JSON Variables

Tuesday, May 6, 2025

WAZIRI MAVUNDE ATANGAZA KIAMA KWA KAMPUNI 95 ZA UCHIMBAJI MADINI

 


 ▪️Yatoa hati za makosa kwa kukiuka masharti ya Leseni

▪️Kampuni 7 tu kati ya 95 ambazo hazijaanza uchimbaji zimelaza mtaji wa Trilion 15 

▪️Zapewa siku 30 kujibu hoja


*Dar Es Salaam*

SERIKALI  imetoa Hati za Makosa kwa Kampuni  95 za Uchimbaji Mkubwa na wa Kati wa Madini kutokana na wamiliki wa leseni hizo kukiuka masharti ya Leseni  kama yalivyoainishwa kwenye Sheria ya Madini.

Akizungumza leo Mei 6, 2025 jijiini Dar es Salaam, Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde amesema kampuni hizo zinapaswa kujibu hoja ndani ya siku 30 la sivyo zitafutiwa leseni zao.

Hati hizo za makosa zimetolewa rasmi kuanzia Aprili 14, 2025 na muda wake utamalizika Mei 13 mwaka huu. 

 “Kama wanahoja walete majibu yao, tuyahakiki tukijiridhisha na hoja zao tutawaondolea makatazo kama hawana hoja tutawafutia leseni zao kwa  mujibu wa Sheria ya Madini Sura 123  ya  utoaji na ufutaji wa leseni za  madini na uchimbaji kifungu cha 63 na Kanuni zake, ambacho kinaeleza ukipewa leseni unapaswa uanze kazi ndani ya miezi 18.

Amesema, Serikali imetoa leseni kwa wachimbaji wa kati na wakubwa ambazo tangu kutolewa kwake hazifanyiwa kazi.

Zipo Kampuni tangu zimechukua leseni mwaka 2011 mpaka leo hazijaingiza hata koleo kwenye eneo miaka 14 sasa hazijaanza shughuli zozote, hatuwezi kuwa nchi ya namna hii.

Leseni 7 tu kati ya 95 ukiziweka pembeni zina mtaji wa Shilingi Trilioni 15 zimelala, sisi hatuwezi kuwa nchi ambayo  inatoa leseni kwa ajili ya kuchochea sekta ya madini kukua,halafu kuna watu wanachukua leseni wanakaa nazo hawafanyii kazi kwa kisingizio kuwa tupo kwenye mazungumzo na serikali  na sababu mbali mbali.

Leseni za madini zikitolewa zina masharti nyuma yake kwenye ile karatasi hakuna sharti linalosema mtu  ataanza uchimbaji wa madini nchini Tanzania akikamilisha mazungumzo na serikali, hiyo si sehemu ya sharti.

Masharti ni kwamba mwombaji anapopewa  leseni ni lazima aanze uchimbaji ndani ya miezi 18 vinginevyo awe na sababu ambazo zimeridhiwa na Waziri wa Madini kupitia Tume ya Madini, vinginevyo unapaswa kuanza uchimbaji ndani ya miezi 18.

Amesema na wale wote ambao  wamepata hati  ya makosa ambao wamejibu waende na barua ya ‘Commitment’ ya kueleza wataanza uchimbaji lini, ambao katika barua hiyo pia ikitokea ameshindwa kukidhi kile alichosema kwenye barua  sheria itafuata mkondo wake.

Kuna vitu kama nchi ni lazima tuchukue maamuzi magumu, hatuwezi kuifanya nchi yetu mtu anakuja anachukua leseni alafu akaitafutie mtaji, sheria inataka mtu yoyote anayekuja kufanya maombi ya leseni lazima atoe udhibitisho wa uwezo wa kifedha na kiufundi kabla ya kupata leseni,  sio nikupe ndio ukatafutie mtaji maana yake utakuwa umekiuka masharti ya sheri kwa kutoa taarifa ambazo sio sahihi wakati wa kuomba leseni.

Wale wote ambao hawatajibu ndani ya muda uliowekwa wasitegemee huruma yoyote, na wamekuwa ni mabingwa wakukimbilia mahakamani kuishtaki serikali katika hili Serikali imefuata taratibu zote kwa mujibu wa sheria inayowataka waliopata Leseni wote kufanya uendelezaji wa Leseni zao” Alisema Mavunde

Sekta ya Madini ni kati ya sekta zenye mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi hivyo shughuli za uchimbaji wa madini huchochea maendeleo makubwa ya kiuchumi.

RAIS MWINYI AKUTANA NA KAMATI YA AMANI YA VIONGOZI WA DINI ZANZIBAR

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi amekutana na Kamati ya Amani ya Viongozi  wa Dini Zanzibar kujadili Mustakabali wa Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba Mwaka  Huu.


Rais Dkt,Mwinyi ameihakikishia Kamati hiyo kuwa Serikali inafanya kila Juhudi Kuhakikisha Mifumo yote ya Uchaguzi inafanya Kazi kwa  Uhuru ,Amani na Uwazi  wakati wa Kampeni, Upigaji kura na Matokeo ya Uchaguzi kwa dhamira ya kudumisha Amani Iliopo kwa Maslahi ya Nchi.

Rais Dkt, Mwinyi ameishauri Kamati hiyo kuwakutanisha Wanasiasa kufanya Mjadala wa pamoja Kuzungumzia Umuhimu wa Amani ya Nchi pamoja na kudhibiti Viashiria  vya Uvunjifu wa Amani kabla na Baada ya Uchaguzi .


Aidha ameahidi   Serikali Kuendelea kushirikiana na Kamati hiyo ambayo imekuwa ikifanya  Kazi Muhimu ya Kuhubiri Amani tangu ilipoasisiwa Mwaka 2005.


Rais Dkt, Mwinyi amesema  Mshikamano wa Wananchi na Amani ni Tunu Muhimu kwa Mustakabali wa Maendeleo  ya Nchi.

Naye Mwenyekiti wa Kamati Hiyo Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kaab amesema Mkakati Wa Kamati Hiyo ni Kuhakikisha Mazingira ya Uchaguzi yanakuwa ya Amani wakati wa Uchaguzi, na baada ya Uchaguzi na Wananchi waingie katika Uchaguzi kwa Uwazi, Upendo na Furaha.


Kamati hiyo imemkabidhi Rais Dkt, Mwinyi   Kitabu Maalum cha Muongozo wa Viongozi wa Dini Kuhusu Uchaguzi.

DAY CARE ZATAKIWA KUSAJILIWA AMA TAFUTENI BIASHARA NYINGINE YA KUFANYA.

 

Mratibu wa Familia na Watoto kutoka Halmashauri ya Jiji la hilo,Christon Cletus, akizungumza na wamiliki na walezi wa watoto katika vituo vilivypo Ilala jijini Dar es Salaam leo wakati wa semina ya namna ya kupambana na ukatili kwa watoto.



NA MWANDISHI WETU



WAMILIKI wa vituo vinavyotoa huduma ya kulea watoto na masomo ya awali ‘Day Care’ wametakiwa kusajili vituo vyao la si sivyo watafute shughuli nyingine za kufanya.

Wito huo umetolewa leo Mei 5, 2025 jijini Dar es Salaam, Mratibu wa Familia na Watoto kutoka Halmashauri ya Jiji la hilo,Christon Cletus,  wakati akifungua semina ya siku tatu kwa wamiliki na walezi wa watoto wa vituo vya Wilaya ya Ilala.



Semina hiyo yenye lengo la kuwaelimisha watoa huduma hao wa malezi kwa watoto kukabilana na changamoto ya ukatili, imeratibiwa na Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stad, Furahika kilichopo Buguruni Malapa, Ilala jijini Dar es Salaam.

“Nikiangalia mmejitokeza kwa wingi lakini kwa uzoefu wangu nikiwaangalia hapa, nagundua waliosajili vituo vyao hawazidi wawili na sijajua kuna ugumu gani, hivyo natoa wito kwa wale ambao bado hawajasajili kuwasaliana na Ofisa Ustawi husika ili kupata utaratibu na kusajili.


“Mnaposajili inakuwa rahisi kuwafikia inapotokea miradi mbalimbali ya maendeleo na hata inapotokea unyanyasaji kwa kituo furani inakuwa rahisi pia kufika na kuchukua hatua stahiki, naamini wasio sajiliwa baada ya mafunzo hayo watafuata utaratibu na kukamilisha mchakato huo,” amesema.


Pia alimpongeza Mkuu wa Chuo hicho kwa jitihada za kupambana na ukatili wa watoto na kumtaka hasiishie kwa Wilaya ya Ilala pekee bali afanye semina kama hiyo kwa mkoa wote wa Dar es Salaam ili kuwafikia walimiki na walezi wengi.


Naye Kaimu Mkuu wa Chuo Cha Furahika, Dkt David Msuya amewasistiza washiriki wa semina hiyo kuhakikisha baada ya mafunzo hayo wanakwenda kuwa mabalozi wazuri watakaosaidia kuwajenga watoto katika misingi bora na kuwa na kizazi imara kitakachojenga taifa imara siku za usoni.


Kuna baadhi ya vituo kuna mambo mengi mengi mabaya ya unyanyasaji watoto ambayo yanafanywa wakati mwingine kwa kutojua misingi ya malezi na hiyo inakuja kutokana na kuajiri baadhi ya watumishi wasiokuwa na elimu.


Naamini baada ya mafunzo hayo mambo yatabadilika unyanyasaji utapungua kama si kuundosha kabisa na hapo tutakuwa tumeunga mkono Serikali kwa vitendo katika kupambana na ukatili wa watoto hususan katika  baadhi ya vituo vya ‘Day Care’, amesema.     


Joyce Mndima mshiriki kutoka, Mish Day Care, kilichopo Kata ya Buguruni, amesema anaamini baada ya mafunzo hayo ya siku tatu watatoka na uelewa wa kutosha namna ya kulea watoto toafuti na awali.

“Nashukuru kwa mafunzo hayo kwa maana yatatusaidia kuwalea watoto vizuri na tunakwenda kuwa mabalozi wazuri,” amesema. 

ASEMA MBETO "CCM ITAHESHIMU NA KUFUATA USHAURI BILA KUVUNJA KATIBA NA SHERIA "


Mwandishi  Wetu, Zanzibar 


Chama Cha Mapinduzi  kimesema kwa miaka yote  kimepokea , kusikiliza na kutekeleza Ushauri  wa Wazee, watu  mbalimbali , Viongozi wa Dini na  Kijamii  bila kukiuka  matakwa ya Katiba na Sheria. 


CCM na serilali  zake huendesha utawala bila  kuingilia mipaka ya Sheria  huku kikiheshimu madaraka ya  Serikali,  Bunge  na Mahakama.


Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC Zanzibar,  Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis  Mbeto  Khamis , ameeleza hayo alipotakiwa  kutoa maoni yake kufuatia ushauri uliotolewa na  Waziri Mkuu  Mstaafu  Joseph  Warioba.


Mbeto alisema  Serikali  haziwezi kuzuia Uhuru wa mawazo  ya watu na ushauri wa Wazee, lakini akawataka wanaoshauri  ,  watambue  kuna mahali  unapoishia ushauri  wao.


Alisema  kupokea ushauri  si kosa ila kosa huweza kuwa  makosa zaidi  aidha  katika utekelezaji wa Ushauri  huo    usiokiuka na kuvunja Sheria, Katiba au kuingilia  madaraka ya mihimili mingine. 


'Ushauri  wa Wazee utabaki kuwa sehemu ya utamaduni  wa Serikali  za CCM. Kama Taifa tumefika mahali  tulipo kwa  kuthamini michango  na ushauri  wa Wazee . Kila jambo lina kipimo na mipaka ya utekelezaji wake  " Alisema  Mbeto .


Katibu huyo  Mwenezi  aliongeza kusema , kupokea ushauri   wowote , lazima anaeshauri na anayeshauriwa wote  walitazame  suala husika kama lipo kisheria , lina ugumu na wepesi  upi  ,  kwakuwa  kila hatua, inahitaji kutekelezwa kwa umakini na tahadhari. 


"Mwalimu Julius  Nyerere  alitoa  msamaha kwa Wafungwa wa Kesi ya uhaini baada ya Mahakama kuhukumu  kisheria.  Rais hakuingilia kesi wakati  ikiwa   Mahakamani. Alifanya hivyo kwa kuheshimu dhana ya  mgawanyo wa Madaraka "Alieleza  


Mbeto  alisema katika Kesi  ya kina Michael  Kamaliza na wenzake    , alikuwemo  Mpigania Uhuru  Mstari  wa mbele wa TANU , Titi Mohamed lakini Rais kwanza  aliheshimu Sheria na Mhimili wa Mahakama.


Aliongeza kusema    ikiwa leo Viongozi  aidha wa CCM, ACT , Chadema ,  Chauma na vingine, ikitokea kuvunja sheria,  kisha  yaanze  mazungumzo ya  usuluhishi, itakuwa kila anayevunja sheria lazima iwepo meza ya mazungumzo , huko si katika kuheshimu dhana ya  Utawala wa  Sheria.


"Meli, Jahazi au Ngarawa zinapita majini .Ukiona vyombo hivyo vinasafiri Nchi Kavu au Angani  huo ni uchuro. Sheria lazima  ifuate mkondo   wake. Iwe kwa Wazee  , Wanasiasa au Viongozi  wote tutumie hekima kila  tunaposhauri" Alieleza.


Kadhalika Mbeto  alisema katika Awamu ya Tano ya Utawala kulikuwa na  baadhi ya mambo kadhaa yalioonekana kuwa magumu lakini hawakutokea

Wazee waliokuwa na ujasiri  na  kushauri lolote .

NYAMGUMA MAHAMUD AIBUKA MSHINDI HABARI ZA NISHATI SAFI YA KUPIKIA


๐Ÿ“ŒNi kupitia Tuzo za Uandishi wa Habari za  Samia Kalamu Awards

๐Ÿ“ŒWizara ya Nishati yatambua mchango wake

๐Ÿ“Œ Yamzawadia fedha taslimu, jiko linalotumia umeme kidogo, kompyuta mpakato na uniti za umeme za mwaka mmoja

๐Ÿ“Œ Mhandisi Mramba asema Tuzo ni kielelezo cha kuunga mkono juhudi za Rais Samia uhamasishaji Nishati Safi ya Kupikia.

Nyamguma Mahamud, Mwandishi wa Habari  kutoka Mlimani FM ameibuka kidedea katika Tuzo za Uandishi wa Habari za Samia Kalamu Awards 2025 kupitia kipengele cha habari za Nishati Safi ya Kupikia ambapo Wizara ya Nishati imetambua mchango wake kwa kumpa zawadi mbalimbali ili kuendelea kuhamasisha utoaji wa elimu ya Nishati Safi ya Kupikia.

Hafla ya utoaji wa Tuzo hizo imefanyika jijini Dar es Salaam huku mgeni rasmi akiwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mohamud amekabidhiwa zawadi zake na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba kwa niaba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko.

Mshindi huyo amekabidhiwa fedha taslimu shilingi milioni tano, kompyuta mpakato, jiko linalotumia umeme kidogo na uniti za umeme za mwaka mzima.

"Tunatambua  masuala aliyoyaandika katika kuhamasisha nishati safi ya kupikia, kwahiyo tumemzawadia pia jiko la umeme la kisasa linalotumia umeme mdogo pamoja na umeme wa kutumia nyumbani kwake kwa mwaka mmoja," amesema Mha. Mramba

Amesema Tuzo ya Nishati Safi ya Kupikia ni kielelezo cha  kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika  kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Samia Kalamu Awards  imeandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikiwa na kaulimbiu ya "Uzalendo Ndio Ujanja'









 

Monday, May 5, 2025

BASHUNGWA APONGEZA JESHI LA POLISI, KWA KUMKAMATA MTUHUMIWA WA VITISHO DHIDI YA PADRI KITIMA.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa, amelipongeza Jeshi la Polisi kwa juhudi zake katika kufuatilia na kuchukua hatua dhidi ya matukio mbalimbali ya kihalifu, ikiwemo tukio la kukamatwa na kuhojiwa kwa mtu anayetuhumiwa kutoa ujumbe wa vitisho kabla ya shambulio dhidi ya Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Dkt. Charles Kitima.

Bashungwa alitoa pongezi hizo leo, Mei 5, 2025, mara baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Jumanne Muliro, kuhusu hatua zinazochukuliwa na Jeshi hilo kufuatia matukio mbalimbali ya kihalifu.

“Nimepata taarifa za kukamatwa na kuhojiwa kwa aliyetoa vitisho kabla ya tukio la kushambiliwa la Padri Kitima. Nalipongeza Jeshi la Polisi kwa jitihada  mbalimbali zinazoendelea za ufutiliaji wa matukio mbalimbali yaliyotokea” amesema Waziri Bashungwa.

Aidha, Waziri Bashungwa amelielekeza Jeshi la Polisi kuendelea na msako dhidi ya washukiwa wa matukio yote ya kihalifu na kuhakikisha wanachukuliwa hatua kali za kisheria kwa haraka.

BALOZI KAGANDA AHIMIZA USHIRIKIANO KWA WATUMISHI WA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI ZIMBABWE

 

Mwandishi Wetu Harare Zimbabwe.

Balozi wa Tanzania Nchini Zimbabwe Mheshimiwa Suzan Kaganda, amewasili Nchini humo tayari kuanza majukumu yake katika Balozi hiyo huku akiwaomba watumishi kushirikiana ili kutimiza azima ya viongozi wa Nchi hizo mbili katika masuala mbalimbali.

Ametoa kauli hiyo leo Mei 05, 2025, Jijini Harare wakati alipowasili kwa mara ya kwanza na alipofanya kikao na maafisa kutoka ubalozi wa Tanzania nchini Zimbabwe ambapo amesisitiza kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuleta ufanisi na tija kwa mataifa hayo.

Balozi Kaganda ameongeza kuwa, matarajio ya viongozi wakuu wa Tanzania na Zimbabwe wanategemea kuona Balozi hizo zinaleta matokeo chanya na kutangaza fursa zilizopo katika nchi hizo.

Vilevile amesisitiza kuwa, ni vyema kudumisha umoja uliopo baina ya maafisa katika kutekeleza sera ya Mambo ya Nje.

Friday, May 2, 2025

UJENZI WA DARAJA LA JPM UMEFIKIA 99% KUKAMILIKA MWANZA

 

Mradi mkubwa wa ujenzi wa Daraja  la JPM linalounganisha wilaya ya Misungwi na wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza umefikia asilimia 99  ili kuweza kukamilika .

Hayo yamesemwa na msemaji mkuu wa Serikali Greyson Msigwa mara baada ya kufanya ziara katika Daraja hilo na kujionea hatua ya ujenzi iliyofikiwa ambapo kwasasa yamebakia marekebisho madogo ili kukamilika

Msigwa pia amesema kuwa daraja hilo litakuwa na uhai wa miaka mia moja ambapo siku nyingi litaanza kufanya kazi ili kuondoa changamoto ya wananchi kusubiri kivuko kwa muda mrefu


Aidha kwa upande wake Msimamizi wa Mradi wa ujenzi huo Mhandi Wiliam Sanga kutoka Tanroad amesema kuwa tangu kuanza kwa ujenzi   wa  mradi huo jumla ya ajira 33505 ambapo wazawa ni asilimia 91.9 ambapo mpaka sasa wamemlipa mkandarasi shilingi Bilioni 539 . 

Katika ziara hiyo ya Msemaji mkuu wa serikali ametembelea na kukagua pia mradi wa ujenzi wa vivuko 5 vinavyojengwa na Songoro Marine pamoja ujenzi wa meli ya Mv Mwanza.