JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumatano, 4 Juni 2025

KIWANDA CHA KUSAFISHA NA KUONGEZA THAMANI MADINI ADIMU KUJENGWA KIJIJINI NGWALA,SONGWE

 

KIWANDA CHA KUSAFISHA NA KUONGEZA THAMANI MADINI ADIMU KUJENGWA KIJIJINI NGWALA,SONGWE


▪️Uendelezaji wa Mradi kuanza rasmi    Disemba 2025


▪️Ni mradi wa Madini Adimu utakaogharimu Bilioni 771


▪️Waziri Mavunde azindua zoezi la ulipwaji fidia wananchi 192


▪️Wananchi wamshukuru Rais Samia kwa mazingira ya uwekezaji


▪️Serikali kuvuna mapato ya zaidi ya Trilioni 12 


Ngwala,Songwe


Kampuni ya Mamba Minerals Ltd inayowekeza kwenye mradi wa Madini adimu imeweka wazi mpango wake wa kujenga kiwanda cha kusafisha na kuongeza thamani madini adimu kijijini,Ngwala Mkoani Songwe badala ya kusafirisha madini hayo yakiwa ghafi.


Hayo yamesemwa leo Kijijini Ngwala,Songwe wakati wa uzinduzi wa zoezi la ulipwaji fidia wananchi waguswa wa mradi takribani 192 zoezi ambalo limezunduliwa na Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde.

Akitoa maelezo ya awali,Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mamba Minerals Ltd Ndg. Ismail Diwani amesema zoezi hilo la fidia litagharimu kiasi cha Tsh 5.3 Bilioni kwa kuhusisha wananchi waguswa wa mradi 192 ambapo mpaka sasa wananchi 116 wamepokea malipo yao tayari.


“Hatua hizi ni za awali kuelekea kwenye utekelezaji wa mradi ambapo shughuli rasmi za ujenzi wa mradi zitaanza Disemba 2025 sambamba na ujenzi wa kiwanda cha kusafisha madini adimu na ujenzi wa mtambo wa kufua umeme utakaozalisha megawati 12”Alisema Ismail

Waziri Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Mamba Minerals Ltd kwa ujenzi wa kiwanda cha kusafisha madini hayo hapa nchin ikiwa ni uongezaji wa thamani wa madini hayo kabla ya kusafirishwa ikiwa ni sehemu ya kuitikia wito uliotolewa na Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan juu ya uongezaji thamani madini nchini.


“Mradi huu pamoja na Ajira,mrabaha,ushuru wa Halmashauri pia utaipa serikali mapato ya moja kwa moja ya zaidi ya Tsh 12 Trilioni wakati wote wa uhai wa mgodi.


Tutahakikisha wananchi wa Ngwala wananufaika na mradi huu mkubwa kupitia maudhui ya ndani(𝙡𝙤𝙘𝙖𝙡 𝙘𝙤𝙣𝙩𝙚𝙣𝙩) na hivyo mradi huu kuwa kichocheo cha maendeleo ya kiuchumi ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Mradi huu una wastani wa mashapo ya  Tani 18.5 milioni  za madini adimu ni kati ya miradi mikubwa  duniani ya madini adimu na hivyo itaifanya Tanzania kuwa mzalishaji wa malighafi kwa ajili ya vifaa vya matibabu,kieletroniki na ufuaji wa umeme wa upepo”Alisema Mavunde


Naye Mkuu wa Wilaya wa Songwe Mh. Solomon Itunda amesema mradi huu utachochea ukuaji wa sekta ya madini Mkoani Songwe kwa kiwango kikubwa na hivyo kuufanya mkoa huu kuwa kati ya wachangiaji wakubwa katika kukuza uchumi wa nchi kupitia sekta ya madini.

KAMPUNI YA KIZALENDO (MOFAT) YAULA MABASI YA ENDAYO HARAKA (BRT)


 Na Mwandishi wetu 


KAMPUNI ya Kizalendo ya Mofat imepewa mkataba wa miaka 12 na Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (Dart) kwa ajili ya kuendesha Awamu ya Pili ya mfumo wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT), unaotoka Gerezani hadi Mbagala. 


Kampuni hiyo ya Kizalendo ya Mofat inatarajiwa kuanza kutumia mabasi 255 yanayotumia gesi ifikapo Agosti 2025.

Akizungumza hayo hivi karibuni Mkurugenzi Mtendaji wa Dart, Dkt. Athuman Kihamia, alithibitisha kuhusu mkataba huo jana katika mahojiano ya simu akiwa nje ya nchi.


Alisema maendeleo yanakuja wakati serikali ikihamia rasmi katika kuhamisha uendeshaji wa awamu ya kwanza na ya pili ya mfumo wa BRT kwa sekta binafsi, ikiwa ni juhudi za kuongeza ufanisi na kushughulikia changamoto za muda mrefu za usafiri kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam.

''Hii ni kampuni ya kizalendo na tayari imepata mitaji na dhamana zinazohitajika kuendesha huduma hii.


"Hivyo hii ni hatua kubwa katika juhudi zetu za kutoa huduma za usafiri wa uhakika na bora kwa wakazi wa jiji. Kampuni hiyo imejitolea kuleta mabasi ndani ya muda tuliokubaliana,"alisema Dkt. Kihamia.

Mwelekeo wa kuwashirikisha zaidi waendeshaji wa ndani ulisisitizwa pia Jumatatu na Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu, aliyewaambia wahariri jijini Dar es Salaam kuwa Dart sasa inalenga kuvutia wawekezaji zaidi—hasa kwa kuwa ujenzi wa Awamu ya Kwanza na ya Pili umekamilika, huku Awamu ya Tatu ikitarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.


Kwa mujibu wa mfumo mpya, mfumo wa BRT utaendeshwa na kampuni kati ya nne hadi sita, badala ya mfumo wa sasa wa mtoa huduma mmoja unaoongozwa na UDA Rapid Transit (Udart).

UTENDAJI KAZI WA WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE WAIMARIKA KWA ZAIDI YA ASILIMIA 95

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza na viongozi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake wakati wa kikao cha tathmini ya utendaji kazi wa Wizara hizo na Taasisi kilichofanyka tarehe 03 Mei, 2025 Jijini Dodoma. Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhadisi Felchesmi Mramba.

..,..,........

📌 Dkt. Biteko apongeza; akumbusha Watendaji umuhimu wa tathmini katika kuboresha utendaji kazi

📌Ataka TANESCO kuendelea kuboresha miundombinu ya umeme; kubuni vyanzo vipya

📌 *Aziagiza Taasisi chini ya Wizara kuungana kuitekeleza Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia*

📌 *Ofisi ya Waziri Mkuu yaipongeza Wizara kutekeleza miongozo ya ufuatiliaji na Tathmini kwa asilimia 100*

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewapongeza Watendaji wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa kuendelea kuimarisha utendaji kazi na hivyo kuifanya Sekta ya Nishati kuwa na matokeo chanya katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Dkt. Biteko ametoa pongezi hizo kufuatia tathmini ya utendaji kazi iliyofanywa na Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini katika Wizara ya Nishati ambayo imeonesha kuwa katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 utendaji kazi wa Wizara/Taasisi umeimarika kwa zaidi ya asilimia 95.

Katika kikao cha Nne cha tathmini ya utendaji kazi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kilichofanyika jijini Dodoma, Dkt. Biteko amesema kuwa, tathmini hiyo inasaidia kujiimarisha hasa ikizingatiwa kuwa Sekta ya Nishati ina muhimu mkubwa kiuchumi na kijamii.

“Sekta hii ni muhimu sana nchini kwa kuwa ni Sekta ya huduma na sekta ya uchumi hivyo ikilegalega italeta malalamiko, ningependa kuona sekta hii inaendelea kuwa na matokeo mazuri kwa wananchi.” Amesema Dkt. Biteko

Katika kikao hicho, Dkt. Biteko ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuendelea na kasi ya ukarabati wa miundombinu ya umeme pamoja na kuendelea kutafuta vyanzo vipya vya umeme.

Aidha, ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kwa kasi iliyofanya ya kupeleka umeme vijijini na kuwezesha vijiji vyote kupata umeme pia kwa kuendelea na kasi ya kupeleka umeme vitongojini.

Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia, Dkt. Biteko amezitaka Taasisi zilizo chini ya Wizara hususan, REA, TPDC na TANESCO kuunganisha nguvu katika kutekeleza Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia ili ikue na kufanikiwa na hivyo kutimiza lengo la Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha kuwa wananchi wanahama kutoka matumizi ya Nishati isiyo safi kwenda kwenye matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Dkt. Biteko amekipongeza Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini katika Wizara ya Nishati kwa kutekeleza jukumu lao kwa ufanisi na kukumbusha Watendaji wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kuwa, zoezi hilo la tathmini linapaswa kuwa ni endelevu kutokana na umuhimu wake katika kuboresha utendaji kazi.

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith.Kapinga kwa upande wake, amezipongeza Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Nishati pamoja na Idara na Vitengo vya Wizara ya Nishati kwa utendaji kazi wenye kuleta matokeo kama ambavyo tathmini ya utendaji kazi iliyotolewa ilivyoonesha kuwa ufanisi wa kazi umeendelea kuimarika.

Aidha amezitaka Taasisi chini ya Wizara ya Nishati kuibeba Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia ili kufikia lengo la Serikali la kufikisha asilimia 80 ya Watanzania wanaotumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo 2034.

Awali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba alisema kuwa kikao hicho cha tathmini ya utendaji kazi wa Wizara na Taasisi zake ni cha nne kutoka vikao vivyo vimeanza kufanyika.

Alieleza kuwa, kutoka zoezi la kupima utendaji kazi wa Wizara na Taasisi lianze kufanyika limeleta ufanisi hasa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali pamoja na mipango ya Wizara.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Serikali, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bi. Sakina Mwinyimkuu ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kutekeleza miongozo iliyowekwa na Ofisi hiyo ya ufuatiliaji na tathmini ambapo ameeleza kuwa Wizara ya Nishati imetekeleza miongozo iliyowekwa kwa asilimia 100.

Pia amempongeza Dkt. Doto Biteko kwa dhamira yake ya dhati katika kusimamia utendaji kazi wa Serikali hasa Sekta ya Nishati ambayo anaisimamia akiwa ni Waziri wa Nishati.

Vilevile, ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kutoa motisha kwa Taasisi na Idara/Vitengo zilizofanya vizuri zaidi katika tathmini ya utendaji kazi hali ambayo inaongeza ari ya kazi.

Taasisi zilizofanya vizuri Katika tathmini ya utendaji kazi iliyofanyika katika robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 ni Wakala wa Nishati Vijijini (REA) aliyeshika nafasi ya kwanza, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) aliyeshika nafasi ya pili na Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) aliyeshika nafasi ya tatu.  

Aidha, Idara/Vitengo vya Wizara ya Nishati vilivyofanya vizuri Katika tathmini ya utendaji kazi iliyofanyika katika robo ya tatu ya mwaka 2024/2025 ni Kitengo cha Ugavi na Manunuzi (nafasi ya kwanza), Kitengo cha Sheria (nafasi ya pili), na Kitengo cha TEHAMA (nafasi ya tatu).

Mikoa ya Kitanesco iliyofanya vizuri katika tathmni ya utendaji kazi ni Manyara (nafasi ya kwanza), Arusha (nafasi ya pili) na Simiyu (nafasi ya tatu).

Hata hivyo ilielezwa kuwa kwa ujumla ufanisi wa utendaji kazi wa Idara na Vitengo vya Wizara pamoja na Taasisi zake umeendelea kuimarika kwa zaidi ya asilimia 95.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt, James Mataragio, Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Menejimenti ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake pamoja na Mameneja wa Mikoa wa TANESCO.

VITONGOJI 284 ARUMERU MASHARIKI VYAFIKIWA NA UMEME


...........

📌  Ni kati ya Vitongoji 330 vya Jimbo la Arumeru Mashariki.

📌Kapinga asema upelekaji umeme unafanyika kwa  awamu kulingana na upatikanaji wa fedha

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imevifikishia huduma ya umeme Vitongoji 284 katika Jimbo la Arumeru Mashariki kati ya Vitongoji 330.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Juni 03, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Arumeru Mashariki, Mhe. Dkt. John Danielson Pallangyo aliyeuliza ni  lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme wa REA katika Vitongoji 37 ambavyo vipo gizani katika Jimbo la Arumeru Mashariki.

"Mheshimiwa Mwenyekiti, Vitongoji 17 vipo katika hatua ya utekelezaji kupitia Mradi wa Ujazilizi (Densification IIB) na mradi wa kupeleka umeme katika Vitongoji Awamu ya Pili  A (HEP IIA), aidha, katika Vitongoji 29 zabuni imetangazwa ili kupata Wakandarasi wa kutekeleza miradi kupitia mradi wa kupeleka umeme Vitongojini Awamu ya Pili B (HEP IIB). 

Amesema kukamilika kwa miradi hiyo, kutawezesha vitongoji vyote vya Jimbo la Arumeru Mashariki kufikiwa na umeme.

Akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Arumeru Mashariki, Mhe. Dkt.John Danielson Pallangyo aliyeuliza kuhusu  Kata za Arumeru Mashariki zinazo pata maji kutoka msitu wa mlima Arumeru na kuwa na  flouride ambapo Kampuni ya Kweka imejitolea kuweka mtambo wa kusafisha lakini kinachohitajika ni umeme,   Mhe. Kapinga amesema tayari Serikali imetenga fedha katika mwaka ujao wa fedha kukipelekea umeme wa uhakika Kitongoji cha Seneto Kata ya Legeruki kwa ajili ya kutibu flouride katika maji.

Akijibu swali la Mbunge wa Moshi Vijijini, Mhe. Profesa Patrick Alois Ndakidemi aliyeuliza Serikali itakiunganishia lini umeme Kitongoji cha Orera kilichopo Kijiji cha Mweka, Mhe. Kapinga amesema katika Jimbo la Moshi Vijijini yupo Mkandarasi anayetekeleza miradi ya kupeleka umeme kwenye Vitongoji 15 vya kila Mbunge na kuongeza kuwa kitongoji hicho kipo katika orodha hiyo ya Mkandarasi.

Akijibu swali la Mbunge wa Kondoa Mjini, Mhe. Ally Makoa aliyeuliza Serikali itapeleka lini umeme kwenye mitaa ya Mongoroma, Chandimo na Hachi,  Mhe. Kapinga amesema Serikali imeipelekea umeme mitaa ya Kondoa Mjini ambapo imebaki mitaa hiyo mitatu na kuongeza kuwa itatengwa fedha katika bajeti ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuifikishia mitaa hiyo umeme.

Mhe. Kapinga ameongeza kuwa upelekaji wa umeme unafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha na bajeti ambayo imetengwa.

Akijibu swali la Mbunge wa Mwibara, Mhe. Charles Kajage aliyeuliza kuhusu lini Serikali itavipelekea umeme Vitongoji vya Jimbo la Mwibara ambavyo havina umeme, Mhe. Kapinga amesema Jimbo la Mwibara lina miradi ya Vitongoji ambayo inaendelea kutekelezwa. 

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Mhe. Rita Kabati aliyeuliza kauli ya Serikali kuhusu uwepo wa nguzo Kata ya Ilula Wilaya ya Kilolo toka mwezi wa 11 mwaka jana na hadi leo umeme haujawaka, Mhe. Kapinga amesema hadi kufikia mwezi wa saba eneo hilo litakuwa limefikiwa na huduma ya umeme.

Jumatatu, 2 Juni 2025

WAZIRI AWESO ATAKA WANANCHI WALINDE VYANZO VYA MAJI


......................

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso amewataka wananchi kulinda mazingira ya vyanzo vya maji kwa kuacha kukata miti ovyo na kufanya shughuli za kibinadamu ili kuepuka ukame. 

Ametoa wito huo mara baada ya kutembelea mabanda ya maonesho wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani leo Juni 2, 2025 yanayoendelea kwenye Viwanja vya Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete jijini Dodoma. 

Mhe. Aweso amesema kuwa uwepo kwa rasilimali za maji toshevleu ni usalama wa taifa kwakuwa uwepo wa maji ni uhakika wa chakula, nishati ya umeme pamoja na mipango ya kimaendeleo ambapo yote hayo yanategemea na mazingira endelevu.

Pia, Waziri Aweso alisema ni wakati sasa Watanzania watambue kuwa athari za mazingira ziwe funzo, akitolea mfano Mto Ruvu mkoani Pwani ulivyokauka kutokana na mabadiliko ya tabianchi ambayo yalisababishwa na binadamu wenyewe. 

“Athari za mazingira ziko wazi kwa mfano ukienda Pangani athari zikio wazi, leo tunaona bahari imekula mji na hivyo kina cha maji kinaongezeka kina kwahiyo changamoto hizi za kimazingira tunazoziona sasa ziwe funzo kwetu,” alisema. 

Pamoja na changamoto hizo, alishukuru na kuipoingeza Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kuandaa mikakati thabiti na hatua madhubuti inazochukua katika kuyasimamia na kuyatunza mazingira.

Amesema hayo yote yanafanyika kutokana na jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ni kinara wa kusimamia agenda ya mazingira.

“Nashukuru kwa kupata nafasi ya kutembelea mabanda haya, hakika Ofisi ya Makamu wa Rais mmejipanga na sisi kama Wizara ya Maji tutaendelea kushirikiana na wadau wote katika kuyalinda na kuyatunza mazingira ili kuhakikisha Tanzania inakuwa bora na salama, kama mtakumbuka tumefanya mabadiliko ya Sera ili yaendane na mazingira,” alisema Mhe. Aweso.

 

Maonesho hayo ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 5, 2025 ambayo ndio kilele.

 

TAWA MGUU SAWA KUDHIBITI WANYAMAPORI WAKALI IKUNGI

.................

Ester Maile Dodoma

Mamlaka ya usimamizi wa wanyamapori(TAWA) imeanza kutekeleza mikakati ya kudhibiti makundi ya wanyamapori wakali na waharibifu hususan tembo katika wilaya ya Ikungi mkoani Singida.

Haya yamebainishwa na Naibu Waziri wa Malisili na Utalii, Mhe. Dunstan Kitandula(Mb) alipokuwa akijibu swali la  Miraji Jumanne Mtaturu ambaye alitaka kujua Serikali ina mpango gani wa kuondoa Tembo Singida Mashariki ambao wanasumbua na kuharibu mashamba ya Wananchi.

Aidha  Kitandula alisema Katika kudhibiti tembo wanaovamia na kuharibu mashamba ya wananchi wa Singida Mashariki, Serikali kupitia TAWA imeendelea  kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kuweka vikosi viwili vyenye Askari 24 wakiwemo Wahifadhi 13 na Askari Wanyamapori wa Vijiji (VGS) 11 na kutoa magari matatu (3).

Vilevile, TAWA imeimarisha matumizi ya ndege nyuki kwa kuwafukuza tembo kutoka kwenye maeneo ya wananchi na kuwarejesha hifadhini. Mathalan, kati ya mwezi Novemba 2024 na Mei 2025 kikosi maalum cha Askari Wahifadhi 18 na VGS 6 kikitumia ndege nyuki 2 na mabomu baridi kiliweka kambi katika Jimbo la Singida Mashariki, Wilayani Ikungi na kufanikiwa kudhibiti makundi 23 ya tembo kwa kuwarudisha ndani ya hifadhi. 

Serikali inaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na wanyamapori wakali na waharibifu wakiwemo tembo. Mathalan, kwa kipindi cha Julai 2024 hadi Mei 2025 elimu hiyo imetolewa kwa wananchi 517 na Askari 110 wa Jeshi la Akiba katika Kata za Mkiwa, Igombwe, Iglansonia, Mang’onyi, Issuna, Ntuntu na Ikungi.

‘Serikali itaendelea kutumia teknolojia ikiwemo ndege nyuki na kufunga visukuma mawimb (GPS Satellite Collars) ili kufuatilia mienendo ya tembo na kuwadhibiti’ alisisitiza  Kitandula.

Jumapili, 1 Juni 2025

PROFESA MDEBE: MATUMIZI YA NISHATI JADIDIFU YAMESAIDIA KUPUNGUZA VIFO VYA WATOTO NJITI


Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Shule ya Madini na Jiosayansi , Profesa Evelyne Mbede (wa pili kushoto) na  wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wadau wa Nishati Jadidifu Tanzania (TAREA), Prosper Magali wakiwa na Katibu Mtendaji wa TAREA, Mhandisi Mathew Matimbwi akifuatilia. akitembelea madanda anuai ya wadau wa nishati jadidifu kwenye hafla ya ufungaji wa Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu yaliofanyika jijini Dar es Salaam. 

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Shule ya Madini na Jiosayansi , Profesa Evelyne Mbede (wa pili kushoto) na  wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wadau wa Nishati Jadidifu Tanzania (TAREA), Prosper Magali wakiwa na Katibu Mtendaji wa TAREA, Mhandisi Mathew Matimbwi akifuatilia. akitembelea madanda anuai ya wadau wa nishati jadidifu kwenye hafla ya ufungaji wa Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu yaliofanyika jijini Dar es Salaam. 

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Shule ya Madini na Jiosayansi , Profesa Evelyne Mbede (wa pili kushoto) akitembelea madanda anuai ya wadau wa nishati jadidifu kwenye hafla ya ufungaji wa Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mtendaji wa TAREA, Mhandisi Mathew Matimbwi akifuatilia.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Shule ya Madini na Jiosayansi , Profesa Evelyne Mbede akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufunga rasmi Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu yaliofanyika jijini Dar es Salaam.

Katibu Mtendaji wa TAREA, Mhandisi Mathew Matimbwi akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya hafla ya kufunga Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu yaliofanyika jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu

MHADHIRI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Shule ya Madini na Jiosayansi , Profesa Evelyne Mbede amesema matumizi ya Nishati Jadidifu yamesaidia kupunguza vifo vya watoto wanaozaliwa kabla ya miezi yao kutimia (njiti).

 Profesa Mbede ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu aliyasema hayo Mei 29, 2025 wakati akifunga maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

“Zamani wajawazito walikuwa wakijifungua kwa shida vijijini kutokana na kukosa umeme hadi kusababisha watoto waliozaliwa chini ya muda wao (njiti) kupoteza maisha lakini leo hii kwa kutumia nishati jadidifu imesaidia kuokoa maisha ya watoto hao,” alisema Mbede.

Alisema nishati jadidifu hivi sasa inatumika katika vituo vya afya na zahanati mbalimbali nchini na si kwa Tanzania tu bali dunia nzima kusaidia nishati ya umeme kwenye vituo hivyo muhimu kwa jamii.

Profesa Mdebe alisema kumalizika kwa maadhimisho hayo ndio mwanzo wa maandalizi ya maadhimisho ya msimu mwingine wa 2026 mwakani.

Alisema maadhimisho hayo yamekuwa yakipanua wigo wa ubunifu, kwani vijana wengi wamekuwa wakiibuka na bunifu mbalimbali na kuongeza matumizi ya nishati jadidifu na kusaidia maeneo yenye uhitaji, ambako hakuna umeme wa TANESCO na REA na kutatua changamoto za wananchi.

Profesa huyo alisema Tanzania kushiriki katika maadhimisho hayo ni kuendana na hali ya mazingira dunia ili kufikia malengo ya 2030 ya kukabiliana na tabianchi.

 “Maonesho haya yanatija sana, kama nchi tumetoka mbali zamani tulikuwa tukitegemea umeme wa Tanesco pekee lakini hivi sasa tunazalisha umeme kwa kutumia vifaa mbalimbali na hii ni hatua kubwa,” alisema Mbede.

Maadhimisho hayo yaliandaliwa na Jumuiya ya Wadau wa Nishati Jadidifu Tanzania (TAREA) kwa kushirikiana na Wizara ya Madini na wadau mbalimbali wa sekta hiyo.

Jumamosi, 31 Mei 2025

WAZIRI MKUU AKUTANA NA MWENYEKITI WA CHAMA CHA URAFIKI WA WABUNGE WA JAPAN NA AFRIKA

................

Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa Mei 29, 2025 alikutana na kuzungumza na Mwenyekiti  wa Chama cha Wabunge wa Japan cha Urafiki na Afrika (Africa Union Parliamentarians Friendship) Mheshimiwa  Ichiro Aisawa, kwenye Ofisi za Bunge la Japan.

Katika mazungumzo yao walijadili kuhusu kuendeleza urafiki kati ya Bunge la Tanzania na Bunge la Japan.

Pia, walijadili kuhusu masuala mbalimbali ya uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na Japan, pamoja na kumkaribisha kutembelea Tanzania ili kujionea vivutio mbalimbali ya utalii.


 

Ijumaa, 30 Mei 2025

STAMICO YAANIKA FURSA YA NISHATI MBADALA KWA WAJASIRIAMALI MANISPAA YA UBUNGO

Afisa Masoko Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Bw. Mark Stephano (wa kwanza kushoto) akitoa ufafanuzi kwa Afisa Mazingira wa Manispaa ya Ubungo Bi. Jesca Stanley kuhusu nishati mbadala ya Rafiki Briquettes inavyofanya kazi kwa ufanisi, wakati semina ya wajasiriamali iliyofanyika leo Mei 30, 2025, Dar es Salaam. 

Afisa Mazingira wa Manispaa ya Ubungo Bi. Jesca Stanley akimkabidhi Cheti cha pongezi Afisa Masoko Mwandamizi wa STAMICO, Bw. Bilton Otto ikiwa ni sehemu shukrani kwa Shirika hilo baada ya kudhamini mafunzo  wajasiriamali zaidi ya 700 kutoka Manispaa hiyo.

Picha za matukio mbalimbali.

.............

NA NOEL RUKANUGA, DAR ES SAlAAM

Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limewajengea uwezo wajasiriamali zaidi ya 700 kutoka Manispaa ya Ubungo kuhusu namna ya kuchangamkia fursa ya kuwekeza katika nishati mbadala ya Rafiki Briquettes, ambayo ni rafiki kwa mazingira na nafuu kwa matumizi ya kila Mtanzania.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo wakati akifungua semina hiyo, iliyofanyika leo, Mei 30, 2025, jijini Dar es Salaam, Afisa Mazingira wa Manispaa hiyo, Bi. Jesca Stanley, amesisitiza umuhimu wa kutumia nishati mbadala si tu kwa ajili ya kulinda mazingira, bali kama fursa ya kiuchumi kwa vijana na jamii kwa ujumla.

Bi. Stanley amesema kuwa Manispaa ya Ubungo itaendelea kutengeneza mazingira rafiki pamoja na kuwawezesha vijana kwa kuwajengea uwezo katika matumizi ya nishati mbadala, ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu na uhifadhi wa mazingira Kitaifa.

"Watu wenye sifa wafike katika Ofisi ya Maendeleo ya jamii Manispaa ya Ubungo kwa ajili ya kupewa utaratibu wa kupata mikopo na baada ya kupata tunaomba watumie kulingana na vigezo walivyopewa  kupata mikopo jambo ambalo litasaidia  kufanya marejesho" amesema Stanley.

Kwa upande wao, Afisa Masoko Mwandamizi wa STAMICO, Bw. Bilton Otto, pamoja na Afisa Masoko, Bw. Mark Stephano, wameeleza kuwa kuna fursa kubwa ya biashara katika nishati mbadala ya Rafiki Briquettes kutokana na gharama yake kuwa nafuu na manufaa ya kimazingira.

"Tumefadhili wajasiriamali zaidi ya 700 ili waweze kupata mafunzo katika semina hii, mwitikio ni mkubwa na wengi wameonesha nia ya kuwa mawakala wa bidhaa ya nishati mbadala ya Rafiki Briquettes baada ya kuona umuhimu na faida katika matumizi ukilinganisha na nishati nyengine" amesema Bw. Bilton Otto.

Bw. Stephano amesema kuwa STAMICO imekuja na bidhaa hiyo kwa lengo la kuwasaidia watanzania kuondokana na ukosefu wa nishati ya kupikia, hivyo ni wakati wa vijana kuanzishaji vikundi kwa ajili ya kupata mkopo kwa kushirikiana na Manispaa ya Ubungo kwani uhitaji ni mkubwa.

Amebainisha kuwa kwa mujibu wa takwimu mbalimbali, Mkoa wa Dar es Salaam ni miongoni mwa mikoa yenye matumizi makubwa ya mkaa, ambapo takribani tani milioni moja hutumika kwa mwaka.

"STAMICO tumekuja na bidhaa hii kwa lengo la kuonesha fursa zilizopo, tukishirikiana na Manispaa ya Ubungo ili kuwawezesha wajasiriamali kupitia mikopo rasmi na kuhamasisha vijana kuwa mawakala wa nishati mbadala ya Rafiki Briquettes," amesema

Nao baadhi ya wajasiriamali wa Manispaa ya Ubungo walioshiriki semina hiyo, akiwemo Asinath Jameson na Julius Msele, wamelishukuru Shirika la STAMICO kwa kudhamini mafunzo  kwani yamekuwa na msaada mkubwa kwao pamoja na kupatiwa fursa ya kipekee ya kuingia katika biashara ya nishati mbadala ya Rafiki Briquettes

CHAMA CHA MAPINDUZI CHAZINDUA ILANI YAKE YA UCHAGUZI MKUU MWAKA 2025

Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 yazinduliwa leo katika mkutano mkuu maalum wa chama cha mapinduzi (CCM) Taifa unaonedelea katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Center Jijini Dodoma.


Akizundua ilahi hiyo Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) na Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Katibu Mkuu na mgombea mwenza wa Chama cha Mapinduzi Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar na Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, makamu mwenyekiti wa CCM Mhe. Stephen Wasira pamoja na viongozi wengine wa chama hicho.







WAKUU WA MAJESHI YA POLISI NCHI ZA SADC KUKUTANA TANZANIA


 

Listen Mkisi Radio