JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumatano, 30 Aprili 2025

WAFUNGWA NA MAHABUSU KUSIKILIZA KESI KWA MAHAKAMA MTANDAO NI KWA SABABU ZA KIUSALAMA: BASHUNGWA

 

VIDEO KESI ZA WAFUNGWA NA MAABUSU👇👇👇

https://youtu.be/2HjUC6IJ524


Atoa maelekezo kufuatia matamko ya CHADEMA. 


Asema hakuna ‘VIP treatment’ kwa wanaotaka kuwaona Wafungwa na Mahabusu.


Aagiza Jeshi la Polisi kudhibiti maandamano na matishio ya kiusalama.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amesema kuwa Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania litaendelea kuwawezesha Wafungwa na Mahabusu kusikiliza mashauri yao wakiwa magerezani kupitia Mahakama Mtandao, hasa kunapokuwepo na viashiria vya matishio ya kiusalama, ili kudumisha amani na kulinda usalama wa raia na mali zao.


Ameeleza kuwa mojawapo ya sababu ya kuendelea kutumia Mahakama Mtandao ni masuala ya kiusalama, ambapo hivi karibuni baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wametoa matamko yanayoashiria uvunjifu wa amani na usalama, hali iliyosababisha baadhi ya Wafungwa na Mahabusu kusikiliza mashauri yao kwa njia ya mtandao.


Bashungwa ameyasema hayo leo, tarehe 30 Aprili 2025 jijini Dodoma, alipoambata na Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), kukagua Makasha ya kisasa ya Mahakama Mtandao yanayowezesha usikilizaji wa mashauri kwa njia ya kiteknolojia katima Gereza la Isanga -Dodoma

“Jeshi la Polisi linapokuwa na taarifa za kiinterejensia za wazi na zisizo wazi, kwa mfano maandamano ya CHADEMA na Watanzania ni mashahidi, Viongozi wa CHADEMA walisema waziwazi kwamba waandamana wakakinukishe. Jeshi linapokuwa na taarifa za kiusalama likashirikiana na Mahakama kutoa haki ile ile lakini kwa kutumia teknologia ya Mahakama Mtandao ili kuzuia fujo mtaani, naomba Watanzania watuelewe” amesema Bashungwa.


Aidha, Bashungwa amewahakikishia wananchi kuwa Vyombo vya Usalama vitaendelea kuhakikisha kuna utulivu kwa kudhibiti maandamano, matishio ya kiusalama, na vitendo vyote vinavyoweza kuhatarisha amani na usalama wa nchi.


“Niendelee kuliagiza Jeshi la Polisi  kusimamia sheria na kuhakikisha nchi yetu inaendelea kuwa na amani, hata yule ambaye hataki amani, sisi tutamlazimisha kuhakikisha nchi yetu inakuwa amani na salama” amesisitiza Bashungwa


Pia, Bashungwa ameliagiza Jeshi la Magereza kusimamia kwa ukamilifu sheria na taratibu kwa wale wanaotaka kuwaona Wafungwa na Mahabusu, akieleza kuwa taratibu hizo lazima ziheshimiwe bila upendeleo.

““Niliona moja ya viongozi akisema anataka ‘Special treatment’ anapoenda kumuona Maabusu, hiyo nayo sio sawa. Zipo taratibu zinazosimamiwa ndugu, jamaa na rafiki anapotaka kwenda kumuona Maabusu au Mfungwa, kwahiyo mkitaka tuwe na ‘VIP treatment’ na yenyewe sio sawa” amesema Bashungwa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), Vita Kawawa, amelipongeza Jeshi la Magereza kwa kuendelea kuwawezesha Wafungwa na Mahabusu kupata haki zao kwa kusikiliza mashauri kupitia Mahakama Mtandao, hatua inayotekeleza mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai.

SH MILIONI 12,470 ZAMTIA MGANGA WA TIBA ZA ASILI LUMANDE

 


VIDEO MGANGA FEKI MBALONI KWA UTAPELIhttps://youtu.be/pHWAb6rJ6Qs

Mwalimu wa shule ya Sekondari Nyakabungo Edward Bihemo Mwenye umri wa miaka 43 Mkazi wa mtaa wa Nyamanoro Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza ametapeliwa na mganga wa tiba asilia aliyejulikana Kwa jina la Edward Emmanuel kiasi Cha sh, Mil 12,470.


Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa Mwanza Wilbroad Mtafungwa ameeleza kuwa jeshi la polisi lilimkamata Edward Emmanuel miaka 38 na mmiliki wa nyumba ya kulala wageni Private Lodge Mkazi wa Nyamohongolo Wilaya Ilemela Kwa kosa la kujipatia pesa Kwa njia ya udanganyifu.


Mtafungwa ameeleza kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo mnamo April 18 Mwaka huu kujipatia fedha Kwa njia ya  udanganyifu Kwa kumlaghai Edward Bihemo kupitia kazi yake ya uganga wa tiba asilia.


Mtuhumiwa Edward Emmanuel alimweleza Edward Bihemo kuwa ana uwezo wa kuzalisha fedha Kwa njia ya miujiza ambapo mtuhumiwa alichukuwa fedha hizo na kuziweka katika begi lake na kumuamuru mhanga awe anazitolea sadaka mara Kwa mara ili ziweze kuongezeka.


"Aliendelea kutoa sadaka hizo Kwa muda mrefu hadi kufika hatua ya kukosa fedha ya kujikimu na kuamua kwenda Kwa mtuhumiwa Kwa lengo la kuchukua fedha alizowekeza na ndio alipogundua kuwa alikuwa ametapeliwa" Alisema Mtafungwa.

WIKI YA UTALII TANZANIA ILIVYONOGESHA OSAKA EXPO 2025.

 

Wiki ya Utalii Osaka Expo 2025 iliyoanza rasmi tarehe 25  Aprili, 2025  inatarajiwa kumalizika  tarehe 6  mwezi  May, 2025 ambapo mojawapo ya tukio kubwa linaloloendelea kufanyika  katika  wiki hii ni pamoja na Tanzania kuonesha vivutio vya Utalii vilivyopo nchini ikiwakilishwa na Bodi ya Utalii Tanzania pamoja na taasisi zilizopo chini ya wizara ya Maliasili na Utalii.


Hifadhi ya Ngorongoro, Mlima Kilimanjaro, Visiwa vya Zanzibar, Serengeti pamoja na vivutio vingine vya malikale na urithi wa utamaduni vimeweza kuwa na mvuto mkubwa kwa wageni mbalimbali wanaofika katika Banda la Tanzania nchini Japan na kujionea namna nchi hiyo ilivyoweza kuwa na rasilimali nyingi na za kuvutia.


Balozi wa Tanzania nchini Japan Mheshimiwa Baraka Luvanda aliongoza timu ya Tanzania katika ufunguzi wa maonesho hayo katika banda la Tanzania na kupongeza juhudi zinazofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Bodi ya Utalii katika kuhakikisha kuwa wageni wengi wanafikiwa kwa kupata taarifa ya vivutio vilivyopo na namna ya kuweza kuvitembelea vivutio hivyo.


“Hongereni sana TTB na TanTrade kwa kazi kubwa mnayoifanya ya kuitangaza nchi yetu katika maonesho kama haya, hii inasaidia kwa kiasi kikubwa kuendelea kuwavutia wageni wengi kuja kuona vivutio tulivyonavyo na hapa kwa kweli tunamuunga mkono Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kutangaza utalii wetu”,alisema Balozi Luvanda.


Mkurugenzi wa Masoko kutoka Bodi ya Utalii Tanzania Ernest Mwamwaja alieleza kwamba sekta ya utalii imekuwa ikifanya vizuri kadri miaka inavyosonga mbele hasa kutokana na juhudi kubwa zinazofanywa za kutangaza vivutio vyote vilivyopo kwa nguvu kubwa ambapo kwa sasa imekuwa ikiingiza asilimia katika ya 17 mpaka 20 ya pato la taifa.


“Sekta hii inakua na ndiyo maana mpaka sasa tumevuka lengo la watalii milioni tano kama ilivyoelekezwa kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi, tutaendelea kuutangaza utalii katika kila matukio kwani hii ndiyo njia sahihi ya kupeleka taarifa kwa wadau na watumiaji wa sekta hii.”alisema Mwamwaja.


Meneja wa banda la Tanzania nchini Japan bwana Deo Shayo alisema kuwa Tantrade imekuwa ikiwaunganisha wadau wa sekta mbalimbali katika maonesho makubwa kama EXPO 2025 ili kutoa fursa kwa kila sekta kuweza kujitangaza katika masoko ya kimataifa na kusaidia pia kuvutia wawezekezaji kutoka mataifa mengine.


Kwa upande wake Afisa Makoso Mkuu kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro bwana Michael Makombe alisema EXPO 2025 inaonesha kuwa na faida kubwa kwa Tanzania na Ngorongoro kwa ujumla kutokana na wageni wengi kuonesha kuvutiwa na utalii wa wanyama na hivyo maonesho hayo yatasaidia kuongezeka kwa idadi ya wageni msimu ujao wa utalii.


Maonesho ya EXPO 2025 yanaendelea nchini Japan ambapo kwa wiki mbili hizi wadau wa sekta ya utalii wamekuwa katika pilika pilika kubwa ya kutangaza vivutio na kujiandaa kwa mikutano ya wadau wa sekta hiyo ili kuweza kubadilishana mawazo na kuainisha maeneo ambayo wanaweza kutembelea.

NIMERIDHISHWA NA MAANDALIZI KUELEKEA SHEREHE ZA MEI MOSI-MAJALIWA

 

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema ameridhishwa na Maandalizi kuelekea sherehe za siku ya wafanyakazi duniani zitakazofanyika kesho Mei mosi, 2025 kitaifa Mkoani Singida katika Uwanja wa Bombadia

 

Ameyasema hayo leo Jumatano (Aprili 30, 2025) alipopokea taarifa na kukagua maandalizi ya Maadhimisho ya Sherehe hizo. Mgeni rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Mheshimiwa Majaliwa ameipongeza kamati inayoratibu sherehe hizo na kuwataka kuhakikisha wanakamilisha maeneo machache yaliyobaki ambayo yanahitaji maboresho.

 

Awali, akitoa taarifa ya maandalizi hayo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Ridhiwani Kikwete amesema maandalizi yamekamilika kwa kiasi kikubwa na wapo tayari kumpokea Rais Dkt. Samia kwa ajili ya sherehe hizo.

JESSICA MSHAMA MGENI RASMI KATIKA KONGAMANO LA BINTI NA DKT. SAMIA.

 

Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa UVCCM Taifa, Ndugu *Jessica Mshama*, atakuwa mgeni rasmi katika *Kongamano Maalum la Mabinti na Dkt. Samia* litakalofanyika   tarehe 1 Mei 2025 katika ukumbi wa Kibo Garden. Kongamano hili limeandaliwa na *UVCCM UDSM MLIMANI* kwa lengo la kuwaunganisha vijana wa elimu ya juu na kuwawezesha kubadilishana mawazo, kuongeza uelewa wa masuala ya uongozi n.k. kama ilivyo elezwa hapo juu.


🇹🇿 Ndugu *Jessica Mshama* anatarajiwa kutoa hotuba ya kuhamasisha, kuelimisha  mabinti na vijana wote wa UDSM kushiriki kikamilifu katika kuchangia maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla. Kongamano hili litakuwa jukwaa muhimu kwa vijana wasomi wa kike na wa kiume kujifunza na kupata mwanga kuhusu nafasi ya vijana katika siasa na Uongozi  hasa kupitia dira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, *Dkt. Samia Suluhu Hassan*. 


 "KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE" 

RAIS MWINYI:SMZ KUVIONDOA VIKWAZO VINAVYOKWAMISHA UENDESHAJI WA BIASHARA.

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi ameahidi Serikali kuviondoa Vikwazo vyote vinavyochangia Kukwamisha Uendeshaji wa Biashara hapa nchini.


Rais Dkt,Mwinyi amesema hayo alipoizindua Sera ya Biashara ya 2024 na Tathmini ya Uimarishaji wa Mazingira ya Biashara (Zanzibar Blue Print) 2025 Hafla iliofanyika New Amani Hotel , Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 30 Aprili 2025.

Aidha Rais Dkt, Mwinyi amebainisha kuwa bado lipo Tatizo la  kuwepo kwa Urasimu,Ucheleweshaji wa Watu kufanya Biashara zao na Utendaji usio na Ufanisi kwa baadhi ya Watendaji katika Sekta ya Biashara.


Rais Dkt Mwinyi amesema Serikali haiwezi Kuendelea na  Watendaji wanaosababisha kuwepo kwa Vikwazo katika Uendeshaji wa Biashara.


Vilevile Rais Dkt.Mwinyi amewatoa hofu Wadau na Taasisi   zinazosimamia Sekta ya Biashara  kuwa Serikali imedhamiria kuweka Mazingira mazuri ya  Ufanyaji wa Biashara.

Halikadhalika, Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa licha ya kuwepo kwa Sera ya Biashara na Ripoti ya Tathmini lazima kuwepo na Msimamizi Mwenye dhamira ya Kweli ya  kusimamia Utekelezaji wa Sera Hiyo na kuahidi kulivalia njuga Suala Hilo na  Utekelezaji wa Sera Hiyo.

 Ameziagiza Taasisi zote za Umma na Binafsi kutekeleza kikamilifu Sera ya Biashara 2024 na tathmini ya Uimarishaji wa Mazingira ya Biashara.(Zanzibar Blue Print) 2025.


Akizungumzia Uzinduzi huo wa Sera amesema itasaidia kwa kiwango kikubwa kuleta Ufanisi wa Utekelezaji wa Sekta ya Biashara  na kuifanya Zanzibar kuwa kitovu cha Biashara.

Kwa upande mwingine, Rais Dkt Mwinyi amesema kuwa Sera hiyo ni hatua ya Kufanikisha Ahadi ya Ilani ya CCM ya 2020-2025  ilioitaka Serikali Kuandaa Mazingira Bora ya Biashara Nchini.


"ACT BILA KULITAJA JINA LA MAALIM SEIF HAKUNA JIPYA KWA WAZANZIBARI" ASEMA MBETO

 

Na Mwandishi  wetu,Micheweni 


Chama Cha Mapinduzi kimesema  Viongozi  wa   ACT  Wazalendo bila   kulitaja jina la Marehemu   Maalim  Seif Sharif Hamad, hawana uwezo wa kukubalika katika jamii na kupata viti  vya  udiwani ,uwakilishi ubunge na kuongeza kura za urais. 


Kimesisitiza kuwa ndio maana hueneza na kuhubiri    Siasa za utengano , shari au kukimbilia kukosoa  mfumo  wa  Muungano wa serikali  mbili si sahihi ili wapatwe kusikilizwa 


Katibu wa Kamati Maalum  ya NEC  Zanzibar  Idara  ya itikadi  ,Uenezi na Mafunzo,  Khamisi  Mbeto  Khamis, ameeleza hayo akiwa katika ziara ya kizazi huko  Micheweni Mkoa wa Kaskazini  Pemba



Akizungumza na wanachama wa  CCM  Wilaya  hiyo , Mbeto  alisema kisiasa ACT  Wazalendo  kimeshakwama, hakina maneno ya kuwashawishi wananchi ili kiweze kukubalila  na kuchagulika katika  uchaguzi mkuu wa oktoba  Mwaka huu.


Mbeto  alisema baada ya chama hicho  kukosa sera zenye matumaini kwa wananchi,  kinga yao kuu ni  kulitumia jina la Maalim  Seif, kuhubiri Siasa za fitna ,majungu na ubaguzi  au kuzungumzia muundo wa Muungano .


"Juussa na viongozi  wenzake  hawana uwezo  wa kuwaeleza lolote wazanzibari wakasilizwa na kufahamika.Wana dosari  na shutuma  katika  jamii zisizowapa heshima.Baada ya kujua  wana udhaifu huo   jina la Maalim  Seif kwao huwa ngao  yao  "Alisema Mbeto 


Aidha  alisema iwapo kungekuwa na tija ya  kuzungumzia kasoro za  chaguzi zilizopita CCM kingezungumzia chaguzi za  mwaka  1957, '61 na '63,  lakini  hakioninkama kuna  umiumu  wowote.


Alisema ACT  kinapozungumzia chaguzi  za  mwaka 1995 hadi 2015 ni katika  kuiaminisha jamii katika uongo wao wa kudai kuwa hakuna  ambao CCM kilishinda kama kinavyojidanganya. .


"Kuzungumzia Uchaguzi uliopita  ni   kutonesha vidonda vilivyoanza kupona .CCM na ACT vyote havitakiwi  kuzumgumzia  chaguzi zilizopita.Kufanya hivyo  ni kupoteza wakati  bure. Ni  sawa na kufufua makaburi ya  wafu  "Alieleza 


Alisema kwa vyovyote itakavyokuwa ,  Zanzibar  haiwezi kujitoa katika  Muungano wa serikali  mbili ili mataifa  ya Tanganyika na zanzibar yawe na mamlaka kamili kama ilivyokuwa kabla ya Aprili 26  mwaka 1964.


"Serikali ya Rais Dk   Hussein Ali Mwinyi ina cha kuwaonyesha wananchi kwa  iliofanyika miaka mitano  iliopita .Yaliofanyika yanaonekana na kila mzanzibari .Rais Dk Mwinyi hana kazi ngumu Oktoba  mwaka huu" Alisema Mbeto.


Hata hivyo, Katibu  huyo Mwenezi  aliwataka wananchi wa mkoa wa  Kaskazini  Unguja kutazama mema waliofanyiwa na serikali ya awamu ya nane  Zanzibar na manufaa walioyapata.

WAZIRI CHANA AKUTANA NA SEKRETARIETI YA MKATABA WA LUSAKA

 

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Sekretarieti ya mkataba wa Lusaka (Lusaka Agreement) kuhusu Mkutano wa 14 wa Baraza la Usimamizi wa Mkataba wa Lusaka(LATF) unaotarajiwa kufanyika jijini Arusha kuanzia Mei 6-8, 2025.

Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika Ofisi za Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Dodoma leo Aprili, 30 2025 Mhe. Chana amesema Tanzania iko tayari kupokea  wageni zaidi ya 100 kutoka Nchi wanachama na Nchi waalikwa na kuwahakikishia usalama wao kwa kipindi chote wawapo nchini. 

Naye, Mkurugenzi wa Sekretarieti ya Mkataba wa Lusaka, Bw. Edward Phiri amesema maandalizi  ya mkutano huo yamekamilika  na  tayari viongozi mbalimbali kutoka nchi wanachama wa Mkataba wa Lusaka wameshathibitisha kushiriki.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii (anayeshughulikia maliasili), CP Benedict Wakulyamba , Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii (anayeshughulikia utalii), Bw. Nkoba Mabula, Mkurugenzi wa Wanyamapori, Dkt. Alexander Lobora pamoja na Maafisa Waandamizi kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii.



Listen Mkisi Radio