JSON Variables

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Jumapili, 11 Mei 2025

CHARLES HILLARY AFARIKI DUNIA LEO ALFAJIRI


Msemaji Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Znz ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais wa Zanzibar Charles Hillary, amefariki alfajiri ya leo May 11 2025 katika Hospitali ya Muhimbili Mloganzila, alikokuwa akipatiwa matibabu.


Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar Mhandisi Zena Ahmed Said, amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kutoa pole kwa Familia, Ndugu, Jamaa na Marafiki wote walioguswa na msiba huu.

Charles Hillary ni miongoni mwa Watangazaji bora wa Redio na Televisheni Nchini Tanzania ambaye amefanya kazi katika vituo mbalimbali vya ndani na nje ya Tanzania ikiwemo Radio One 

Jumamosi, 10 Mei 2025

Rais Mstaafu Dkt. JM Kikwete pamoja na Mkewake wahani msiba wa Hayati Cleopa Msuya.

 


RIAS Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Mkewake wahani msiba wa Hayati Cleopa Msuya, Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu nyumbani kwake Upanga Jijini Dar es Salaam leo 10 Mei, 2025.


Dkt. Kikwete ameungana na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa pamoja na waombolezaji wengine.



DINI ZINA MCHANGO MKUBWA KATIKA KUIMARISHA USTAWI WA JAMII


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema madhehebu ya dini yana mchango mkubwa katika kuimarisha ustawi wa jamii na kutoa huduma za kiroho.

 

Amesema kwa kutambua hilo, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wote amekuwa akitekeleza kwa vitendo dhamira ya kukuza ushirikiano kati ya Serikali na madhehebu ya dini.

 

Amesema hayo leo Jumamosi (Mei 10, 2025) alipomuwakilisha Mheshimiwa Dkt. Samia katika kilele cha dua maalum ya kuombea viongozi wa Kitaifa, amani, uchaguzi mkuu pamoja na kuwaombea mamufti na masheikh waliotangulia mbele za haki, kwenye Viwanja vya Msikiti wa Mohammed VI, Kinondoni Dar es Salaam.

 

“Ni ukweli usiopingika sote tumeshuhudia kuwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jinsi gani anawathamini, anawasilikiza na kuwashirikisha viongozi wa madhehebu ya dini katika masuala muhimu ya kitaifa”.

 


Kadhalika Mheshimiwa Majaliwa amempongeza Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir bin Ali Mbwana kwa kuandaa dua hiyo kwa ajili ya baraka na amani ya Tanzania wakati wa uchaguzi mkuu.

 

“Nikiri kwamba Serikali inatambua umuhimu wa sala na dua. Viongozi tunatekeleza majukumu yetu kwa salama kwa kuwa viongozi wetu wa dini na waumini wote mnatuombea dua. Hii ndiyo sababu Serikali imekuwa ikishirikiana na madhehebu ya dini katika shughuli zake.”


Ameongeza kuwa Serikali inathamini kazi kubwa inayofanywa katika maeneo mbalimbali hususan katika kutoa huduma za kijamii na hivyo kuchangia kasi ya maendeleo ya Taifa letu. “Huduma hizo ni pamoja na zile za elimu, afya, maji, nishati, mafunzo kuhusu kilimo bora na ufugaji, na huduma nyingine mbalimbali.”

 

Naye, Mwenyekiti wa Kamati ya dua hiyo Kitaifa Hajati Mwamtumu Mahiza amesema kuwa dua hiyo ni kwa ajili ya kuwaombea masheikh na Mamufti walioleta mchango chanya katika dini ya kiislamu.

 

Amesema kuwa dua hiyo ambayo imefanyika kwa siku tatu ililenga kuombea viongozi wakuu wa nchi na wote wanaoingia kwenye mchakato wa uchaguzi pamoja na kuombea amani nchini,

 

“Tunahitaji kuwa wanyenyekevu kwa Mwenyezi Mungu kwa sababu anasema katika Quran kuwa niombeni nami nitawapa, tunataka kuingia kwenye uchaguzi mkuu na kutoka tukiwa salama na wamoja”.

 

RAIS MWINYI AZINDUA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amezindua Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia na kuiagiza Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais – Katiba, Sheria na Utawala Bora kutenga fedha maalum kwa ajili ya utekelezaji endelevu wa kampeni hiyo.


Amesema ili kufanikisha kampeni hiyo, ni muhimu kuandaa mkakati madhubuti wa kutafuta rasilimali fedha, nyenzo, na utaalamu, ili kufikia lengo la kuwafikishia wananchi wengi huduma za msaada wa kisheria kote nchini.


Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo katika Uwanja wa Donda, Mtende, Mkoa wa Kusini Unguja.


Aidha, amezitaka wizara zote mbili zinazoshughulikia masuala ya sheria kuongeza ushirikiano, kufanya kazi kwa ukaribu, na kubadilishana uzoefu ili kufanikisha kampeni hiyo.


Ameeleza kuwa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ni nguzo muhimu ya kuimarisha utawala bora, upatikanaji wa haki na kichocheo cha amani, utatuzi wa migogoro, utulivu, na ustawi wa jamii.


Rais Dkt. Mwinyi pia amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa maono yake ya mbali, huruma, na upendo kwa Watanzania, kwa kuanzisha kampeni hiyo inayolenga kutoa huduma za sheria kwa wananchi wasio na uwezo wa kupata huduma hizo kwa njia ya kawaida, ameahidi kuziunga mkono kikamilifu juhudi hizo.


Amesisitiza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuimarisha utawala wa sheria kupitia ujenzi wa mahakama saba za mikoa na mbili za wilaya, ambapo tano ni za mikoa na mbili ni za wilaya.


Vilevile, kupitia Mradi wa Maboresho ya Mahakama, Serikali inalenga kuongeza ufanisi katika utendaji wa mahakama na kuhakikisha wananchi wanashirikishwa kikamilifu katika mchakato wa upatikanaji wa haki, sambamba na kuongeza rasilimali watu.


Mwisho, Rais Mwinyi ametoa wito kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika kampeni hiyo, hususan kwa wale wenye malalamiko yanayohusu udhalilishaji wa kijinsia, mirathi, na masuala ya wanawake na watoto.


Kampeni hii ya msaada wa kisheria ni mpango wa miaka mitatu unaolenga kuwafikia wananchi katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar.

WAZIRI MAVUNDE: MGODI WA MAGAMBAZI WILAYANI HANDENI KUANZA KAZI JULAI 2025


◾️ Kampuni ya kuendeleza mgodi kupatikana mwezi wa 5 mwishoni


◾️ Wananchi wamshukuru Rais Samia kwa kusimamia kuanza tena kwa shughuli za Mgodi Magambazi


▪️Wilaya ya Handeni kuongeza mapato zaidi


▪️Waziri Mavunde asisitiza ajira kwa wananchi wanaouzunguka Mgodi


📍Handeni, Tanga


Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, ameeleza kuwa Mgodi wa Kati wa Dhahabu wa Magambazi uliopo Wilayani Handeni Mkoani Tanga utaanza kufanya kazi rasmi ifikapo Julai 2025 na unatarajiwa kuleta tija kwa kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika Kijiji cha Nyasa na Wilaya ya Handeni kwa ujumla.


Waziri Mavunde ameeleza hayo leo Mei 10, 2025, wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Nyasa, Kata ya Kang’ata, Wilaya ya Handeni, ambapo amekuja kuleta mrejesho wa ahadi aliyotoa Aprili 6, 2025 kuhusu hatma ya uendelezaji wa mgodi huo uliosubiriwa kwa muda mrefu.

“Tunamshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maelekezo yake kuhakikisha Mgodi huu wa Magambazi unaanza kufanya kazi na kuwainua wananchi wa hapa na mnyororo mzima wa shughuli za maendeleo.


Baada ya kuchukua hatua ya kupata muafaka wa kuhakikisha mgodi huo unaanza kufanya kazi, Kampuni nyingine ya tatu itateuliwa ndani ya siku 14 kuanzia Mei 12 hadi Mei 26, ambayo itaungana na Kampuni za PMM na East African Metals/CANACO ili kuendesha mgodi huo.

Kipekee nawashukuru sana wananchi wa Nyasa kwa uvumilivu wenu, hili jambo lilikuwa la muda mrefu tangu tumeanza kulifanyia kazi, mlikubali kukaa hapa na kunyeshewa na mvua, na leo mmekuja tena na kukubali kukaa nami kwenye mvua ili kuwapa mrejesho wenu.


Kampuni zinazoendesha mgodi huo kuhakikisha zinatoa kipaumbele kwa wakazi wa Nyasa katika ajira ili wananchi wa Nyasa wanufaike moja kwa moja na uwepo wa mgodi huo katika Kijiji chao.


Faida zitakazopatikana ikiwa ni pamoja na kuinua mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, uboreshaji wa miundombinu ya afya, elimu, barabara na mengine kupitia Wajibu wa Kampuni kwa Jamii (CSR) pamoja na ushiriki wa Watanzania katika mgodi huo kwa kutoa huduma na kuuza bidhaa (Local Content)”amesema Mavunde

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Handeni, Mhe. Amiri Changogo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Japhari Kubecha, na Mbunge wa Handeni Vijijini, Mhe. John Sallu, wamemshukuru Waziri Mavunde kwa kufanyia kazi suala hilo na hatimaye kuondoa kiu ya muda mrefu ya wananchi wa Nyasa na Handeni kwa ujumla.


Naye, Wakili Albert Msando (aliyekuwa Mkuu wa Wilaya Handeni, hivi sasa ni Mkuu wa Wilaya Ubungo) ameeleza hisia zake za kufurahishwa na hatua hiyo kwani alikuwa akilisimamia kwa ukaribu kipindi akiwa Mkuu wa Wilaya hiyo na kwamba hana deni na wananchi wa Kata ya Kang’ata na Kijiji cha Nyasa baada ya kutatuliwa kwa changamoto hiyo iliyokuwa inawakabili kwa muda mrefu.

RC CHALAMILA AZINDUA MPANGO WA KUFANYA BIASHARA SAA 24 WILAYA YA UBUNGO

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amezindua mpango wa ufanyaji biashara kwa saa 24 kwenye soko la Mbezi eneo la stendi ya Malamba Mawili wilayani Ubungo na kuwahakikishia usalama wafanyabiashara huku akiwataka maafisa biashara kutowaonea wafanyabiashara


Akizungza wilayani Ubungo Jijini Dar es salaam katika uzinduzi huo uliofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye soko la mbezi mbele ya mamia ya wafanyabiashara wa Soko hilo waliokusanyika kumsikiliza Mkuu wa Mkoa huyo amesema jiji hilo ni kitovu cha biashara inayochagizwa na uwepo wa bandari,kituo cha mabasi cha Magufuli na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl Nyerere hivyo hakuna sababu ya kulala


Aidha RC Chalamila amewataka wafanyabiashara kutohofia usalama wao kwani Serikali Mkoani humo inazidi kuimarisha ulinzi na usalama ili jiji hilo liwe na amani zaidi huku akimuagiza mkuu wa wilaya ya Ubungo kutoruhusu maafisa biashara kuwaonea wafanyabiashara hao kwani vitendo hivyo ni kinyume na utaratibu


Hata hivyo RC Chalamila ametumia nafasi hiyo kuitaka Halmashauri ya Ubungo kutengeneza vizimba vya mfano vya kufanyia biashara ambapo ametoa muda wa wiki moja kukamilisha kazi hiyo ili wafanyabiashara wenyewe watengeneze vizimba vyao


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Wakili Albert Msando amewahakikishia usalama wafanya biashara, madereva pamoja na wananchi huku Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Hassan Mkwawa akiwahakikishia kuwa pamoja na taa zilizofungwa kwenye maeneo mengi wataendelea kuweka taa za kutosha ili biashara ifanyike saa 24 kwa ufanisi


Shamra shamra za uzinduzi huo zimefanyika usiku mzima hadi asubuhi huku jukwaa likipendezeshwa na wasanii mbalimbali pamoja na Rdj kutoka Efm redio amkiambatana na MC Pilau kutoka Efm.

DKT. MWIGULU AWATAKA WATUMISHI WA WIZARA YA FEDHA KUZINGATIA MISINGI YA KAZI NA UTAWALA BORA

 

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amewataka Watumishi wa Wizara ya Fedha, kutekeleza majukumu yao ya kila siku kwa kuzingatia misingi ya kazi na utawala bora ili kuepusha malalamiko yasiyo na lazima kutoka kwa wadau wake wakiwemo wananchi.


Mhe. Dkt. Nchemba alisema hayo wakati akifungua Mkutano wa 38 wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Fedha, lililofanyika katika katika Kituo cha Mikutano cha APC, kilichoko Bunju mkoani Dar es Salaam.


Aidha, Mhe. Dkt. Nchemba aliutaka Uongozi wa Wizara kumchukulia hatua stahiki kwa mujibu wa taratibu mtumishi yeyote atakayebainika na kuthibitika kwenda kinyume na misingi ya maadili katika utendaji kazi ili kulinda heshima ya Wizara.


‘’Ninatambua kwamba mnafahamu misingi ya utendaji kazi katika utumishi wa umma, hivyo, si jambo jema kusikia mtumishi yeyote wa Wizara ya Fedha anakiuka misingi ya utawala bora katika utumishi wa umma’’, alisema Mhe. Dkt. Nchemba.

Pia, Mhe. Dkt. Nchemba aliwapongeza watumishi wote wa Wizara hiyo kwa kazi na mchango wao moubwa uliofanikisha majukumu yake ya kuismamia uchimi wa nchi na kuwezesha upatikanaji wa Fedha zinazotumika kutekeleza miradi mbalimbali ya kiuchumi na kijamii.


Aliwataka Watumishi wa Wizara kuendelea kufanyakazi kwa ushirikiano kati ya Watumishi ndani ya Idara, Wizara na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Fedha, na kuzielekeza Taasisi kutekeleza majukumu yao ya msingi kama inavyoratajiwa na Serikali pamoja na wadau wengine.


Mhe. Dkt. Nchemba aliongeza kuwa kutokana na Uwekezaji mkubwa uliofanywa na Wizara katika kuwapatia mafunzo Watumishi wake, hivyo ni lazima matokeo ya mafunzo hayo yaonekane kwa vitendo kupitia utendaji wa kila mtumishi, na kusisitiza umuhimu wa Watumishi kuendelea kupatiwa mafunzo ya mara kwa mara ili kuboresha utendaji na kuendana na kasi ya mabadiliko ya teknolojia.

Awali, akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mwenyekiti wa Baraza hilo la Watanyakazi ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, alisema kuwa lengo kuu la Baraza la Wafanyakazi ni kuwashirikisha Wafanyakazi katika utekelezaji wa shughuli za Wizara kwa kushirikiana na Uongozi ikiwa ni pamoja na kuishauri Wizara juu ya ufanisi wa kazi na hatua zinazofaa kuchukuliwa ili huduma zinazotolewa na Wizara zikidhi matarajo ya wateja.


Dkt. Mwamba aliongeza kuwa katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2024/25, Wizara imepata mafanikio mbalimbali yakiwezo kupandishwa vyeo kwa Watumishi 484 wa kada mbalimbali na kulipa jumla ya shilingi 521,980,765/= yakiwa ni malimbikizo ya mishahara kwa Watumishi wa Wizara.


‘’ Aidha, katika mwaka wa fedha 2024/25 Serikali imeshatoa kibali ili watumishi wenye sifa waweze kupandishwa vyeo. Uchambuzi wa awali umebaini kwamba watumishi 313 wana sifa za kupandishwa vyeo’’ alisema Dkt. Mwamba.

Dkt. Mwamba aliongeza kuwa Mkutano wa 38 wa Baraza la Wafanyakazi ni mwendelezo wa mikutano mingine ambayo imekuwa ikifanyika kila mwaka ambapo kupitia mikutano hiyo wajumbe wamekuwa wakitoa maoni na mapendekezo ambayo yamesaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha maslahi ya watumishi na utendaji kazi wa Wizara.


Mkutano wa 38 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha, umekutanisha Wajumbe kutoka Makao Makuu ya Wizara, Wakuu wa Hazina Ndogo na Wahakikimali kutoka Mikoa yote ya Tanzania Bara.

Kongamano la Kimataifa la 18 la Elimu Mtandao kwa Afrika lafikia kilele, Mhe. Zainab Katimba (Mb) Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi (Elimu) akishiriki katika kilele hicho.

 

Mhe. Zainab Katimba (Mb) Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI (ELIMU)  tarehe 9 Mei, 2025 amehudhuria kilele cha Kongamano la Kimataifa la 18 la Elimu Mtandao kwa Afrika ‘eLearning Africa’ ambapo Mgeni rasmi alikuwa Mhe. Hemed Abdulla Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akimwakilisha Mhe Dkt. Hussein Mwinyi, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.


Mhe. Hemed Abdulla amewataka washiriki wote kuendelea kuunga jitihada za pamoja katika kukuza matumizi ya TEHAMA katika elimu kwa mustakabali wa Tanzania na nchi nyingine za Afrika. Aidha, amewaalika wafanyabiashara, wawekezaji na taasisi kuja kuwekeza na kuongeza wigo wa ushirikiano Tanzania Bara na Zanzibar katika teknolojia ya digiti hususani elimu na biashara.

Listen Mkisi Radio