JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumanne, 13 Mei 2025

ZAIDI YA NYUMBA 800 MTWARA KUUNGANISHWA NA MFUMO WA GESI YA KUPIKIA – KAPINGA


*📌 Awasisitiza TPDC na REA kushirikiana ili kuongeza kasi ya kuunganisha gesi majumbani*


*📌 Asema Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia  ni endelevu.*


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) inatarajia kuunganisha mfumo wa gesi ya kupikia katika nyumba takribani 865 mkoani Mtwara kwenye maeneo ambayo yana miundombinu ya bomba la gesi.


Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Mei 13, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Tunza Malipo aliyetaka kufahamu mkakati wa Serikali katika kuunganisha gesi kwa Taasisi na Nyumba za Wananchi mkoani Mtwara kwa ajili ya kupikia.

 

"Katika Mkoa wa Mtwara, Serikali imeshapeleka miundombinu ya usambazaji gesi asilia katika baadhi ya maeneo ambapo jumla ya nyumba 425 na Taasisi nne (4) zimeunganishwa na mtandao wa matumizi ya gesi asilia katika maeneo ya Mtwara mjini."  Amesema  Kapinga


Ameongeza kuwa,  katika nyumba hizo 865 zitakazounganishwa na mfumo,  Serikali imeshafanya usanifu wa kihandisi kwa ajili ya kwenda hatua ya kuunganisha.


Ameweka bayana kuwa,  tayari Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati,  Mhe. Dkt. Doto Biteko ameshauagiza  Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na TPDC  kushirikiana ili  kuongeza kasi ya kuunganisha gesi asilia kwa wananchi wa Mtwara na Lindi. 


Akijibu swali la Mbunge wa Temeke, Mhe. Dorothy Kilave aliyeuliza kuhusu Serikali kuona umuhimu wa kuharakisha kuunganisha gesi kwenye masoko kama vile Sterio, Temeke, Keko na Mtoni kwa ajili ya Mama Lishe na Baba Lishe, Mhe. Kapinga amesema  Serikali inao mkakati kupitia TPDC kuunganisha gesi asilia katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam. 


Ameeleza kuwa, kwa masoko ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja Serikali imeyachukua na itaenda kuyafanyia tathmini.


 Mbunge wa Momba, Mhe. Mhe. Kondesta Sichwale kwa upande wake aliuliza kuhusu suala la  mitungi ya ruzuku kufikia idadi ndogo ya wananchi na kuishauri Serikali kupeleka mitungi ya ruzuku kwa watendaji wa Kata ili kila mwananchi achukukulie hapo kwa kitambulisho cha NIDA.


 Kuhusu suala hilo Kapinga amesema Serikali inaanza kugawa mitungi ya ruzuku takribani  420,000 ambapo utaratibu ni kila mwananchi kuchukua mtungi wa gesi kwa kutumia namba yake ya NIDA ama kitambulisho cha NIDA  ili kumuwezesha mwananchi mmoja kupata mtungi mmoja.


Ameongeza kuwa,  Serikali pia ilitenga mitungi  3,255 kwa kila Wilaya ikiwa ni hatua ya kuanza kwa mkakati wa nishati safi ya kupikia ambapo amewahakikishia Wabunge kuwa mkakati huo ni wa miaka kumi na endelevu.


Mhe. Kapinga ameongeza kuwa katika kipindi cha miaka kumi asilimia 80 ya watanzania watakuwa wanatumia nishati safi ya kupikia ambayo ndio maono ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

KIJANA KABLA YA KUOA SOMA HII

 

Kijana wangu njoo  usikie maneno yangu

 Usioe mwanamke ambaye kwa kumtazama tu unajua ana matunzo ,anaweza kuwa anajitunza mwenyewe anapendeza ,au ana matunzo nyuma usiyoyajua ..endapo unajua maisha Yako ni ya kuungaunga usisogee Kaa pembeni. 


Chukuaaliye pauka au wa kawaida ili angalau wewe unatakapokuwa unampa mafuta ya 3000 anafurahi na kuona anathaminiwa ,, lakini ukichukua mtu anapaka mafuta ya 140000, sabuni ya 40000

Wakati wewe laki na40 unaipigia hesabu za mwezi mzima 😃😃 utaenda pasuka kichwa huko ....


Mwanamke anapiga pamba za 700k 

Wewe unawaza kumzawadia kitenge cha morogo utaenda kuumia

OA mwanamke anayefanana na kiwango chako Cha maisha utaishi kwa furaha ..OA mwanamke anayezidi kiwango chako Cha maisha ukapate presha ...


Usije sema sikusiki ..umesikia Leo


#PASTORLEAH 

.

WAZIRI MKUU ASHIRIKI MDAHALO WA MAWAZIRI WAKUU KWENYE JUKWAA LA MAAFISA WATENDAJI WAKUU


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza katika mdahalo wa Mawaziri Wakuu kuhusu namna Sekta ya Umma inavyoweza kushirikiana sekta binafsi ili kuchochea maendeleo, mjadala huo umefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hotel ya Sofitel Mei 12, 2025 jijini Abidjan, Ivory Coast. Mawaziri Wakuu walioshiriki mjadala huo ni Waziri Mkuu wa Cameroon, Joseph Dion Ngute,Waziri Mkuu wa Ivory Coast Robert Beugré Mambé pamoja na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Guinea Amadou Oury Bah

MACHINGA DODOMA WAMPONGEZA RAIS SAMIA KWA UJENZI WA SOKO LA KISASA

 

▪️Ni soko kubwa la kipekee la Machinga Complex


▪️Machinga Wanawake Dodoma wazindua Umoja wao


▪️RC Senyamule ataka Jiji kuongeza maeneo ya kufanyia biashara 


▪️Mbunge Mavunde awataka Machinga Dodoma kuchangamkia Mkopo wa Bilioni 7 za Jiji


*Dodoma*


Umoja wa Wanawake Machinga Dodoma(UWAMADO) wamempongeza Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa ujenzi wa soko la kisasa la Machinga Complex na miundombinu ya kisasa ya soko hilo ambalo ni la kipekee nchini.


Hayo yamesemwa jana wakati wa uzinduzi wa chama cha UWAMADO uliofanyika kwenye eneo la soko la Machinga Complex kwa kuzinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mh. Rosemary Senyamule

Akisoma Risala Katibu wa UWAMADO Bi. Mariam Kajembe amesema umoja huo umelenga kuwaleta wanawake Machinga pamoja ili kujijenga na kujiimarisha uchumi.


Aidha pia UWAMADO umempongeza Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa ujenzi wa Soko la Machinga Complex ambalo limesaidia kuwaleta pamoja wafanyabiashara wengi wadogo pamoja ambao awali hawakuwa katika maeneo rasmi na hivyo kuwafanya kutokuwa rasmi.


Akitoa hotuba yake,Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mh. Rosemary Senyamule amewapongeza UWAMADO kwa kuamua kuanzisha umoja wao ambao utawasaidia kujiendeleza zaidi na kujiimarisha kiuchumi.

“Jambo hili la kuanzisha umoja ni jambo jema,hakikisheni umoja unafikia malengo mliyokusudia.


Mh. Rais kawajengea soko kubwa na zuri,soko hili liwe kichocheo cha ukuaji wenu kimtaji na kibiashara.


Niwatake Uongozi wa Jiji la Dodoma kuendelea kubuni na kuanzisha maeneo mapya ya kuwapanga vizuri wafanyabiashara wadogo wa Dodoma”Alisema Senyamule

 

Akitoa salamu zake Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh. Anthony Mavunde amewapongeza UWAMADO kwa kuona umuhimu wa kukaa pamoja kujiinua kiuchumi na kuwataka kuchangamkia fursa ya mikopo ya asilimia 10% ya mapato ya ndani ya Jiji ambayo kiasi cha Shilingi Bilioni 7 kimetengwa kwa ajili ya kuwawezesha wakina mama,vijana na watu wenye ulemavu.

Jumatatu, 12 Mei 2025

INEC YAGAWA MAJIMBO YAANZISHA CHAMAZI NA KIVULE DAR

........................

TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imeanzisha majimbo mapya nane nchini kote, ambapo jijini Dar es Salaam, majimbo mawili ya Chamazi na Kivule yameanzishwa kutokana na mgawanyo wa majimbo ya Mbagala wilayani Temeke na Ukonga Wilaya ya Ilala.

Majimbo mapya yatakuwa sehemu ya Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge, unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, ambapo Mwenyekiti wa INEC, Jaji wa Rufani Jacob Mwambegele, amesema tume yake imefikia uamuzi huo baada ya kupitia maombi kutoka kwenye mikoa mbalimbali nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo, Jaji Mwambegele amesema uamuzi huo umefanyika kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 75(1), (2) na (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 ikisomwa pamoja na Kanuni ya 18(7) ya Kanuni za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi za Mwaka 2024.

Ameyataja majimbo hayo kuwa ni Jimbo la Kivule amabalo limegawanywa kutoka Jimbo la Ukonga na Jimbo la Uchaguzi la Chamazi lililogawanywa kutoka Jimbo la Mbagala yote ya mkoani Dar es Salaam.

“Mkoani Dodoma limeanzishwa jimbo jipya moja, ambapo Jimbo la Uchaguzi la Dodoma Mjini limegawanywa na kuanzishwa jimbo jipya la Uchaguzi la Mtumba na Mkoani Mbeya limeanzishwa jimbo jipya moja, ambapo Jimbo la Uchaguzi la Mbeya Mjini limegawanywa na kuanzishwa Jimbo jipya la Uchaguzi la Uyole,” amesema.

Jaji Mwambegele ameongeza kuwa, Mkoani Simiyu limeanzishwa jimbo jipya moja ambapo Jimbo la Uchaguzi la Bariadi limegawanywa na kuanzishwa Jimbo jipya la uchaguzi la Bariadi Mjini.

“Huko Geita yameanzishwa majimbo mawili, Jimbo la Busanda limegawanywa na kuanzishwa Jimbo jipya la Katoro na Jimbo la Chato likigawanywa pia na kuanzishwa Jimbo jipya la Chato Kusini.

“Mkoani Shinyanga limeanzishwa jimbo jipya moja, ambapo Jimbo la Uchaguzi la Solwa limegawanywa na kuanzishwa Jimbo jipya la Uchaguzi la Itwangi,” amesema Jaji Mwambegele mbele ya wanahabari.

SERIKALI INABORESHA MIUNDOMBINU YA UMEME KIBITI KUONDOA CHANGAMOTO YA UMEME- KAPINGA


.......................

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) inatekeleza miradi mbalimbali ya matengenezo na ukarabati wa njia za kusafirisha na kusambaza umeme katika Wilaya ya Kibiti ili kuondokana na tatizo la kukatika kwa umeme kunakotokana na uchakavu wa miundombinu hiyo.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Mei 12, 2025 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Kibiti, Mhe. Twaha Mpembenwe aliyetaka kufahamu mkakati wa Serikali kutatua tatizo la kukatika kwa umeme Jimbo la Kibiti. 

Ameitaja Mikakati hiyo ni kubadili nyanya za umeme kwa kuweka zenye uwezo mkubwa, kubadili nguzo za umeme na kuweka za zege, kubadili Pin insulators na kuweka mpya, na kufunga vidhibiti matatizo (fault auto recloser) kwenye line zenye urefu wa zaidi ya Kilomita 50.


 

WACHIMBAJI GEITA WAMPONGEZA RAIS SAMIA KWA MAFANIKIO MAKUBWA YA SEKTA YA MADINI

 

▪️Wachimbaji Madini wapongeza upatikanaji wa Leseni na mazingira rafiki ya biashara


▪️Waziri Mavunde aainisha mafanikio 16 ya Rais Samia kwenye sekta ya Madini


▪️Aagiza uanzishwaji wa Soko la Dhahabu Katoro


▪️RC Shigela aja na mikakati mizito ya kupaisha sekta ya madini Geita


*Katoro,Geita*


Wachimbaji na Wafanyabiashara wa Madini wa Mkoa wa Geita wamempongeza Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana kupitia sekta ya madini katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake.

Hayo yamesemwa jana kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na wachimbaji hao katika eneo la mnada wa zamani Katoro,Geita kwa lengo la kumpongeza Rais Samia kwa mafanikio yaliyopatikana kupitia sekta ya madini.


Akitoa maelezo ya awali,Mwenyekiti wa Chama cha Wachimba Madini Mkoa wa Geita(GEREMA) Ndg. Titus Kabuo amesema dhumuni kubwa la kusanyiko hilo ni kumpongeza Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa kuiboresha sekta ya madini na kuweka mazingira rafiki ya uchimbaji na ufanyaji biashara hali inayopelekea kukua kwa shughuli za uchimbaji na kuathiri chanya maendeleo ya wachimbaji na uchumi wa nchi.

Naye Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimba Madini Tanzania(FEMATA) Ndg. John Bina amesema katika kipindi cha miaka minne ya Rais Samia  sekta ya madini imeshuhudia mabadilko makubwa hasa katika upatikanaji wa Leseni kwa wachimbaji na hatua iliyoanzwa na serikali ya kufanya utafiti wa kina ili kuwaongoza vyema wachimbaji madini nchini.


Akiwasilisha hotuba yake,Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde ameyataja mafanikio 16 ya Rais Samia S. Hassan katika kuipaisha sekta ya madini kubwa ikiwa ni kuongezeka kwa mchango wa sekta ya madini kwenye pato la Taifa kufikia 10.1%,ununuzi wa Dhahabu kupitia Benki Kuu,Kuongezeka kwa makusanyo ya maduhuli kuelekea lengo la kukusanya Shilingi Trilioni moja na upatikanaji wa mitambo ya kuchoronga 15 kwa ajili yaa wachimbaji wadogo.

Aidha, Waziri Mavunde ametumia fursa hiyo kukipandisha hadhi kituo cha ununuzi wa dhahabu cha Katoro na kuwa soko kamili la Dhahabu la Katoro.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti wabunge Joseph Msukuma na Tumaini Magesa wamempongeza Rais Samia kwa kuweka mazingira rafiki ya biashara ambayo yamesaidia kupatikana kwa maendeleo makubwa na kukuza uchumi wa watu wa Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mh. Martin R. Shigela amesema Mkoa wa Geita umejipanga kuchochea shughuli za madini kwa kuboresha mazingira ya uchimbaji ili kukuza uchumi wa  wananchi wa mkoa wa Geita kupitia upatikanaji wa Leseni zaidi ya 5308 na mitambo ya Uchorongaji ambayo Mh. Rais ameitoa kwa kwa wachimbaji wadogo.

Jumapili, 11 Mei 2025

NYAHOZA AKIPONGEZA CHAMA CHA CCK KWA KUMPATA MGOMBEA URAIS

Naibu Msajili wa vyama vya siasa nchini Sisty Nyahoza akizungumza na wajumbe wa Chama Cha Siasa Cha Kijamii (CCK) katika mkutano Mkuu maalum wa Chama hicho kwa ajili ya kuwachagua na kuwapitisha wagombea nafasi ya Urais wa Tanzania Bara na Zanzibar ambao umefanyika tar 10/5/2025 jijini Dar es salaam.

Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Kijamii cha CCK David Daudi Mwaijolele ambaye pia amepitishwa kwa kupigiwa kura kugombea nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bara akizungumza katika mkutano Mkuu maalum wa Chama hicho ambao umefanyika tar 10/5/2025 jijini Dar es salaam.

Aisha Salum Hamadi ambaye amepitishwa kugombea nafasi ya Urais kupitia Chama cha Kijamii cha CCK Zanzibar akizungumza na wajumbe wa chama hicho katika mkutano Mkuu maalum wa Chama hicho ambao umefanyika tar 10/5/2025 jijini Dar es salaam.

Viongozi wa Kitaifa wa Vyama vya siasa waliohudhuria katika katika mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha siasa cha Kijamii cha CCK ambao umefanyika tar 10/5/2025 jijini Dar es salaam.

Wajumbe mbalimbali waliohudhuria katika mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha siasa cha Kijamii cha CCK ambao umefanyika tar 10/5/2025 jijini Dar es salaam. 

........................

NA MUSSA KHALID

Naibu Msajili wa vyama vya siasa nchini Sisty Nyahoza amekipongeza Chama Cha Siasa Cha Kijamii - CCK kwa kufanya Uchaguzi wa wazi na demokrasia wa kumchagua Mgombea Urais wa Tanzania bara na Zanzibar kupitia Chama hicho.

Katika Uchaguzi huo uliofanyia jijini Dar es salaam wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa Chama hicho wamepiga kura na kumchagua Mwenyekiti wa Chama hicho David Daudi Mwaijojele kuwa mgombea Urais kwa Tanzania Bara huku  Isha Salum akiteuliwa na Halmashauri kuu kuwa mgombea Pekee wa Nafasi ya Urais Kupitia Chama Cha CCK  Zanzibar.

Akizungumza kwenye mkutano huo Naibu Msajili wa vyama vya siasa Sisty Nyahoza amevisisitiza Vyama vya siasa nchini kueendelea kudumisha amani na kulinda umoja wetu wakati huu wa kuelekea uchaguzi ili nchi iweze kupita salama.

Nyahoza amesema mkutano huo umefanyika kwa sababu taifa lina amani na hivyo mtu yeyote mwenye nia ya kuvunja amani ni vyema akakemewa mapema.

‘Umoja wetu ndio unatufanya tuwe Pamoja hapa tukiwa wazanzibari na watu wa bara hivyo tulinde umoja wetu ili tfanye siasa kwa amani na utulivu’amesema Nyahoza

Kwa upande wake Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Kijamii cha CCK David Daudi Mwaijolele amesema kuwa wananchi watarajie makubwa pindi atakapofanikiwa kuitangaza mikakati mbalimbali wakati wa kampeni.

Amesema kuwa malengo yao ni kutaka kuhakikisha jamii ya kitanzania inaishi maisha bora katika maeneo mbalimbali ya kilimo ,uvuvi,ujasiriamali ikiwemo makundi maalum.

‘Chama cha CCK tutakapopewa ridhaa kupitia tume Tutahakikisha vijana wanaweza kujiajiri wenyewe pindi wanapomaliza elimu,lakini pia wanawake kunufaika na uchumi wao’amesema Mwaijolele

Naye Aisha Salum Hamadi ambaye amepitishwa kugombea nafasi ya Urais kupitia chama chake cha CCK Zanzibar amesema kuwa anajivunia kuwa mwanamke wa kwanza chama chake kumuamini kuiepeperusha bendera ya chama katika visiwa hivyo.

Amesema kuwa yupo tayari kukipambania chama cha CCK kwa Zanzibar ambapo vipaumbele vyake ni kuwasaidia watui wenye uhitaji wakiwemo walemavu.

Amewasisitiza watanzania kuwaonyesha mshikamano kwa kuwaunga mkono kukichagua chama chao ili kiweze kuwasaidi kuzitatua changamoto mbalimbali kwenye maeneo yao.

   

Listen Mkisi Radio