kifungu cha 22, ili kuahirisha wajibu wa kulipa kodi ya awamu chini ya Sheria ya Kodi ya Mapato kwa kipindi cha miezi sita (6) tangu tarehe ambayo Nambari ya Utambulisho wa Mlipaji (TIN) ilipotolewa kwa mtu yeyote anayesajiliwa na kupewa TIN kwa mara ya kwanza.

“Lengo la mabadiliko hayo ya Sheria ni kuweka mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara na wawekezaji”, alibainisha.
Mhe. Chande alisisitiza kuwa kwa wale ambao hawatofuata sheria na taratibu , Sheria ya kiutumishi itachukua mkondo wake.

Wakati huo huo, Mhe. Chande iliwatoa hofu wananchi kuwa “Single Window” haitasababisha uzoroteshaji wa ukusanyaji mapato ya Serikali bali utasaidia kuondoa usumbufu kwa wateja na kurahisisha ukokotoaji wa kodi mbalimbali kupitia Mfumo wa TANCIS uliohuishwa.

Alisema hayo alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kondo, Mhe. Mohamed Said Issa aliyetaka kujua changamoto zinazoweza kuzorotesha ukusanyaji wa mapato katika mfumo mpya wa kuchakata kodi ya forodha ambao ni "single window"

Mhe. Chande alisema “Single Window” ni dirisha moja la kufanikisha uwasilishaji wa nyaraka mbalimbali kutoka kwa wadau wote muhimu katika mnyororo wa ugomboaji mizigo Forodha.

Alibainisha kuwa kabla ya mfumo huo, mteja alilazimika kuwasilisha nyaraka na vielelezo mbalimbali kwenda kila idara ya Serikali inayohusika katika mnyororo wa ugomboaji wa mizigo na hivyo kusababisha usumbufu mkubwa na kuchelewesha ugomboaji wa mizigo forodhani.

Jumapili, 15 Juni 2025

SERIKALI YAHAMASISHA WADAU KUWEKEZA KATIKA UTALII ENDELEVU


.....................

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Khamis Hamza Khamis ametoa wito kwa wadau katika sekta ya utalii kuongeza uwekezaji na juhudi za pamoja katika usimamizi wa utalii katika maeneo yanayolindwa ili kuwa na Utalii endelevu.

Mhe. Khamis ameongeza kuwa kuwekeza katika utalii wa maeneo yaliyolindwa sio tu kunafaida kwa uhifadhi, bali pia unahamasisha maendeleo ya kimkakati ya jamii inayozunguka maeneo hayo.

Akifungua warsha ya kujadili umuhimu wa Uhifadhi, Ukuaji wa Utalii na Ustawi wa Jamii iliyofanyika kwenye hotel ya Mt. Meru jijini Arusha leo tarehe 14.06.2025 amesema ni wakati sasa wadau kujitokeza kwa wingi kuwekeza na kujikita katika usimamizi wa Rasilimali za utalii ili ziweze kutuletea faida kwa jamii na Taifa kwa ujumla.

Pia amesisitiza juu ya umuhimu wa kubadilishana uzoefu utakaosaidia katika kuchunguza fursa zilizopo kwenye Maliasili zitakazoweza kunufaisha jamii kama kichocheo muhimu cha maendeleo.

Amesema bila wanayama hakuna Utalii, bila misitu hakuna utalii hivyo ni vyema tukahamasisha watu kutumia nishati safi ili kuendelea kutunza misitu yetu, kulinda na kuhifadhi wanyama wetu ili utalii uendelee na uingize pato kwa Taifa na jamii ya maeneo husika ipate manufaa.

Akizungumza wakati wa warsha huyo ya Mkurugenzi wa Benki ya Dunia Kanda ya Tanzania Nathan Belete amesema kukuza ushirikiano kati ya wadau ni njia bora ya kusaidia juhudi za uhifadhi.

"Utafiti umeonesha kuwa utalii katika maeneo yanayolindwa una faida kubwa, unatoa ajira, na unaingiza Taifa pato kubwa ambalo hurudishwa kwa jamii kwa kuwekezwa katika miradi ya maendeleo’

Alibainisha kuwa, katika baadhi ya nchi, kila dola moja iliyowekezwa katika maeneo yanayolindwa huzalisha hadi dola 28 ambapo ni faidi kwa jamii na Taifa lwa ujumla.

Naye Mkurugenzi wa Utekelezaji wa Kanda kutoka Benki ya Dunia Anna Wellenstein amesisitiza umuhimu wa ushirikiano na mafunzo

"Warsha hii imetujengea uwezo kwamba rasilimali asilia si muhimu tu kwa bioanuai ila pia ni injini yenye nguvu katika ukuaji wa uchumi na maendeleo ya jamii," alisema.

Amesema mkutano huu wa siku mbili umtengeneza jukwaa lililowezesha washiriki kujifunza kutoka kwa kila mmoja kati ya nchi na nchi, Taasisi kwa Taasisi, Sekta binafsi pamoja na wadau wa utalii.

Warsha hii ya siku mbili imehudhuriwa na wataalamu wa kitaifa na kimataifa zaidi ya 100 kutoka katika Taasisi za Serikali, mashirika ya kiraia, sekta binafsi, na washirika wa maendeleo kujadili mambo muhimu ya kuhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii.

Jumamosi, 14 Juni 2025

RAIS SAMIA NA RAIS WA BENKI YA AFRIKA AfDB WAKAGUA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE MSALATO

Muonekano wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato Jijini Dodoma tarehe 14 Juni, 2025. ujenzi wa Kiwanja hicho cha Msalato unahusisha njia ya kuruka na kutua ndege (runway) jengo la abiria, jengo la kuongozea ndege pamoja na Miundombinu mengine.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Nala Jijini Dodoma mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato pamoja na ujenzi wa barabara ya mzunguko wa nje ya Jiji la Dodoma yenye urefu wa km (112.3) tarehe 14 Juni, 2025.

Matukio mbalimbali kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Nala Jijini Dodoma tarehe 14 Juni, 2025.

DC MSANDO AONGOZA MAADHIMISHO SIKU YA MAZINGIRA MKOA WA DAR,ASISITIZA NISHATI SAFI

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mkoani Dar es salaam Albert Msando akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya mazingira kimkoa ambayo yamefanyika katika viwanja vya shule ya msingi Makuburi kwenye Wilaya hiyo Leo tar 14/6/2025.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ubungo Jaffary Juma Nyaigesha akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya mazingira kimkoa ambayo yamefanyika katika viwanja vya shule ya msingi Makuburi Ubungo Leo tar 14/6/2025 jijini Dar es salaam.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Songoro Mnyonge akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya mazingira kimkoa ambayo yamefanyika katika viwanja vya shule ya msingi Makuburi Ubungo Leo tar 14/6/2025 jijini Dar es salaam.

...........................

NA MUSSA KHALID 

Serikali imeendelea kuweka msisitizo wa kupunguza athari za uharibifu wa mazingira kwa kupunguza matumizi ya nishati ya kuni na mkaa kwa shughuli za kupikia ili kuepukana na changamoto ya uharibifu wa mazingira.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Albert Msando alipomwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam katika maadhimisho ya Siku ya mazingira kimkoa ambayo yamefanyika katika viwanja vya shule ya msingi Makuburi kwenye Wilaya hiyo,yakienda sambamba na kauli mbiu ya "Mazingira yetu na Tanzania Ijayo,tuwajibike sasa dhibiti matumizi ya Plastiki"

DC Msando amesema kuwa kauli mbiu hiyo inatoa chajizo la kila mwananchi kuhakikisha anahifadhi mazingira ikiwemo kuhamasisha na kuielimisha jamii kuhusu umuhimu wa mazingira kwa kudhibiti matumizi ya plastika.

"Nitoe wito kwa vyombo vya Habari,taaisisi zote za serikali na zisizoza serikali pamoja na wadau mbalimbali kushirikiana katika kutoa elimu kwa jamii ili kupunguza uharibifu wa mazingira nchini Kwa kudhibiti matumizi ya Plastiki"amesema DC Msando

Aidha amesema kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Albert Chalamila ameziagiza Halmashauri zote katika Mkoa huo kuendeleza juhudi za ukusanyaji wa taka ngumu na laini ili kudumisha usafi wa mazingira kwenye maeneo yao.

Pia amewaagiza wakandarasi wote waliopewa kazi ya kukusanya taka kwenye Mkoa huo kuhakikisha wanatimiza wajibu wao wa kimkataba Kwa ufanisi.

Awali wakizungumza Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinonondoni Songoro Mnyonge amesema wataendelea kutoa elimu ikiwemo kuhamasisha matumizi ya nishati safi huku Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ubungo Jaffary Juma Nyaigesha akisisitiza kuthaminiwa Kwa watu wanaofanya shughuli za kuokota na kukusanya taka katika maeneo mbalimbali.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Bonde la Wamiruvu Mkoa wa Dar es salaam Bi Diana Kimbute amesema mazingira yanapotunzwa ndivyo pia vyanzo vya Maji vinatunzwa.

Katika Maadhimisho yao yamezikutanisha kwa pamoja Halmashauri za Mkoa wa Dar es salaam ambapo pia wameshiri wadau kutoka Taasisi mbalimbali wa mazingira ikiwemo Taasisi isiyokuwa ya Kiserikali ya HUDEFO,Taasisi zinazojihusisha na masuala ya nishati,wanafunzi na wazalishaji wa mitungo ya gesi


Listen Mkisi Radio